Filamu inayoelezea kuwa sisi ni Wayahudi

Filamu inayoelezea kuwa sisi ni Wayahudi

Mohamed Said

JF-Expert Member
Joined
Nov 2, 2008
Posts
21,967
Reaction score
32,074
‘’SISI NI WAYAHUDI’’ (THE BOY IN STRIPPED PYJAMAS)

Hiki ni kitabu kilichoandikwa na John Boyne na kikafanywa filamu.

Hii ni hadith katika mambo ya kweli kuhusu kijana wa miaka tisa Bruno ambae baba yake ni katika askari katika jeshi la Wajerumani wakati wa Vita Vya Pili Vya Dunia.

Baba yake ndiye kiongozi wa kambi ya mateso na mauaji ya Wayahudi.

Kisa kinaanza mara tu baada ya baba yake Bruno kuhamia kwenye kambi hiyo.

Mtoto Bruno anashangazwa na uzio wa miba ya chuma kati ya nyumba yao na kambi halikadhalika anashangazwa na watu na watoto anaowaona upande ule wa pili.

Ni watu kama baba yake na watoto ni watoto kama yeye lakini watu anaowaona upande wa pili wa uzio muda wote wako katika vikundi na wanaswagwa na wanaonekana wako katika majonzi.

Katika filamu kuna ‘’scene,’’ ya kumtoa mtazamaji machozi pale Bruno na rafiki yake wakiwa wametenganishwa na uzio wa miba ya chuma wanacheza ‘’draft."

Hili "draft" liko upande alioko Bruno.

Wayahudi ni hodari sana wa mambo haya wameweza kuhifadhi historia yao yote ya mateso katika mikono ya Manazi katika maandishi, sauti na picha na duniani pote utakapokwenda utakuta hizi makumbusho.

Turudi kwa Bruno na rafiki yake.

Muongozaji filamu hafanyi haraka kuondoa camera anataka mtazamaji ushibishe macho yako na anachokusudia kikuingie akilini.

Bruno amenawiri na kavaa nguo safi shati jeupe na kaptula iiyomkaa vema.

Rafiki yake kavaa pyjamas zilizochoka na zisizovutia kutazama na uso wake umesinyaa kwa shida.

Bruno akiwa pale katika mpaka ule anashuhudia mengi upande wa pili ambao hayaelewi na anamuuliza maswali rafiki yake.

Lakini katika maswali yote aliyomuuliza rafiki yake ambayo yeye hakuwa na majibu swali moja alikuwa na jibu lake.

Bruno alimuuliza, ‘’ Kwa nini nyinyi mko katika hali hii?

Rafiki yake alimjibu akamwambia, ‘’Sisi ni Wayahudi.’’
 
"Sisi ni Wayahudi," llakini inaweza kuwa kabila lolote.

Screenshot_20201112-152433.jpg
Screenshot_20201112-152145.jpg
Screenshot_20201112-152010.jpg
 
Dah! Nitaitafuta hii movie inaonyesha inagusa hisia sana.
 
Mzee wangu Mohamed Said haya mambo ukiyafikiria huwa yanaumiza sana na hayatakiwi kuungwa mkono na mtu muungwana popote pale duniani. Lakini leo hii kumekuwa na kitabia fulani cha wasomi kutokuwa Morally Objective hasa linapokuja suala zima la ubaguzi na unyanyasaji. Leo hii kuna watu kutokana na sababu zao za kisiasa wanakataa kwamba mauaji ya Wayahudi hayakufanyika kule Auschwitz: Wengine wanaenda mbali kabisa na kutilia shaka kwamba mauji yale mauji ya Rwanda hayakuwa ni Genocide na kwenda mbali na kusema watusi waliyataka wenyewe. Hili huwa linanishangaza mno.

Sasa ili kuwa Morally Objective ni lazima tujifunze kuwa na kifua cha kuyaona madhaifu yetu na kuyakemea pale inapostahili. Hichi kinachofanywa leo na CCM dhidi ya Wazanzibari kilifanywa sana na watawala wa kiarabu huko Zanzibar dhidi ya watu weusi wakati wa biashara ya utumwa: Hili ndugu zangu wengi Wazanzibari huwa mnalifumbia kabisa macho na kutaka kuonesha kuwa mikono yeni ni safi (Not Right at all).

Ifike mahali tuseme yale ya Dr Martin Luther King kwamba "Injustice Somewhere, is injustice everywhere" akimanisha kwamba tatizo la binadamu mwenzako ni lako. Katika hili mimi nasema nobody should belittle the history, adverse experiences and struggles of a particular group. Ikiwezekana wanapolalamika tutulie tusikilize ili tujifunze kukaa chini ya viatu vye wenzetu na kusikiliza madai yao. Binafsi nadhani tukijiaminisha kwamba kila jambo la kijamii tunaweza kulitatua kisiasa nadhani hatutafika popote maana kila kundi lina mtizamo wake.
 
Back
Top Bottom