FIFA kutoa Bilioni 1.1 kwa kila mwanachama, Hatutakubali upigaji TFF

OKW BOBAN SUNZU

Platinum Member
Joined
Aug 24, 2011
Posts
53,868
Reaction score
121,001
SHIRIKISHO la Soka Tanzania (TFF) litapokea takribani kiasi cha fedha Dola 500,000 (Sh 1.1 bilioni) kutoka Shirikisho la Soka Duniani (FIFA) ili kusaidia uendeshaji wa shughuli za kimpira.

Fedha hizo ni sehemu ya mgawo wa takribani Dola 150 milioni (Sh 347 bilioni) ambao FIFA watautoa kwa nchi 211 ambazo ni wanachama wa shirikisho hilo.

Rais wa FIFA, Gianni Infantino amesema kuwa watahakikisha fedha hizo zinagawiwa haraka ili kusaidia wanachama wake kuendesha shughuli za kimpira wa miguu katika kipindi hiki ambacho idadi kubwa ya mashindano yamesimama kutokana na tatizo la kusambaa kwa virusi vya corona duniani.

"Ugonjwa huu umesababisha mabadiliko ambayo hayakutegemewa katika jumuiya ya mpira wa miguu na kama chombo kinachosimamia soka, ni jukumu la FIFA kuwa pamoja na kusapoti wale wenye mahitaji makubwa.

"Hii inaanzia kwa kutoa msaada wa haraka wa kifedha kwa vyama wanachama wetu ambao wengi wanakabiliwa na hali ngumu ya kiuchumi katika kipindi hiki," amesema Infantino.

My Take

Tunawaonya TFF kujiepusha na upigaji wowote. Fedha zitumike inavyotakiwa kwa maslahi ya soka letu.
 
Jamal Malinzi kampeni yake alianzia hili jukwaa,alipopata urais akasusa,alipokosolewa humu akaanza kukashimu JF
alikimbia JF bila kuaga. Kabla ya kudakwa alitushutumu JF tunamkashifu. kiko wapi

♡♤Life belongs to all who struggle for it♤♡♧
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…