Fikra pevu. Tanua ufahamu wako

Fikra pevu. Tanua ufahamu wako

Raia Fulani

JF-Expert Member
Joined
Mar 12, 2009
Posts
11,478
Reaction score
3,659
Nimeona nianzishe uzi wenye mada za kufikirisha katika maandishi na kudadavua maana ya maandishi yenyewe. Kwa kuanza naanza na mada ya njaa.


Ni nadra kutokukubali kuwa kuna uhaba wa njaa ulimwenguni. Upembuzi anuai unaweza bainisha hili. Njaa ni hulka. Ni fursa ya mja kujiainisha kihisia mbele ya jamii kimahitaji. Njaa ya fikra na njaa ya mwili zote njaa. Fikra ni sehemu ya mwili usio na shibe. Kutokujua kuwa hujui unahitaji nini ni njaa. Fikra si tendo la hiari, ila unapotaka kuanza kuwaza kufikiri ni wazi kuwa wazo lililotunga kuwaza kufikiri linatokana na ombwe la sintofahamu katika mfumo wa ufahamu. Kuwaza ni suala mtambuka kama ilivyo kupambana na njaa. Tamaa ni upungufu wa shibe ya hisia. Tamaa si hulka bali ni matokeo ya hulka. Njaa inaonekana, inasikika, inahisiwa. Si sahihi kusema kuwa njaa si nzuri. Njaa ni heri. Njaa ni amani. Njaa ni silaha. Lakini pia njaa ni janga. Nini njaa yako?
 
Nina njaa ya chapaa ya kunivusha kigamboni kaka
 
Njaa kama njaa mara nyingi ni neno ambalo hutupeleka moja kwa moja kwenye fikra ya kitendo cha mwanadamu kukosa chakula kwa mda mrefu... kupata hamu ya kula, kusikia mwili (tumbo na kinywa) kikidai kupata kula na hatimae kutaka hicho chakula by any means tokana na jinsi ambavo wajisikia wataka kula.

Tokana na post yako ya jinsi ninavoweza ona njaa.... Njaa kwangu ni ile hali ya mwanadamu kua na hisia ya kutaka kidhi hitaji lake kwa kiwango ambacho ni sahihi ama atakacho. Yategemea hitaji lake ni nini hasa ili kuweza jua kama ataweza kidhi ama lah... Kuna hitaji ambalo akisha kidhi anakua kisha maliza tatizo lake la uhitaji kwa mda mrefu na kuna hitaji ambalo hata akikidhi inakua tu kakidhi kwa mda mfupi hata kama katosheka kwa mda huo.

Mfano njaa ya kutaka kua na elimu. Mhusika aweza kua na njaa ya kufika shahada ya kwanza na akajua kabisa kua atatosheka na hio shahada. However with time aja kugundua kua tatizo (njaa) yake ya awali imerudi kwa kutaka kukidhi kwa kupata shahada ya pili.
 
Njaa kama njaa mara nyingi ni neno ambalo hutupeleka moja kwa moja kwenye fikra ya kitendo cha mwanadamu kukosa chakula kwa mda mrefu... kupata hamu ya kula, kusikia mwili (tumbo na kinywa) kikidai kupata kula na hatimae kutaka hicho chakula by any means tokana na jinsi ambavo wajisikia wataka kula.

Tokana na post yako ya jinsi ninavoweza ona njaa.... Njaa kwangu ni ile hali ya mwanadamu kua na hisia ya kutaka kidhi hitaji lake kwa kiwango ambacho ni sahihi ama atakacho. Yategemea hitaji lake ni nini hasa ili kuweza jua kama ataweza kidhi ama lah... Kuna hitaji ambalo akisha kidhi anakua kisha maliza tatizo lake la uhitaji kwa mda mrefu na kuna hitaji ambalo hata akikidhi inakua tu kakidhi kwa mda mfupi hata kama katosheka kwa mda huo.

Mfano njaa ya kutaka kua na elimu. Mhusika aweza kua na njaa ya kufika shahada ya kwanza na akajua kabisa kua atatosheka na hio shahada. However with time aja kugundua kua tatizo (njaa) yake ya awali imerudi kwa kutaka kukidhi kwa kupata shahada ya pili.

