#COVID19 Fomu ya kuridhia chanjo ya corona (conset form) irekebishwe. Serikali ikubali kuwajibika kwa madhara ya chanjo kwa watu

#COVID19 Fomu ya kuridhia chanjo ya corona (conset form) irekebishwe. Serikali ikubali kuwajibika kwa madhara ya chanjo kwa watu

mbingunikwetu

JF-Expert Member
Joined
Feb 17, 2015
Posts
13,897
Reaction score
18,477
Kamati ya corona pamoja na majukumu mengine ilipewa kazi ya kuzifanyia utafiti chanjo za corona ili kujiridhisha kwa ubora na usalama wake kabla ya kuziruhusu kutumika kwa watanzania.

Kamati hiyo ilijitokeza mbele ya watanzania wakiwa wameficha nyuso zao kwa kisingizio cha kuvaa barakoa, na wakasema chanjo hizo ni salama! Serikali kwa kuzingatia na kuuamini utafiti wa kamati ya corona wakaamua kuanza mchakato wa kuagiza chanjo za corona.

Swali: Kwa nini sasa serikali inakwepa kukubali kuwajibika kwa athari wanazoweza kupata watakaokubali kuchanjwa kama wanaamini kuwa chanjo hizo ni salama?

Naomba kuhusiana na chanjo hizi za corona lazima serikali iseme kwa wazi moja ya mambo haya mawili:

1. Kama wanakubali kuwa chanjo hizi ni salama, basi wakubali kuwajibika kwa matokeo hasi za chanjo hizo na waathirika wawe na haki ya kuidai fidia serikali mahakamani kwa madhara yanayoweza kujitokeza ya chanjo za corona.

2. Kama hilo la kwanza hawawezi kulisema, basi serikali lazima iseme wazi kuwa hawana uhakika na usalama wa chanjo hizo na atakayeamua kuchanjwa atawajibika mwenyewe kwa kukubali kwake kuchanjwa yaani "take a jab at your own risk"!

Baada ya serikali kusema moja ya mambo hayo hapo juu, hilo jambo liandikwe juu kabisa kwenye fomu ya kuridhia chanjo, na fomu hiyo iandikwe kwa kiswahili ili kila mmoja aielewe vizuri na ibandikwe kwenye mbao za matangazo kwenye kila ofisi ya serikali kuanzia serikali za mitaa na kila kwenye zahanati, kituo cha afya na hospitali zote.

Haiwezekani serikali ikatuambia chanjo ni salama halafu ikakataa kuwajibika kwa matokeo ya chanjo

Mambo ya kukataa kuwajibika huwa ni kwa chanjo za majaribio ambazo walioridhia kujitolea kwa majaribio hayo huwa wamekubali kujitoa muhanga wenyewe kwa manufaa ya utafiti. Kama serikali inatufanyia utafiti basi iseme hivyo wazi

Lakini pia majina yote ya kamati ya corona na nafasi zao yawekwe wazi. Maana tunajua jina la mwenyekiti tu, nalo tulilijua mwishoni. Historia itakuwa na jambo na kamati hii, huwezi kujua!! Wasifichwe! Kama wamefanya kazi njema wawekwe wazi ili historia iwapongeze au iwashutumu.
 
Tanzania ndiyo itakuwa nchi ya kwanza duniani kufanya hicho ulichoshauri hapo! Ni kwamba ukipata tatizo kutokana na hiyo chanjo utapewa msaada wa kitabibu, lakini kama hilo tatizo litashindwa kutatuliwa then ukawa kilema or maiti then serikali imejivua uhusika, ndiyo maana ukaambiwa siyo lazima
 
Umeshaambiwa kuchanja ni hiyari sio lazima. Kwa maana nyingine unawajibika kwa maamuzi yako yoyote utakayochukua. Ukikataa, faida na hasara ni juu yako na ukikubali, faida na hasara ni juu yako.

Epuka kuishi kwenye fikra za marehemu. Covid-19 ipo na inaua. Chukua tahadhari,jikinge na ulinde familia yako
 
Mpaka unachanjwa si unaridhia mwenyewe kwa kitu chochote, hapo serikali iwajibike kwa lipi?

