Fikra za Askofu Bagonza

Matanga

JF-Expert Member
Joined
Nov 13, 2019
Posts
2,281
Reaction score
3,976
CHANJO. MBOWE. KATIBA MPYA. TOZO ZA MIAMALA. RAIS SSH

Mambo haya 5 yameshikilia mustakabali wa nchi kwa sasa. Amani, haki, Maendeleo na ustawi vinatikiswa. Jiulize:

1. Kwa nini itumike nguvu na jitihada za ziada kuwaaminisha watu wakachanje wakati afya ni mali yao?

2. Kwa nini wana CCM wapinge chanjo wakati afya ni sera ya ilani yao ya Uchaguzi?

3. Kwa nini suala la Mbowe kufunguliwa mashtaka ya ugaidi linapigiwa kelele na watu bila kujali itikadi zao?

4. Kwa nini tozo za mihamala zimeligawa bunge na serikali na kuusambaratisha uwajibikaji wa pamoja?

5. Kwa nini madai ya Katiba Mpya sasa yanaanza kusikia ndani ya CCM kuliko ilivyokuwa katika awamu ya 5?

6. Kwa nini watu wengi wakiwamo Wana CCM wanamlaumu Rais SSH kwa yote 4 (Mbowe, Tozo, Katiba Mpya na Chanjo)?

UKWELI USIOTAMKWA:

a). Awamu ya 5 ilimwaga sumu kali kupinga chanjo. Waliopinga chanjo hawawezi kuinadi leo itakubalika. Watafutwe wengine kutoka makundi yote.

b). Serikali na Chama tawala vimegawanyika juu ya chanjo. Kila mtu anatamani katiba mpya inayoruhusu Rais kuhojiwa bila ya anayehoji kupata madhara. Kuna wengi waliomuunga mkono lakini sasa wanafikiri vinginevyo.

c). Tuhuma za ugaidi dhidi ya Mbowe zimeligawa Taifa. Zimefuta mazuri yote ya awamu ya 6. Zimechochea madai ya Katiba Mpya. Waliomshauri Rais hawalitakii mema Taifa. Hata chama tawala wanataka haki za Binadamu. Urais uko mnadani.

c). Mpaka sasa mawaziri (wa fedha na Waziri wa Mihamala ya simu) hawajatoa hoja zenye nguvu kuhalalisha tozo za juu kwa watumiaji. Wengi wanaona mawaziri wanamhujumu Rais au Rais ameruhusu kuhujumiwa.

d). Rais SSH ni "Rais wa Katiba" kwa mujibu wa Katiba. Kuna "wapotoshaji" pande zote (CCM na Upinzani) wanaosema Rais hapendi katiba mpya kwa sababu hii anaiona nzuri kwa kumleta madarakani. Muungano huu wa "wapotoshaji" si salama kwa Rais. Rais ana fursa nzuri ya kuweka historia. Anaelekea kuipoteza.

MUHIMU:


Kumshikilia Mbowe kwa tuhuma zinazoonekana "bambikizi", kunaua uwezekano wa maridhiano na mazungumzo ya kuliunganisha Taifa. Taifa lililogawanyika:

-Haliwezi kujibu ushirikina wa
kisomi (conspiracy)
-Haliwezi kuchanja kikamilifu
-Haliwezi kuingia vita dhidi ya corona
-Haliwezi kuwa na bajeti endelevu
-Linaongozwa na nguvu kuliko akili
-Haliwajibiki kwa pamoja mbele ya
umma
-Huwaona raia kuwa maadui wa Taifa.

DAMU ISIYO NA HATIA ISIPOKOMBOA HUANGAMIZA. MATESO YA MWENYE HAKI NI HUKUMU KWA MTAWALA ASIYEONA DHULUMA.

Kuna watu wanaomba Novena leo siku ya 5.

Sent from my TECNO LC6 using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom