Frederick Mpendazoe atimkia CCJ...

niko tayari kuchangia dizeli aanze mikakati yake, MUNGU akubariki ewe Fred kwa kukataa unafiki, wizi, na ula rushwa wa kikwete.

naomba mwenye contact zake anipe
 
Namba zake ni 0717 050335. Lakini hapokei simu
 
Naomba kuelimishwa iwapo CCJ walishapata Usajili wa Kudumu?
Bado hawajapata usajili wa kudumu.

Hii CCJ na CHADEMA watagawana kura na kuiacha CCM inapeta kilaini sana. Labda wakubali kuachiana majimbo hapo kutakuwa na la maana.
 
Mwache aende zake - ameshakuwa "liability" na angebakia CCM "tungempiga chini" katika kura za MAONI!

OFF Topic: TuskerBariiiidi? Siku hizi sikuoni mitaa yetu ya Meeda na B-Bar! Au kwa sababu Tusker imekuwa adimu?
...Liability kwa kuwa mkweli??? dont be stupidd!
 
Hivi huyu mpendazoe alikuwa pande ipi kati ya Lowassa na Sitta?
 
Nimjuavyo Mpendazoe,

Alikuwa DG wa baraza la mazingira, akahamia wizara ya maji kabla ya kwenda jimboni. Kwa watu waliofanya nae kazi wanamjua. Ana msimamo ya yale anayoyaamini, ni mchapakazi. Wavivu wote wa kufikiri na kutenda kwa mazoea wanamjua vizuri huyu.
 
huu ni kati ya uamuzi mmbaya kabisa kuwahi kuona maishani mwangu, habari za yeye kuondoka alianza kuwaambia watu wake wa karibu mwezi fenruary siku chache tu baada ya CCM kuadhimisha miaka 33 ya kuzaliwa kwake. alishajadiliwa mara kadhaa na chama hakikuona tishio lolote la ushindi kama angeamua kutelkeleza mpango yake hiyo. kuna wakati inanfika unaona mwenyewe kuwa huwezi siasa za CCM na mh. mpendazote ndio kaona wakati huo ndio huu. tunamtakia kila la heri. lakini wapinzani wasitarajie lolote la maana kutokana na ujio wake. ccj hawatashiriki uchaguzi huu na chadema hawataweza kuongeza ushindi wao kwa kiasi kikubwa hivyo mwisho wa uamuzi kama huu ni kama ule wa augustine mrema.

kila la heri
 
Ni mapema mno kusema, tusubiri tuone kwa vile ishara zimeanza kujitokeza.
 


Naomba uyakumbuke haya maneno yako vizuri
 

Mkubwa,
Mbona unasikitika sana Mpendazoe kuhama sisiemu? Unasema ni uamuzi mbaya, kwa mujibu wa nani? Mpendazoe ama wewe?
Katiba inamruhusu kuhama kadri atakavyo, ilimradi havunji sheria za nchi. Ametumia haki yake ya kikatiba.
 
Mwache aende zake - ameshakuwa "liability" na angebakia CCM "tungempiga chini" katika kura za MAONI!

OFF Topic: TuskerBariiiidi? Siku hizi sikuoni mitaa yetu ya Meeda na B-Bar! Au kwa sababu Tusker imekuwa adimu?

Ni haki ya kikatiba ya kila Mtanzania kujiunga na chama chochote apendacho.Liability ni wale wanaoiba fedha za umma na kuzitumia kujipatia ushindi kwenye chaguzi!
Mpendazoe anastahili pongezi kwa kuamua kuondokana na CCM iliyojaa unafiki na uozo!
 
mai mai lazima ameona mbali angekuwa mroho angesubiri bunge livunjwe achukue chake atangaze, nadhani ni mzalendo halisi anafaa aigwe. si si emu tumewazoea na maneno yenu sizitaki mbichi hizi...
 

Mawazo finyu! Sidhani kwamba Mpendazoe alichowaza ni kupata ushindi wa aina yoyote. Anajua yaliyo mbele yake lakini ameamua liwalo na liwe. Tunapenda watu ambao wako tayari ku-sacrifice 'luxuries' za kuwemo ndani ya CCM kwa ajili ya kutetea misimamo yao. Hongera Mpendazoe!
 
Does this prove something about CCJ?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…