Asha nimependa ufafanuzi wako. Njaa yaweza kuwa ni tendo la muda mfupi ama mrefu. Njaa ya hisia na fikra zaweza tofautiana. Njaa ya hisia inahusisha mwili zaidi. Njaa ya fikra inahusisha vilivyo zaidi ya mwili, kama elimu, kujitambua, maendeleo n.k. Katika mfano wako nimepata kitu kingine kuwa jamii inatengeneza njaa. Kwamba shibe (elimu) yangu ya awali haikidhi tena hitaji langu la sasa. Na njaa ya hisia ni zaidi ya tumbo. Wawezaje kuzungumzia kuwa njaa ni heri?
 
Asha nimependa ufafanuzi wako. Njaa yaweza kuwa ni tendo la muda mfupi ama mrefu. Njaa ya hisia na fikra zaweza tofautiana. Njaa ya hisia inahusisha mwili zaidi. Njaa ya fikra inahusisha vilivyo zaidi ya mwili, kama elimu, kujitambua, maendeleo n.k. Katika mfano wako nimepata kitu kingine kuwa jamii inatengeneza njaa. Kwamba shibe (elimu) yangu ya awali haikidhi tena hitaji langu la sasa. Na njaa ya hisia ni zaidi ya tumbo. Wawezaje kuzungumzia kuwa njaa ni heri?


Asante kwa acknowledgement of my post.... Hapo bold hapo.... Nawezaje zungumzia kua njaa ni heri....

Wanadamu tumetofautiana saaana. Kama unavoelewa katika jamii yetu familia nyingi tumejijengea kula milo mitatu kwa siku; Yaani asubuhi mchana jioni.... Katika familia moja kuna ambae yeye lazima ale mda wa mlo ukifika iwe ana njaa ama Lah! Kuna mwingine yeye mlo ni pale ataposikia njaa regardless kua chakula kimeandaliwa mara tatu zoote siku nzima. Yaweza mpelekea akala mara mbili tu kwa siku na saa ingine hata mara moja tu! Kutofautiana kwa wanadamu dhidi ya kuepusha hio hisia (ya njaa) ama kukidhi hio hisia (ya njaa) ndio yaweza pelekea kuonekana umuhimu ama heri.

Njaa ni heri pale ambapo itamandama mara kwa mara yule ambae hataki kabisa kukidhi njaa yake bila kusia hio hisia... For in other words ni kwamba asiposikia njaa aweza dhohofika, kosa lishe, na kurutubisha mwili ambao wahitaji saana chakula ili kuweza songa mbele na kukidhi mahitaji ya hisia ya njaa.....
 
jaribu kwanza kuniainishia kauli hizi mbili; kujua kufahamu na kufahamu kujua

Naona kama hujanitendea haki kwa kuniondoa kwenye mada inayplenga kumaliza NJAA YANGU!

Kwani Njaa yangu itamalizika tu punde nitakapo kuwa na elimu kuwa Ufahamu ni nini!

Lakini wewe umetaka tujadili KUFAHAMU !

Wakati kama tungechukulia hivyo kuwanvyakula visinge kuwa vyakula vya aina moja!

Sawa inegeweza kuwa kitu kimioja.. Ni mchele ... Lakini kimoja kikawa Biriani na kingine Ubwabwa!!
 
Asante kwa acknowledgement of my post.... Hapo bold hapo.... Nawezaje zungumzia kua njaa ni heri....

Wanadamu tumetofautiana saaana. Kama unavoelewa katika jamii yetu familia nyingi tumejijengea kula milo mitatu kwa siku; Yaani asubuhi mchana jioni.... Katika familia moja kuna ambae yeye lazima ale mda wa mlo ukifika iwe ana njaa ama Lah! Kuna mwingine yeye mlo ni pale ataposikia njaa regardless kua chakula kimeandaliwa mara tatu zoote siku nzima. Yaweza mpelekea akala mara mbili tu kwa siku na saa ingine hata mara moja tu! Kutofautiana kwa wanadamu dhidi ya kuepusha hio hisia (ya njaa) ama kukidhi hio hisia (ya njaa) ndio yaweza pelekea kuonekana umuhimu ama heri.

