Ewe mvivu, mwendee chungu, Zitafakari njia zake ukapate hekima.
Mithali 6:6
Ewe mvivu, utalala hata lini? Utaondoka lini katika usingizi wako?
Mithali 6:9
Kama siki menoni, na kama moshi machoni, Ndivyo alivyo mtu mvivu kwao wamtumao.
Mithali 10:26
Mkono wa mwenye bidii utatawala; Bali mvivu atalipishwa kodi.
Mithali 12:24
Nafsi ya mtu mvivu hutamani asipate kitu; Bali nafsi ya mwenye bidii itanenepeshwa.
Mithali 13:4
Yeye naye aliye mvivu katika kazi yake, Ni ndugu yake aliye mharabu.
Mithali 18:9
Uvivu humtia mtu katika usingizi mzito; Na nafsi yake mvivu itaona njaa.
Mithali 19:15
Mtu mvivu hataki kulima wakati wa baridi; Hivyo wakati wa mavuno ataomba, hana kitu.
Mithali 20:4