Elections 2015 Fredrick Mwakalebela kipenzi cha wana Iringa kuchukua jimbo.

Elections 2015 Fredrick Mwakalebela kipenzi cha wana Iringa kuchukua jimbo.

Rich Pol

JF-Expert Member
Joined
Oct 11, 2013
Posts
7,874
Reaction score
5,685
ALIYEKUWA Katibu Mkuu wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Fredrick Mwakalebela mwishoni mwa wiki iliyopita alichukua fomu ya kuwania ridhaa ya ubunge wa Jimbo la Iringa mjini na kuwatahadharisha wenzake kuacha siasa za majitaka zinazofanywa na baadhi ya watangaza nia.
Mwakalebela ambaye mwaka 2010 alijitosa kuwania ubunge katika jimbo hilo ambapo alikusanya idadi kubwa ya waliomshabikia na kumhitaji lakini kutokana na baadhi ya changamoto zilizojitokeza alishindwa kuwatumikia alisema bado ana dhamira ya kuwatumikia Iringa mjini kwa sababu bado ana dhamira ya kweli kuwaletea maendeleo wakazi wa jimbo hilo.
Alisema siasa za majitaka zitasababisha kuligawa jimbo hilo kwa Wapinzani ambao macho na masikio yao wameyatega katika chama hicho kinachoshikilia dola.
Mwakalebela alisema Iringa mjini kuna changamoto nyingi ambazo zinatakiwa kutekelezwa kupitia ilani ya Chama cha Mapinduzi (CCM) hivyo wao kama wagombea wazingatie ilani hiyo ili kutolipoteza kwa mara nyingine jimbo hilo.
Aidha Mwakalebela alisema iwapo atashindwa kupata ridhaa ya wakazi wa Iringa Mjini yuko tayari kutoa ushirikiano kwa atakayefanikiwa kupata ridhaa kwa sababu wana CCM wanatakiwa kuwa na nguvu moja ambayo inatakiwa kupata ushirikiano.
“Nachukizwa na siasa za majitaka kwa sababu hazitusaidii hasa kwa changamoto tulizonazo ambazo zinatakiwa kutatuliwa na watia nia kama Mwakalebela na wengine ambao wana dhamira ya kufikia ujumbe wa jamii bungeni,” alisema Mwakalebela.
Mwakalebela mwenye marafiki Uswisi, Australia, America, Denmark, Qatar, Hispania na Scandinavia anajitakasa kupitia mafanikio aliyoyatekeleza alipokuwa TFF ametoa wito kwa wakazi wa Iringa kutofanya makosa kama yaliyotokea mwaka 2010.
Mwakalebela aliyasema hayo muda mfupi baada ya kuchukua fomu ya kuwania ridhaa hiyo aliyoichukua CCM Mkoani Iringa ambako alilakiwa na mashabiki lukuki waliojitokeza kumsindikiza.
 

Attachments

  • 1437211290963.jpg
    1437211290963.jpg
    8 KB · Views: 687
Mwizi mkubwa huyu tangia akiwa TFF,kamwe wanairinga hatuwezi kumpa,ukuu wa wilaya wa viti maalumu asante Shemeji unamtosha,Iringa tuna imani na Mchungaji Msigwa
 
Huyu mzee ni bora angeboresha vitega uchumi vyake vinavyopotea sasa.

Kipind cha sport kizazaa ITV alishindwa kukilipia, sasa ubunge ataweza kuwatumikia watu kweli?

Mwili mkubwa akili hakuna.
 
MSIGWA TENA 2015.

hayupo mtu atakayeliwakilisha vyema jimbo la Iringa kama mch Peter Msigwa

Tunamuamini na katuonyesha yale tuliyokuwa tunayataka Iringa now imeingia katika duru ya mafanikio makubwa

Namuombea kwa Mungu huyu mbunge wangu Mungu ampe maisha marefu na nina imani atamjalia tu


Iringa niyetu sote na mchungaji Msigwa katutosheleza sote tupo nyuma yako mchungaji
 
Msingwa ni brand ya iringa ameitendea kazi ubunge wake.kama mtu kasndwa tff itakuwa ubunge?
 
Hivi Msigwa amefanya kitu gani pale Iringa kwa miaka yote mitano?
 
Ukuu wa Wilaya anauacha lini*?!! Si ni hivi punde tu alipewa u-DC na Kikwete??!!
 
