Nyani Ngabu
Platinum Member
- May 15, 2006
- 94,296
- 122,540
Makamanda wamechanganyikiwa.
Hawajui kama wanaenda au wanakuja.
Sasa sikilizeni nyie makamanda [ingawa najua hamna uwezo mkubwa wa kufikiri kwa kutumia akili, lakini jitahidini kuelewa].
Ni hivi:
Rais Magufuli hatofikishwa huko kwenye mahakama ya kimataifa ya jinai.
Hatofikishwa kwa sababu hakuna sababu yoyote ile ya msingi, inayolazimu yeye kufikishwa huko na kushitakiwa.
Hizi kelele mnazopigishwa na huyo mgombea wenu wa 2025, Bob Amsterdam, ni fikra/ mawazo tamanifu tu.
Sina hakika kama mnalitambua hilo. Kwamba, hawezi kufikishwa huko.
Natambua ni kiasi gani fikra/ mawazo tamanifu [wishful thinking] yanavyoweza kumpa mtu faraja ya muda mfupi pindi apitiapo kipindi kigumu cha maumivu ya kihisia na kiakili.
Mawazo hayo tamanifu hutoa hifadhi ya faraja.
Na ndo maana mnapoona au mnaposikia sijui mwanaharakati gani wa Twitter amepeleka barua au sijui ushahidi huko kwenye hiyo mahakama ya kimataifa ya masuala ya jinai, mnafurahi, mnachekelea, bila hata kuangalia na kupima uhasilia na mwelekeo wa kile mnachokitaka, kutokea.
Mtu yeyote anaweza kutangaza kumshitaki yeyote yule au chochote kile, popote pale. Ukweli huo nadhani hamuuzingatii kwa uzito na u maanani unaostahili.
Licha ya kwamba Tanzania tuna matukio ya hapa na pale ya ukiukwaji wa haki za kibinadamu, bado hatujafikia viwango vya kushitakiwa rasmi kwenye hiyo mahakama.
Najua nyie makamanda huwa hampendi kuambiwa ukweli. Mnachokipenda ni maneno ya kufarijiana tu mpaka uchaguzi ujao.
Na uchaguzi ujao ukifika, haya ya 2020 mtakuwa mshayasahau kama ambavyo mmeyasahau yote ya 2015, 2010, 2005, 2000, na 1995.
Hivyo endeleeni kuota ndoto za mchana. Si Raisi Magufuli, Da Samia, Bw. Majaliwa, au Kamanda Sirro atayetiwa pingu na kupelekwa Uholanzi kusomewa mashitaka.
Najua mnapitia kipindi kigumu sana. Hivyo nawaelewa. Nazielewa fikra zenu tamanifu mlonazo.
Na ni fikra tu. Siyo uhalisia wala mwelekeo wa matukio ya kiuhalisia.
Hawajui kama wanaenda au wanakuja.
Sasa sikilizeni nyie makamanda [ingawa najua hamna uwezo mkubwa wa kufikiri kwa kutumia akili, lakini jitahidini kuelewa].
Ni hivi:
Rais Magufuli hatofikishwa huko kwenye mahakama ya kimataifa ya jinai.
Hatofikishwa kwa sababu hakuna sababu yoyote ile ya msingi, inayolazimu yeye kufikishwa huko na kushitakiwa.
Hizi kelele mnazopigishwa na huyo mgombea wenu wa 2025, Bob Amsterdam, ni fikra/ mawazo tamanifu tu.
Sina hakika kama mnalitambua hilo. Kwamba, hawezi kufikishwa huko.
Natambua ni kiasi gani fikra/ mawazo tamanifu [wishful thinking] yanavyoweza kumpa mtu faraja ya muda mfupi pindi apitiapo kipindi kigumu cha maumivu ya kihisia na kiakili.
Mawazo hayo tamanifu hutoa hifadhi ya faraja.
Na ndo maana mnapoona au mnaposikia sijui mwanaharakati gani wa Twitter amepeleka barua au sijui ushahidi huko kwenye hiyo mahakama ya kimataifa ya masuala ya jinai, mnafurahi, mnachekelea, bila hata kuangalia na kupima uhasilia na mwelekeo wa kile mnachokitaka, kutokea.
Mtu yeyote anaweza kutangaza kumshitaki yeyote yule au chochote kile, popote pale. Ukweli huo nadhani hamuuzingatii kwa uzito na u maanani unaostahili.
Licha ya kwamba Tanzania tuna matukio ya hapa na pale ya ukiukwaji wa haki za kibinadamu, bado hatujafikia viwango vya kushitakiwa rasmi kwenye hiyo mahakama.
Najua nyie makamanda huwa hampendi kuambiwa ukweli. Mnachokipenda ni maneno ya kufarijiana tu mpaka uchaguzi ujao.
Na uchaguzi ujao ukifika, haya ya 2020 mtakuwa mshayasahau kama ambavyo mmeyasahau yote ya 2015, 2010, 2005, 2000, na 1995.
Hivyo endeleeni kuota ndoto za mchana. Si Raisi Magufuli, Da Samia, Bw. Majaliwa, au Kamanda Sirro atayetiwa pingu na kupelekwa Uholanzi kusomewa mashitaka.
Najua mnapitia kipindi kigumu sana. Hivyo nawaelewa. Nazielewa fikra zenu tamanifu mlonazo.
Na ni fikra tu. Siyo uhalisia wala mwelekeo wa matukio ya kiuhalisia.