Freeman Mbowe anamjaribu Rais Samia kwa sababu hizi...

Freeman Mbowe anamjaribu Rais Samia kwa sababu hizi...

MenukaJr

Member
Joined
Apr 24, 2021
Posts
50
Reaction score
128
Freeman Aikael Mbowe, Mwenyekiti wa CHADEMA Taifa akiwa Arusha licha ya kutumia muda mwingi kumsimanga JPM, ambaye hawezi kujitetea tena amemjaribu Rais Samia Suluhu Hassan.

Freeman Mbowe amesema kuwa Chama chake hakitashiriki uchaguzi wowote kuanzia sasa hadi pale itakapopatikana Katiba mpya. Amesisitiza, wanataka Katiba Mpya kabla ya Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025 na hawatasubiri itokee kwa hiari isipokuwa wataidai, watapambana kuipata. Kwa maneno haya ya Freeman ni kwamba, Chama chake kitahakikisha Katiba mpya inapatikana kwa njia yoyote, iwe halali au haramu. Haya ndio mambo JPM alikua anakataa. Freeman Mbowe anamjaribu Rais Samia, anataka kujua ubavu wake katika kutumia mamlaka ya Urais.

Freeman Mbowe anamjaribu Rais kwa sababu zifuatazo;
MOJA
Freeman Mbowe anafahamu kuwa Rais Samia amerithi uchumi mbovu wa nchi ulioathiriwa na janga la corona. Rais mwenyewe amerudia mara kadhaa kwamba mambo mengi katika nchi yetu hayawezi kufanyika kwa sababu ya mdororo wa uchumi uliofishwa na corona katika nchi yetu na Duniani kote. Kwa uchumi huu, hakuna Rais anaweza kuongeza agenda nyingine yenye kuhitaji pesa nyingi. Hiyo bajeti haiwezi kupatikana kwa sasa kama maneno ya Rais kuhusu hali ya uchumi ni ya kweli.

Kwa vyovyote vile kumtaka Rais aanzishe mchakato au aendeleze mchakato wa Katiba mpya katika uchumi wa namna hii ni kumjaribu. Watumishi watamshangaa ikiwa tumeshindwa kuwaongeza mishahara halafu tupeleke pesa nyingi kwenye jambo ambalo linaweza kufanyika wakati wowote.

PILI Freeman Mbowe anafahamu wazi kuwa Rais Samia Suluhu amerithi miradi mingi mikubwa yenye kugharimu pesa nyingi zaidi. Freeman anafahamu namna ambavyo Watanzania wanategemea miradi hii kukamilishwa kwa wakati kama ilivyokusudiwa. Rais mwenyewe amekiri hadharani kwamba atasimamia ukamilifu wa miradi hiyo kwa wakati. Katika nchi yenye kukamilisha miradi mingi, mikubwa yenye kutumia pesa nyingi kama hii, kumtaka Rais kuanzisha mradi mwingine wa Katiba mpya wenye kutaka pesa nyingi ni zaidi ya kumjaribu.

TATU Freeman Mbowe anafahamu kuwa Rais Samia Suluhu amebadilisha kidogo mfumo wa makusayo ya kodi katika nchi. Mfumo wa makusanyo ya kodi kwa sasa unatarajia kupunguza mapato ya nchi kwa kipindi fulani mbele. Kwa sababu hii, nchi haiwezii kuwa na mapato ya kutosha kufadhiri mambo mengi kwa mkupuo mmoja.

Tunahitaji kubana matumizi kuliko ilivyokuwa hapo awali ili nchi isitetereke. Hatuwezi kukopa pesa ughaibuni kwa ajili ya kutengeneza Katiba yetu kwa sababu mashart ya mikopo yanaweza kutupangia aina ya Katiba ya kutengeneza. Hii ni sababu nyingine ya wazi kwamba sharti la Freeman Mbowe kwa Rais Samia ni jaribu kubwa.

Ushauri kwa Rais Samia Suluhu Hassan:
1. Ni lazima ajitokeze kuonesha rangi yake. Wapinzani wasipoifahamu rangi yake wanaweza kumyumbisha. Wapinzani wa nchi hii hawana utulivu, wanaweza kuomba ukutane nao kuzungumza huku wakikutukana kwenye mikutano yao. Wanaweza kutaka hili leo, kesho lile; yote yasiyotekelezeka. Kwa vyovyote iwavyo wanahitaji kudhibitiwa, kuoneshwa mipaka.

2. Ni lazima Rais atoe msimamo wake mapema kuhusu Katiba mpya. Hiyo itasaidia kuinusuru nchi na hekaheka zisizo na msingi. Kama Rais anakubaliana na msimamo wa Katiba mpya tuanze mapema mchakato, kama hakubaliani nao tufunge mjadala. Tuna mambo mengi ya kufanya! Dalili zinaonesha tunaweza kuwa na nchi yenye maandamano ya kisiasa na mizozo isiyokwisha kama ilivyokuwa huko nyuma ikiwa hatukuchukua hatua mapema.

Asanteni!!

MenukaJr,
Da'slam-Tanzania.
 
Upatikanaji wa Katiba Mpya hauna uhusiano wowote na uchumi, Mbowe hamjaribu mtu yeyote, usipotoshe, sababu zote ulizoandika hapo hazina maana.

Kama mnaweza kuwalipa wale wabunge kule bungeni mishahara minono na allowances za vikao, tena mnawalipa mpaka wale wabunge hewa wasio na chama, kwanini mshindwe kuwalipa wajumbe wa bunge la katiba?

