Flyover za Dar es Salaam zamchanganya mjumbe kutoka mkoani

PAZIA 3

JF-Expert Member
Joined
Jan 30, 2018
Posts
1,102
Reaction score
1,919
Kuna jamaa yangu kanichekesha sana, miezi 2 iliyopita alienda Dar es Salaam, kituo cha kwanza kwake ilikuwa kuziona hizo barabara za flyover, ili apate kusafiri kwa kupitia juu.

Sasa anadai alichokiona ni tofauti kabisa, yeye alijua zina urefu kiasi kwamba unaweza kusafiri hata kilometers 4, akawa anauliza, zile ninazozionaga kwenye tv ziko wapi?

Wakamwambia ni hizo, sa mbona nikuvuka upande mmoja kwenda mwingine tu? Akaambiwa ndivyo zilivyo, kwani nyie mikoani mnajuaje?

Akasema tunajua ni barabara ndefu unaweza kusafiri hata siku nzima, jamaa alicheka Sana. Kwa mlioko Dar, tuambieni ukweli.
 
Huyo anawakilisha kundi kubwa la Wanasigimbi walioathirika na propaganda za Magufuli na CCM....cha ajabu kuna wengine humu jukwaani tunao na ni wabishi while wanaishi Sengerema and the like areas!
 
Msiwe mnalinganisha flyover na mambo ya kijinga.
 
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23] nimecheka hadi baas lol
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…