Njaa ni heri pale ambapo itamandama mara kwa mara yule ambae hataki kabisa kukidhi njaa yake bila kusia hio hisia... For in other words ni kwamba asiposikia njaa aweza dhohofika, kosa lishe, na kurutubisha mwili ambao wahitaji saana chakula ili kuweza songa mbele na kukidhi mahitaji ya hisia ya njaa.....

umenipoteza kweli kwenye bandiko lako. Tumekubaliana kuwa njaa ni dhana pana inayohusisha fikra na hisia. Hitaji lako ni heri yangu. Kile utakachotumia unagharamia, iwe chakula, elimu, mahaba(na kero zake) n.k.
 
Naona kama hujanitendea haki kwa kuniondoa kwenye mada inayplenga kumaliza NJAA YANGU!

Kwani Njaa yangu itamalizika tu punde nitakapo kuwa na elimu kuwa Ufahamu ni nini!

Lakini wewe umetaka tujadili KUFAHAMU !

Wakati kama tungechukulia hivyo kuwanvyakula visinge kuwa vyakula vya aina moja!

Sawa inegeweza kuwa kitu kimioja.. Ni mchele ... Lakini kimoja kikawa Biriani na kingine Ubwabwa!!

kufahamu jambo na ufahamu juu ya jambo sioni tofauti sana. Ufahamu ni uelewa (na kujielewa) wa jambo. Ujuzi/kujua ni zaidi ya ufahamu/kufahamu. Ombwe la ukosefu wa ufahamu hujazwa na ujinga, na pengine upumbavu. Ujinga si kosa wala tusi bali ni njaa ya fikra. Upumbavu ni tusi ama kejeli kwa mjinga aliyegoma kuerevuka. Aliyekosa uelewa ambao ni ufahamu. Mpumbavu ameshiba ombwe, lakini mjinga ana njaa ya ufahamu. Tunaenda sawa?
 
wazo ama kuwaza ni matokeo ya jambo lililopita. Kuwaza na kufikiri ni matukio mawili tofauti. Wazo ni mapitio ya mambo yaliyotokea ama yatarajiwayo. Jambo hutarajiwa kutokana na kuwepo awali. Kuwaza yasiyokuwepo ni kutabiri. Lakini kuwazua ni kufikiri, ambapo mtu hutafuta suluhu kati yake na mkingamo unaomkabili. 'wakati nafikiri likanijia wazo...'
 
utu ni sehemu ya mtu. Bila mtu utu haupo. Mtu na binadamu wanatofautiana. binadamu ni usawa lakini mtu ni upekee. Ubinadamu tofauti na utu, una matabaka lakini utu ni uleule. Utu ni hali. Utu ni dhamira iliyo hai. Utu ni kujibainisha. Utu ni hekima. Ubinadamu ni usawa, tena ubinadamu ni matabaka. Ubinadamu ni kuzaliwa (ndani ya tabaka), kukua, kula, kuumwa, kuerevuka, kuchukia, kufa (yote haya ndani ya matabaka-matajiri, masikini, makabika, mataifa). Juu ya yote hayo, utu ni uleule.
 
utu ni sehemu ya mtu. Bila mtu utu haupo. Mtu na binadamu wanatofautiana. binadamu ni usawa lakini mtu ni upekee. Ubinadamu tofauti na utu, una matabaka lakini utu ni uleule. Utu ni hali. Utu ni dhamira iliyo hai. Utu ni kujibainisha. Utu ni hekima. Ubinadamu ni usawa, tena ubinadamu ni matabaka. Ubinadamu ni kuzaliwa (ndani ya tabaka), kukua, kula, kuumwa, kuerevuka, kuchukia, kufa (yote haya ndani ya matabaka-matajiri, masikini, makabika, mataifa). Juu ya yote hayo, utu ni uleule.
Utanzania ni UTU!!Hauna udini, hauna ukabila, hauna Matabaka, hauna Itikadi, hauna jinsia, hauna rangi, hauna urefu, upana, urefu , ufupi ...UTU NI UTU!! UTU NI UTANZANIA KAMILI!!
 
Utanzania ni UTU!!Hauna udini, hauna ukabila, hauna Matabaka, hauna Itikadi, hauna jinsia, hauna rangi, hauna urefu, upana, urefu , ufupi ...UTU NI UTU!! UTU NI UTANZANIA KAMILI!!

nachelea kuafikiana na wewe. Utanzania ni utamaduni na utamaduni si utu mkuu
 
Back
Top Bottom