Baada ya hapo alitolewa kwa mkopo kwenda Stuttgart ili akapate uzoefu wa ligi, maana kwa kipindi hicho Sagnol na Lizarazu ndio walikua mabeki wa kulia chaguo la kwanza kwa upande wa bayern.
Aliichezea Stuttgart toka mwaka 2003 hadi 2005 akiwa kacheza michezo 53 na kufunga magoli mawili.
Mwaka 2008 Philipp alikataa ofa ya kujiunga na Manchester united na Barcelona ni baada Hoeness kumuahidi kujenga timu itakayokua shindani kwenye makombe ya ulaya.
Mwaka 2009 Lahm alipigwa faini kubwa ambayo haijawahi tokea katika historia ya club ya bayern (€25,000) ni baada ya kufanya interview bila ruhusa/kibali.