Hakika BAVICHA Mbowe anawapeleka puta kama gari bovu.
Ridhaa ya mtu lazima ijengwe kwenye taarifa sahihi. Mtu asipewe taarifa potofu halafu ukasema ameridhia mwenyewe! Vinginevyo atakuwa amedanganywa! Amepotoshwa ! Ameingizwa chaka! Hana tofauti na aliyetapeliwa!!
 
Umeshaambiwa kuchanja ni hiyari sio lazima. Kwa maana nyingine unawajibika kwa maamuzi yako yoyote utakayochukua. Ukikataa, faida na hasara ni juu yako na ukikubali, faida na hasara ni juu yako.

Epuka kuishi kwenye fikra za marehemu. Covid-19 ipo na inaua. Chukua tahadhari,jikinge na ulinde familia yako
Kabla ya kusema chanjo ni hiari, wamesema chanjo ni salama!! Wamefanya utafiti! Kwa hiyo hiari ya mtu inajengwa kwenye hiyo taarifa. Kama hawana uhakika na usalama wa chanjo, waseme wazi. Tusidanganyane!! Hiari hujengwa kwenye msingi wa taarifa!! Tunadai taarifa thabiti!!! Serikali lazima iwe na ujasiri huo ili tuiamini katika hili! Haya ni maisha ya watu yasiyokuwa na mbadala!!
 
Mpaka unachanjwa si unaridhia mwenyewe kwa kitu chochote, hapo serikali iwajibike kwa lipi?

Hakika BAVICHA Mbowe anawapeleka puta kama gari bovu.
Usiseme ya Mbowe! Mbowe yeye anataka chanjo iwe lazima!! Nadhani uko nyuma sana ya wakati!
 
A
Ridhaa ya mtu lazima ijengwe kwenye taarifa sahihi. Mtu asipewe taarifa potofu halafu ukasema ameridhia mwenyewe! Vinginevyo atakuwa amedanganywa! Amepotoshwa ! Ameingizwa chaka! Hana tofauti na aliyetapeliwa!!
Acha ubishi usio na maana, chanjo iliyoagizwa ni ile ile ambayo nchi nyingine inaleta madhara baadhi kama kuganda damu na madhara hayo pia yanaweza kuwapata watanzania.

Kwa kuwa bado hatujawa na chanjo yetu wenyewe hivyo serikali imeona ijivue lawama kwa lolote ndio maana unajaza fomu ya kuridhia baada ya hapo madhara na faida za kuchanjwa ni juu yako mwenyewe.

Nafikiri pia kabla ya kuchanjwa na kujaza fomu MTU aambiwe kabisa chanjo hii imeleta madhara kwa baadhi ya watu kama kuganda damu hivyo madhara hayo yanaweza kukukumba wewe , jje unaridhia?

Serikali haikupi taarifa isiyo sahihi kwa sababu chanjo haijatengenezwa Tanzania hivyo taarifa zote serikali inapata huko
 