ALIYEKUWA Katibu Mkuu wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Fredrick Mwakalebela mwishoni mwa wiki iliyopita alichukua fomu ya kuwania ridhaa ya ubunge wa Jimbo la Iringa mjini na kuwatahadharisha wenzake kuacha siasa za majitaka zinazofanywa na baadhi ya watangaza nia.
Mwakalebela ambaye mwaka 2010 alijitosa kuwania ubunge katika jimbo hilo ambapo alikusanya idadi kubwa ya waliomshabikia na kumhitaji lakini kutokana na baadhi ya changamoto zilizojitokeza alishindwa kuwatumikia alisema bado ana dhamira ya kuwatumikia Iringa mjini kwa sababu bado ana dhamira ya kweli kuwaletea maendeleo wakazi wa jimbo hilo.
Alisema siasa za majitaka zitasababisha kuligawa jimbo hilo kwa Wapinzani ambao macho na masikio yao wameyatega katika chama hicho kinachoshikilia dola.
Mwakalebela alisema Iringa mjini kuna changamoto nyingi ambazo zinatakiwa kutekelezwa kupitia ilani ya Chama cha Mapinduzi (CCM) hivyo wao kama wagombea wazingatie ilani hiyo ili kutolipoteza kwa mara nyingine jimbo hilo.
Aidha Mwakalebela alisema iwapo atashindwa kupata ridhaa ya wakazi wa Iringa Mjini yuko tayari kutoa ushirikiano kwa atakayefanikiwa kupata ridhaa kwa sababu wana CCM wanatakiwa kuwa na nguvu moja ambayo inatakiwa kupata ushirikiano.
“Nachukizwa na siasa za majitaka kwa sababu hazitusaidii hasa kwa changamoto tulizonazo ambazo zinatakiwa kutatuliwa na watia nia kama Mwakalebela na wengine ambao wana dhamira ya kufikia ujumbe wa jamii bungeni,” alisema Mwakalebela.
Mwakalebela mwenye marafiki Uswisi, Australia, America, Denmark, Qatar, Hispania na Scandinavia anajitakasa kupitia mafanikio aliyoyatekeleza alipokuwa TFF ametoa wito kwa wakazi wa Iringa kutofanya makosa kama yaliyotokea mwaka 2010.
Mwakalebela aliyasema hayo muda mfupi baada ya kuchukua fomu ya kuwania ridhaa hiyo aliyoichukua CCM Mkoani Iringa ambako alilakiwa na mashabiki lukuki waliojitokeza kumsindikiza.

May be angekuwa anajua kuimba wangempa ukurugenzi wa TOT
 
ALIYEKUWA Katibu Mkuu wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Fredrick Mwakalebela mwishoni mwa wiki iliyopita alichukua fomu ya kuwania ridhaa ya ubunge wa Jimbo la Iringa mjini na kuwatahadharisha wenzake kuacha siasa za majitaka zinazofanywa na baadhi ya watangaza nia.
Mwakalebela ambaye mwaka 2010 alijitosa kuwania ubunge katika jimbo hilo ambapo alikusanya idadi kubwa ya waliomshabikia na kumhitaji lakini kutokana na baadhi ya changamoto zilizojitokeza alishindwa kuwatumikia alisema bado ana dhamira ya kuwatumikia Iringa mjini kwa sababu bado ana dhamira ya kweli kuwaletea maendeleo wakazi wa jimbo hilo.
Alisema siasa za majitaka zitasababisha kuligawa jimbo hilo kwa Wapinzani ambao macho na masikio yao wameyatega katika chama hicho kinachoshikilia dola.
Mwakalebela alisema Iringa mjini kuna changamoto nyingi ambazo zinatakiwa kutekelezwa kupitia ilani ya Chama cha Mapinduzi (CCM) hivyo wao kama wagombea wazingatie ilani hiyo ili kutolipoteza kwa mara nyingine jimbo hilo.
Aidha Mwakalebela alisema iwapo atashindwa kupata ridhaa ya wakazi wa Iringa Mjini yuko tayari kutoa ushirikiano kwa atakayefanikiwa kupata ridhaa kwa sababu wana CCM wanatakiwa kuwa na nguvu moja ambayo inatakiwa kupata ushirikiano.
“Nachukizwa na siasa za majitaka kwa sababu hazitusaidii hasa kwa changamoto tulizonazo ambazo zinatakiwa kutatuliwa na watia nia kama Mwakalebela na wengine ambao wana dhamira ya kufikia ujumbe wa jamii bungeni,” alisema Mwakalebela.
Mwakalebela mwenye marafiki Uswisi, Australia, America, Denmark, Qatar, Hispania na Scandinavia anajitakasa kupitia mafanikio aliyoyatekeleza alipokuwa TFF ametoa wito kwa wakazi wa Iringa kutofanya makosa kama yaliyotokea mwaka 2010.
Mwakalebela aliyasema hayo muda mfupi baada ya kuchukua fomu ya kuwania ridhaa hiyo aliyoichukua CCM Mkoani Iringa ambako alilakiwa na mashabiki lukuki waliojitokeza kumsindikiza.

Changamoto zip mkuu.....mbona huwek ukweli hadharan?
Au ndo upo kazin apa???
Weka mambo bayana bhana, hii ni JF, sio fb au IG
 
Mwakalebela nafasi yake ilikua 2010 awalaani waloMKATA 2010

Tunasubiri Masenemare
 
kwa uchunguzi nilioufanya ni kwamba ndugu mwakalebela hajawahi kushinda uchaguzi wowote ule aloshiriki kihalali , tuanze na uongozi wa darasa ( monitor ) hadi uongozi wa kwaya ya vijana ya kanisa analosali , ana bahati moja tu ya kuteuliwa , kuanzia Tff na u dc , na wachunguzi wa mambo ya mikosi wanabainisha wazi kwamba mambo haya yakimkuta mwanadamu huwa hayambanduki .
 
Back
Top Bottom