For Engineers and Architectures

Picha namba moja nakumbuka wakati nipo chuo tulikuwa tunafundishwa kuchora manually wakati tupo chuo, nikawa nashangaa sana yani wenzetu huko walishatoka na wanabuni mixer ku update softwares ila sisi karne ya 21 tunafundishwa kuchora manually
 
Interested

Nisipopata kazi na humu kwa ma-engineer wenzangu tena itakuwa balaaa

Jamani naombeni kazi kijana wenu hali yangu mbay,nadaiwa kodi matatizo chungu nzima.

Elimu form six PCM

Miaka 26

Naishi tabata.
 
Nyie mnaotegemea msaada wa kompyuta hamna kitu, hawa ndio walikuwa vichwa.
 
Waliosoma zamani kabla ya kuwepo kwa auto-cards na arch-card softwares wamefanya kazi za Kihandisi kwenye mazingira magumu zaidi.

Imagine unapewa tender ya kudesign jengo la ghorofa 5 unajikuta unatumia muda mrefu kuweza kuikamilisha, Wakati kwa mazingira yetu ya Sasa nikikomaa ndani siku 2 hadi 3 nakuwa nimekamilisha kazi ya mteja.

Ninacho kumbuka Engineering drawing kutumia hizo device ilikuwa ni experience ngumu Sana hasa kwa tuliotoka form six Moja kwa Moja compared na waliosoma college kabla ya kuingia Chuo Kikuu.

Unakutana na Prof anakupa jengo la ghorofa kadhaa anakwambia umchoree right real, side view, aerial view n.k au unapewa object ana kwambia ichukue hiyo object ikate Kati alafu chora kitu unachokiona Ndani na ukute hujasoma technical drawing kama wenzako wa college au waliosoma Shule za Ufundi O'level 😢
 
Nyie mnaotegemea msaada wa kompyuta hamna kitu, hawa ndio walikuwa vichwa.
Mkuu unataka uendelee kutumia Uwimbo na Ulindi Kuzalisha moto Wakati Kuna viberiti na lighter nyingine kufanya kazi hiyo?

Yaani unataka kutembea kwa miguu kutoka DSM hadi Dodoma kwa siku 21 Wakati Kuna Basi, Ndege n.k kukufikisha huko kwa Masaa kadhaa?

Sasa hizo skills na Knowledge tulizopewa zinatumikaje Chief kusolve hizo changamoto.

Kunaweza kuwa na mapungufu kiasi kwenye utendaji kazi wetu lakini kusema kweli kila mnachofanya hapa Duniani kinategemea Engineers 💪
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…