The Palm Beach
JF-Expert Member
- Dec 30, 2015
- 1,967
- 4,267
Kwani ulitaka wakilipwa wakujulishe?Mbona hizi fidia ni kama zinatajwa tu kwenye mahakama lkn hazilipwi?
1. Bilioni 5 the late Membe toka kwa Musiba ....kimya.
2. Bilioni 5 za Masoud Kipanya toka kwa Mwijaku.....kimya.
3. Na sasa ni bilioni 5 za Mbowe toka kwa Msigwa.....
Labda iwe hivyoMsigwa ni mbunge, kosakosa DC.
Kumbe kuukubali uongo ni "political tolerance"!!??Sasa kutajwa na msigwa tu alipwe bil5 siku akiwa rais huyo mbowe wenu wananchi si tutalipishwasana hozo bil5? Ina maana mbowe na wafuasi wenu hamna political tolerance?
Kama anamwita Samia mwizi na si mwizi kweli, basi Samia anayo haki na kila sababu ya kwenda mahakamani ili kudai jina lake lisafishwe, lakini kama hajaenda mahakamani, haimaanishi mwingine akiitwa mwizi wakati si kweli, asiende mahakamani.Yeye ni kiongozi wa umma kama hataki kuitwa mwizi wakati kweli chama kinapokea ruzuku lakini hata ofisi hakina achane na siasa akakoroge mbege machame
Mbona yeye anamuita Samia mwizi?
Ulikisoma ulichokiandika na kukielewa kweli kabla ya kutuletea JF!!??Aliyosema Mchungaji ni mambo ambayo yanaonekana ni yeye tu bw.Mbowe aweze kujificha.chama anadai ni cha kidemokrasia lakini ni mara ya 5 anang'ang'ana kwenye kichwa lazima ana jambo lake.na kwa taarifa yenu sasa mbowe ndiye mwenye kukiongezea ccm pumzi tangu zamani na kwa sababu hii ccm itadumu sana hata mbowe atakapoirudia nchi.
Ushahidi wa kuwa madai ya Msigwa ni uongo si utatolewa na upande wa Mbowe (KM Mnyika ataitwa kama shahidi), au ushahidi wa madai ya Msigwa kuwa ni kweli utatolewa na Msigwa (hapa napo KM Mnyika anaweza kuitwa kama shahidi kuthibitisha madai ya Msigwa kama ni kweli ama la, ndipo vielelezo vya ukweli au uongo kuwekwa hadharani na mwisho wa siku hoja zake Msigwa zinakuwa zimejibiwa mbele ya chombo ambacho uongo ni kosa kisheria).Mahakama inaenda kusikiliza madai ya Mwenyekiti kwamba amechafuliwa.
Hoja za msigwa zinapaswa kujibiwa na chama kupitia katibu mkuu kama ambavyo Lissu alipendekeza.
Lissu aliomba hoja za msigwa zijibiwe kabla hata ya sakata hili la kupelekana mahakamani, lakini Mnyika na ofisi yake hawakufanya hivyo.Ushahidi wa kuwa madai ya Msigwa ni uongo si utatolewa na upande wa Mbowe (KM Mnyika ataitwa kama shahidi), au ushahidi wa madai ya Msigwa kuwa ni kweli utatolewa na Msigwa (hapa napo KM Mnyika anaweza kuitwa kama shahidi kuthibitisha madai ya Msigwa kama ni kweli ama la, ndipo vielelezo vya ukweli au uongo kuwekwa hadharani na mwisho wa siku hoja zake Msigwa zinakuwa zimejibiwa mbele ya chombo ambacho uongo ni kosa kisheria).
Kesi tamu sana hii, UTABIRI, ITAPELEKEA ANGUKO LA MWENYEKITI, STAY TUNES!Lissu aliomba hoja za msigwa zijibiwe kabla hata ya sakata hili la kupelekana mahakamani, lakini Mnyika na ofisi yake hawakufanya hivyo.
Ngoja tuone labda huko mahakamani panaweza kuwa sehemu sahihi ya kumaliza utata huu.
Mchungaji nani??🤣🤣🤣Ni sahihi Mkuu
Wanasema nitapiga Mchungaji na kundi lote la Kondoo kutawanyika
Huyu dingi ana matatizoYale yale kama ya kinana na Msigwa hadi akaomba poo... ndilo linaloenda kutokea... Msigwa fanya uungwana mapema kabla mambo hayajawa mambo... kuomba msamaha nayo ni heri, sijui kama unazo hizo billion tano, labda kama mpango ni kukufilisi hadi nyumba....
MwenyekitiMchungaji nani??🤣🤣🤣
Imeandikwa kitaalamu kabisa.1 Kwamba anaiba pesa za chama kwa kutumia Mbowe Foundation
2. Amegeuza chama kuwa SACCOS yake
3. Chadema digital inamilikiwa na Mbowe kwa manufaa yake
My take: hilo nililitegemea and that is the right way to go!