Kamati ya corona pamoja na majukumu mengine ilipewa kazi ya kuzifanyia utafiti chanjo za corona ili kujiridhisha kwa ubora na usalama wake kabla ya kuziruhusu kutumika kwa watanzania. Kamati hiyo ilijitokeza mbele ya watanzania wakiwa wameficha nyuso zao kwa kisingizio cha kuvaa barakoa, na wakasema chanjo hizo ni salama! Serikali kwa kuzingatia na kuuamini utafiti wa kamati ya corona wakaamua kuanza mchakato wa kuagiza chanjo za corona!! SWALI: KWA NINI SASA SERIKALI INAKWEPA KUKUBALI KUWAJIBIKA KWA ATHARI WANAZOWEZA KUPATA WATAKAOKUBALI KUCHANJWA KAMA WANAAMINI KUWA CHANJO HIZO NI SALAMA?
Naomba kuhusiana na chanjo hizi za corona lazima serikali iseme kwa wazi moja ya mambo haya mawili: 1. Kama wanakubali kuwa chanjo hizi ni salama, basi wakubali kuwajibika kwa matokeo hasi za chanjo hizo na waathirika wawe na haki ya kuidai fidia serikali mahakamani kwa madhara yanayoweza kujitokeza ya chanjo za corona. 2. Kama hilo la kwanza hawawezi kulisema, basi SERIKALI LAZIMA ISEME WAZI KUWA HAWANA UHAKIKA NA USALAMA WA CHANJO HIZO NA ATAKAYEAMUA KUCHANJWA ATAWAJIBIKA MWENYEWE KWA KUKUBALI KWAKE KUCHANJWA YAANI "TAKE A JAB AT YOUR OWN RISK"!!
Baada ya serikali kusema moja ya mambo hayo hapo juu, hilo jambo liandikwe juu kabisa kwenye fomu ya kuridhia chanjo, na fomu hiyo iandikwe kwa kiswahili ili kila mmoja aielewe vizuri na ibandikwe kwenye mbao za matangazo kwenye kila ofisi ya serikali kuanzia serikali za mitaa na kila kwenye zahanati, kituo cha afya na hospitali zote.
Haiwezekani serikali ikatuambia chanjo ni salama halafu ikakataa kuwajibika kwa matokeo ya chanjo!!
Mambo ya kukataa kuwajibika huwa ni kwa chanjo za majaribio ambazo walioridhia kujitolea kwa majaribio hayo huwa wamekubali kujitoa muhanga wenyewe kwa manufaa ya utafiti. Kama serikali inatufanyia utafiti basi iseme hivyo wazi!!
Lakini pia majina yote ya kamati ya corona na nafasi zao yawekwe wazi. Maana tunajua jina la mwenyekiti tu, nalo tulilijua mwishoni. Historia itakuwa na jambo na kamati hii, huwezi kujua!! Wasifichwe! Kama wamefanya kazi njema wawekwe wazi ili historia iwapongeze au iwashutumu!!
Wacha kuisingizia serikali maana chanjo ni kwa manufaa yako binafsi.

Ukitaka chanjwa ukikataa kataaa tu na tutakufukia tu kama tunavyo wafukia wengine
 
Oneni hii hapa:
 
Kabla ya kusema chanjo ni hiari, wamesema chanjo ni salama!! Wamefanya utafiti! Kwa hiyo hiari ya mtu inajengwa kwenye hiyo taarifa. Kama hawana uhakika na usalama wa chanjo, waseme wazi. Tusidanganyane!! Hiari hujengwa kwenye msingi wa taarifa!! Tunadai taarifa thabiti!!! Serikali lazima iwe na ujasiri huo ili tuiamini katika hili! Haya ni maisha ya watu yasiyokuwa na mbadala!!
Kuna una mashaka, kwenye options za hiyari chagua kukataa.
 
Wacha kuisingizia serikali maana chanjo ni kwa manufaa yako binafsi.

Ukitaka chanjwa ukikataa kataaa tu na tutakufukia tu kama tunavyo wafukia wengine
Kwa taarifa yako wako wengi sana waliochanjwa na wavaa barakoa lakini wamefukiwa!!! Nchi zinazoongoza kwa chanjo zinaongoza pia kwa kufukia watu wengi!! Tanzania tuko salama sana! Walitutabiria kuokota miili barabarani, na mpaka kesho hatutaokota miilibarabarani!! Mungu wetu ni mkubwa kuliko corona!! Uko mzima leo kama matokeo ya majibu ya Mungu kwa maombi ya watanzania hata kama haulijui hilo!!
Kuna mjinga mmoja na kiongozi wa chama fulani, amesema baada ya wiki mbili hali itakuwa mbaya sana!! Ameshashindwa na kulegea! Wiki mbili zitaisha! miezi miwili itaisha na hata miaka miwili itaisha na atashuhudia watanzania wakiwa salama!! Labda familia yake ndio itaathirika na corona maana ameamua mwenywewe kuwa muumini wa corona badala ya kumwamini Mungu aliye hai!! Inabidi mtu aamue kufumba macho ili asiweze kuona jinsi Tanzania tulivyo salama ukilinganisha na mataifa mengine yaliyoathirika sana!! Wao hawakuweza kujisaidia watatusaidiaje sisi? Silaha iliyoshindwa kuwalinda wao wao itawezaje kutulinda sisi? Huyo mjinga mmoja anathubutu kusema tusimamishe miradi yote ya maendeleo ili tupambane na corona!! Walioingia kwenye huu mtego watakuwa watumwa wa corona maisha yao yote! Chonde chonde Tanzania tusiingizwe mkenge!! Haya ni magonjwa ya kupandikizwa ili watu wapige pesa!!
 
