Hahaha kipindi hiko ghetto langu nimebadika magazeti ya wanamuziki waliochambuliwa na waandishi! Kiss Fm kwenye Top 30 ilikuwa hainipiti.Nilikuwa sikosi Kusikiliza Kiss FM Weekend Top 30 kila Jumamosi na Hollywood Hamilton miaka ya 2000s.
za huko mkuu? unajua kile kipindi cha kiss fm siku ya jumamosi au jumapili (sikumbuki vizuri) mchana hivi kinakuwa na mtangazaji wa uingereza? kinaitwaje?Mara zote naitamani Kiss Fm ya 2010 kurudi nyuma
Asubuhi unaanza na John Karani JK na mwanadada fulani simkumbuki. Baada ya hapo ni Kiss Prime Time
The Big Fuse na Captain JML Joachim Munga Luguru (alikua anasema "keep on your inner ear and get terrifying"). Alikua na DJ Jeff Jerry...noma sana
Baadaye hii show alirithiwa na Ezden The Rocker,akaibadili jina na ikaitwa Bongo Collabo Mix Show. Hakuiharibu sana
Saa tano kamili tunapata News from the BBC na show inaendelea mpaka saa sita. Hapo tunapata show ya afternoon mpaka saa nane
Kuanzia saa nane ni Kiss Hot Wire na Dj Chriss...we acha kabisa
Saa kumi ni Kiss Drive. Ilikua na mtangazaji bonge moja la vocalist Dunia nzima Tobby The Splash! Huyu jamaa sijaona mfano wake mpaka sasa.
Show ya Tobby iliisha saa kumi na mbili jioni. Hapo aliingia Dee Seven na African Beat...mitamboni alikuwepo DJ Maliz..kulikua na jingle ya miluzo...fyuu fyuuuuuu...! acha kabisa Mangi. Hii ilikua ndio show pekee ya kiswahili kwa hii redio. Ilisimamisha mitaa yote na daladala zote Dodoma enzi hizo. Mji mzima iliskika sauti moja tu ya Kiss FM
Saa mbili kamili show iliisha. Aliingia mwanamama Sharbano Aboubakar "Sherry" na Kiss Comfort Zone. Ilikua hatari nyingine
Kuazia saa tatu kulikua na habari za BBC na sports kama sikosei. Saa nne kamili alichukua usukani jamaa mmoja mlavidavi aliitwa Gody B The Pilot na show iliitwa Love Zone! Acha kabisa arif...
Weekends waliungana na redio za marekani. Show ya Ryan Seacrest ya American Top 40 ilirushwa Mubashara. Kulikua pia na Weekend Top 30. Jumamosi kulikua na sebene mix za kufa mtu kuanzia saa tisa mchana
Walikua na best DJ's...Dj Maliz,DJ Devi,DJ Jeff Jerry,DJ Chriss na wengine
Kiss FM ilivyoharibika na watangazaji wote kutimkia kusikojulikana basi nilipatwa na msongo wa mawazo!
Aliyeiloga Kiss FM alaaniwe sana! Sasa hivi redio zote zinatengeneza programu sawa tu na Clouds. Hakuna ubunifu wowote utakaomfanya msikilizaji awe na choice ya program za redio tofauti. Program za asubuhi,mchana,jioni na usiku ni zilezile kwa redio zote. Ovyo kabisa!
Fredwaa pale RFA alikua na show ya tofauti sana na ubunifu wa kipekee nje ya huu mfumo wa ki-clouds. Sasa alipoenda clouds pale alikosa kabisa emotional freedom ya kufanya makeke yake! Natamani kumwona jamaa akiwa na show yake mwenyewe kwenye redio kubwa. Energy Man is very talented! Mashabiki wake tutakua naye mpaka mwisho!
Sent using Jamii Forums mobile app
Bila shaka kipindi kiliitwa American top 40 kilitangazwa na Ryan Seacrest toka Carlifonia Marekani.Ngoma zote kali zilizokua top marekani zilipigwa pamoja na mahojiano mafupimafupi ya wasanii wa huko mbeleza huko mkuu? unajua kile kipindi cha kiss fm siku ya jumamosi au jumapili (sikumbuki vizuri) mchana hivi kinakuwa na mtangazaji wa uingereza? kinaitwaje?
Kila jumamosi ambazo hamna mpira mzuri mida ya saa kumi hadi mbili usiku ni lazima ni tunein into KIIS FM 102.7 Los Angeles kwa internet streaming ili nimsilize Ryan Seacrest na American Top 40 (AT40)Bila shaka kipindi kiliitwa American top 40 kilitangazwa na Ryan Seacrest toka Carlifonia Marekani.Ngoma zote kali zilizokua top marekani zilipigwa pamoja na mahojiano mafupimafupi ya wasanii wa huko mbele
Andika Ryan Seacrest kwa Youtube utawapata
hapana, jina siyo hili, nilishawahi kulisevu sehemu ila nimesahau, ninaomba ukikumbuka zaidi nijuze mkuuBila shaka kipindi kiliitwa American top 40 kilitangazwa na Ryan Seacrest toka Carlifonia Marekani.Ngoma zote kali zilizokua top marekani zilipigwa pamoja na mahojiano mafupimafupi ya wasanii wa huko mbele
Andika Ryan Seacrest kwa Youtube utawapata
Alisha rehemika kwa ajali ya gari njia panda ya kawe mdaa tuu mkuuJamaa kapotea sana
Say R.I.PJamaa kapotea sana
Duuh!!! sikujua kwa kweli, Mungu amlaze mahali pema peponi.Alisha rehemika kwa ajali ya gari njia panda ya kawe mdaa tuu mkuu
Rest in peace ndugu yetuSay R.I.P
Duuh!! R . I. P kwake.Fred Fidelis alishafariki mkuu! Ilikua mwezi wa tano au mwezi wa sita mwaka huu! Ilikua ajali ya gari pale Kawe! Mdogo wake Conrad ndiyo alikua dereva siku hiyo! Na ilikua Jumapili kama ya leo
Sent from my TECNO KC8 using JamiiForums mobile app
Duh..apumzike kwa amaniYeye alikuwa akiendeshwa but alikuwa kalewa, pia dereva aliekuwa akiendesha ambae ni ndugu yake alikuwa kalewa pia, watu wanamengi vifuani mwao ila hawapati watu sahihi wakuwashirikisha.
Mwamba alikuwa anapitia wakati mgumu na tangu April Clouds ilivopitisha panga na yeye alikuwemo, Kifo hakina maandalizi.