=====
Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Freeman Mbowe amempa siku tano aliyekuwa mwenyekiti wa CHADEMA Kanda ya Nyassa, Mchungaji Peter Msigwa, kuomba radhi, asipfanya hivyo ajiandae kulipa kulipa fidia ya shilingi bilioni 5 Mahakamani kutokana na madai ya kumkashifu na kuharibu chapa yake kutokana na matamshi ya Msigwa yaliyotolewa hadharani baada ya kuhamia Chama Cha Mapinduzi (CCM).
Katika barua (notisi ya madai) iliyotolewa Septemba 2, 2024 ikiwa na sahihi ya tarehe 4 Septemba, 2024, mawakili wa Mbowe ambao ni Hekima Mwasipu na wenzake kutoka Matwiga Law Chambers, Msigwa anadaiwa kutoa matamshi ya uongo na kumchafua Mbowe mbele ya umma.
“Msigwa alitumia majukwaa ya mikutano, vyombo vya habari, na hata mitandao ya kijamii kutoa madai ya kumkashifu mteja wetu,” ameleza Wakili Mwasipu.
Imeelezwa kuwa Msigwa alidai kuwa Mbowe ameanzisha "Mbowe Foundation," na anatumia chama cha CHADEMA kwa manufaa yake binafsi. Katika moja ya mikutano yake, Msigwa alinukuliwa akisema, "Mwenyekiti wa CHADEMA amegeuza chama kuwa SACCOS, fedha za chama zinaishia kwenye taasisi binafsi na si kwenye akaunti za chama.”
Mawakili wa Mbowe wameeleza kuwa matamshi hayo yameathiri sifa ya Mbowe ndani na nje ya Tanzania, hasa kutokana na nafasi zake mbalimbali kimataifa, ikiwa ni pamoja na kuwa Naibu Mwenyekiti wa Umoja wa Vyama vya Kidemokrasia vya Afrika (DUA).
“Mteja wetu anaona maneno yote yanayozungumzwa na kunukuliwa hapo juu katika maana yake ya asili, muktadha na misemo kuwa ni kashfa, dharau na kudhuru sio tu sifa yake binafsi bali pia kwa familia yake yote, marafiki, taaluma (Siasa), Jumuiya ya Biashara, Jumuiya ya Kidini, marafiki na rika. Maneno haya si chochote lakini ushahidi dhahiri wa nia mbaya dhidi ya mteja wetu”, imeelezwa na mawakili.
Mbali na hilo, Msigwa alidai kuwa CHADEMA Digital ambayo ni huduma ya usajili wa wanachama, inamilikiwa na kampuni binafsi na kwamba Mbowe anatumia fedha za chama kwa manufaa binafsi.
“Hali hii imeleta hasara kubwa kwa mteja wetu kwani sifa yake ya kiongozi wa kisiasa, mfanyabiashara na mwanafamilia imeathirika sana,” alisema Mwasipu.
Kwa mujibu wa notisi hiyo, Msigwa anatakiwa kuomba radhi kupitia machapisho katika magazeti mawili; moja lenye kuweza kufikia nchi nzima na lingine ambalo linaweza kuwafikia watu walau wa kanda, na kulipa fidia ya Shilingi bilioni 5, la sivyo hatua kali za kisheria zitachukuliwa.
Pia soma
View attachment 3088571View attachment 3088572View attachment 3088573View attachment 3088574View attachment 3088575View attachment 3088576View attachment 3088577
- Freeman Mbowe amdai Mchungaji Peter Msigwa bilioni 5 kwa kumkashifu na kumchafulia jina lake
- Peter Msigwa: Msajili wachunguze CHADEMA, wana vikundi vinaitwa ZOO na JOB. Mbowe ni Nkurunziza
- Mchungaji Msigwa: Nitazunguka Nchi nzima kuelezea Uongo wa CHADEMA
- Mchungaji Msigwa: Mbowe siyo Msakata Rhumba maarufu ndio sababu hadi sasa bado yuko Jukwaani japo muda umeisha!
- Peter Msigwa: CHADEMA idhibitiwe kabla haijaleta vurugu nchini
- Mchungaji Msigwa akiri kumsingizia Kinana ujangili, amwangukia na kumwomba radhi
Mnyika na ofisi yake wanawajibika kujibu hoja zinazoelekezwa CHADEMA tu na si kwa mtu binafsi - tena kwa utaratibu rasmi wa kiutendaji, si kwenye majukwaa ya kisiasa. Itakuwa kituko Mnyika akikurupuka kuja hadharani na mafaili ya chama kujibu porojo zinazoenezwa na Msigwa mitaani kumhusu Mbowe. Katibu Mkuu makini wa chama kikuu cha upinzani hawezi kuwa zoba kiasi hicho.Lissu aliomba hoja za msigwa zijibiwe kabla hata ya sakata hili la kupelekana mahakamani, lakini Mnyika na ofisi yake hawakufanya hivyo.
Ngoja tuone labda huko mahakamani panaweza kuwa sehemu sahihi ya kumaliza utata huu.
Sasa si ukweli utajulikana mahakamani mara hii mnasema Mbowe akiwa raisMbowe kama kuambiwa ukweli kidogo tu anakimbilia mahakamani badala ajibu hoja na kujisafisha je siku akiwa Rais ataweza kuvumilia maneno? Au ndo atapeleka kila mwananchi mahakamani na ikiwezekana kuwa mtekaji pia