SERIKALI LAZIMA ISEME WAZI KUWA HAWANA UHAKIKA NA USALAMA WA CHANJO HIZO NA ATAKAYEAMUA KUCHANJWA ATAWAJIBIKA MWENYEWE KWA KUKUBALI KWAKE KUCHANJWA YAANI "TAKE A JAB AT YOUR OWN RISK"!!
Umeshaambiwa kuchanja ni hiari, hulazimishwi. Sasa changanya akili za kuambiwa na serikali na zako mwenyewe. Acha hoja za "mama nianze mboga nianze ugali?".
 
Kamati ya corona pamoja na majukumu mengine ilipewa kazi ya kuzifanyia utafiti chanjo za corona ili kujiridhisha kwa ubora na usalama wake kabla ya kuziruhusu kutumika kwa watanzania. Kamati hiyo ilijitokeza mbele ya watanzania wakiwa wameficha nyuso zao kwa kisingizio cha kuvaa barakoa, na wakasema chanjo hizo ni salama! Serikali kwa kuzingatia na kuuamini utafiti wa kamati ya corona wakaamua kuanza mchakato wa kuagiza chanjo za corona!! SWALI: KWA NINI SASA SERIKALI INAKWEPA KUKUBALI KUWAJIBIKA KWA ATHARI WANAZOWEZA KUPATA WATAKAOKUBALI KUCHANJWA KAMA WANAAMINI KUWA CHANJO HIZO NI SALAMA?
Naomba kuhusiana na chanjo hizi za corona lazima serikali iseme kwa wazi moja ya mambo haya mawili: 1. Kama wanakubali kuwa chanjo hizi ni salama, basi wakubali kuwajibika kwa matokeo hasi za chanjo hizo na waathirika wawe na haki ya kuidai fidia serikali mahakamani kwa madhara yanayoweza kujitokeza ya chanjo za corona. 2. Kama hilo la kwanza hawawezi kulisema, basi SERIKALI LAZIMA ISEME WAZI KUWA HAWANA UHAKIKA NA USALAMA WA CHANJO HIZO NA ATAKAYEAMUA KUCHANJWA ATAWAJIBIKA MWENYEWE KWA KUKUBALI KWAKE KUCHANJWA YAANI "TAKE A JAB AT YOUR OWN RISK"!!
Baada ya serikali kusema moja ya mambo hayo hapo juu, hilo jambo liandikwe juu kabisa kwenye fomu ya kuridhia chanjo, na fomu hiyo iandikwe kwa kiswahili ili kila mmoja aielewe vizuri na ibandikwe kwenye mbao za matangazo kwenye kila ofisi ya serikali kuanzia serikali za mitaa na kila kwenye zahanati, kituo cha afya na hospitali zote.
Haiwezekani serikali ikatuambia chanjo ni salama halafu ikakataa kuwajibika kwa matokeo ya chanjo!!
Mambo ya kukataa kuwajibika huwa ni kwa chanjo za majaribio ambazo walioridhia kujitolea kwa majaribio hayo huwa wamekubali kujitoa muhanga wenyewe kwa manufaa ya utafiti. Kama serikali inatufanyia utafiti basi iseme hivyo wazi!!
Lakini pia majina yote ya kamati ya corona na nafasi zao yawekwe wazi. Maana tunajua jina la mwenyekiti tu, nalo tulilijua mwishoni. Historia itakuwa na jambo na kamati hii, huwezi kujua!! Wasifichwe! Kama wamefanya kazi njema wawekwe wazi ili historia iwapongeze au iwashutumu!!
Wakati ambapo serikali yeyote ya dunia ingeweza kuamika kwa lolote umepita mkuu.Fanya utafiti wako binafsi,beba msalaba wako.

Kwa kukusaidia fuata link ifuatayo ili uweze kufanya maamuzi ya busara na sahihi kwako binafsi,familia yako na wengine uwapendao.Let make this clear,kwa swala hili la the so called C-19 vaccine no body should make a mistake,it is a matter of life and death.Usiitegemee serikali yetote ya dunia leo ikulinde,hicho kitu hakipo,serikali zote za dunia lao ni moja.

 
Back
Top Bottom