Wewe ndie unajaribu kuleta sura mbaya Mbowe aonekane anataka kuleta vurugu, wakati kimsingi Katiba Mpya ni jukumu la kila mpenda mabadiliko na ustawi wa demokrasia, tuachane na kauli za "chama dola".
 
member since 2021 april 24.

mleta mada bila shaka ni mmoja ya wanufaika wa utawala katili wa mwendazake.

anajaribu kumshawishi Mama atumie mbinu zilezile alizotumia marehemu kudhibiti upinzani ili mwisho wa siku lawama zikianza kusionekane tofauti ya utawala huu na ule uliopita.

Mama usikubali kuingia kwenye mtego huu.
 
Mbowe na wenzake warudishe kwanza hela walizokula kwenye bunge la katiba alafu mwishoni wakatoka nje
 
Wananchi wa nchi gani ndugu yangu, walisema wapi maneno hayo.
Hata mimi nashangaa maana kuna watu hata katiba iliyopo hawaijui ndio watake katiba mpya kweli? ndio wengine huona hitaji la katiba mpya ni la wanasiasa zaidi kuliko hao wananchi.
 
Mbowe angeanza kwanza kubadilisha katiba ya chama chake ambayo haina ukomo wa madaraka, katiba inayompa ubavu wa kuamua chochote na wakati wowote bila kuwashirikisha wenzake.

Ni Mbowe huyu huyu aliesababisha mchungaji Msigwa, Lisu, Lema na wengine wengi wampigie deki Lowasa barabarani ktk uchaguzi mkuu wa mwaka 2015, kabla ya Mbowe kumleta Lowasa Chadema kwa masilahi yake binafsi hao niliowataja hapo juu walikuwa ni maadui wakubwa wa Lowasa mpk kufikia hatua ya kutaka watu wanaom support Lowasa au kupinga kama ni fisadi wapimwe akili.

Mbowe huyu huyu anasema eti Chadema hakitashiriki uchaguzi mkuu wa mwaka 2025, huku makamu mwenyekiti ndugu Mbeleji alisema kwamba anajiandaa kuja kupambana na raisi Samia katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2025.

Je, ina maana Mbowe huwa hawasiliani na makamu wake kuhusu msimamo au misimamo ya chama au Mbowe kaamua kutumia ubavu wake kukiondoa chama ktk chaguzi bila kumshirikisha yoyote including Mbeleji kama alivyofanya kwa Lowasa mwaka 2015 alipomleta kugombea uraisi bila kumshirikisha katibu mkuu na chama kwa ujumla?

Huwezi kulalamika kuwa nyumba ya mwenzako inafuka moshi na wakati huo huo kwako kunateketea.
 
Freeman Aikael Mbowe, Mwenyekiti wa CHADEMA Taifa akiwa Arusha licha ya kutumia muda mwingi kumsimanga JPM, ambaye hawezi kujitetea tena amemjaribu Rais Samia Suluhu Hassan...
Unaduani Bado mpo kwenye utalawa wa kitawliwa na washamba , futa hayo mawazo tupo kwenye utawala wa mtu asiyependa kusifiwa Wala kuimbiwa nyimbo za mapambia kwamba mkiandika makala ndefu zenye kiponda upizani atawasikiliza
 
  • Nzuri
Reactions: BAK
Freeman Aikael Mbowe, Mwenyekiti wa CHADEMA Taifa akiwa Arusha licha ya kutumia muda mwingi kumsimanga JPM, ambaye hawezi kujitetea tena amemjaribu Rais Samia Suluhu Hassan...
menuka Jr, kweli wewe ni mzalendo, nafuatilia Siredi zako zipo nondo. Mwenye macho na haambiwi ona. Sisi chetu macho
 
Mkuu uko sahihi,mkulima wa pamba kama Mimi hapa nafaidaje na hiyo katiba, Halo ya uchumi ni ngumu ,rais asimsikilize huyu Dj ,by the way alishasema katiba so kipaumbele chake
 
Freeman Aikael Mbowe, Mwenyekiti wa CHADEMA Taifa akiwa Arusha licha ya kutumia muda mwingi kumsimanga JPM, ambaye hawezi kujitetea tena amemjaribu Rais Samia Suluhu Hassan...
Huna jipya katiba mpya ni muhimu sana
 
  • Nzuri
Reactions: BAK
Hizi kelele za katiba mpya ni za akina Elkael, tundu na wenzao tujiulize hii nchi ina makundi tofauti tofauti yaani, wafanya biashara, wakulima, wasanii na wafanya biashara wanafanya shughuli zao bila shida yoyote hatujaskia wanafunga maduka kisa wanataka katiba mpya,wala wakulima hatujawasikia hawaendi shambani kisa wanataka katiba mpya.

Ninachotaka kusema hao watu wenye uchu wa madaraka kwa kung'ang'ania serikali tatu na serikali za majimbo wawe magavana waache kuyumbisha wananchi kwa sababu zao binafsi na wananchi hatupo tayari kuyumbishwa na hao watu pia tumeshaona serikali ikiboresha mambo mbalimbali katika maeneo mbalimbali kama afya, elimu na miundombinu ya barabara, maji na huduma nyinginezo.

Tuwe makini na hao watu.
 
Hivi kesi ya Mbowe ya ugaidi waliyotaka kuchoma kituo cha mafuta iliishia wapi ?
 
Acha wamjaribu na kumsumbua, amekaribisha hayo matatizo yeye mwenyewe kwa kujipendekeza kwao, ameihujumu CCM na serikali kwa kuidhoofisha akihisi ndio anaonyesha nguvu yake, she’s in fake bromance with CDM, acha wafundishane raha ya unafiki.
 
1622198794839.jpeg

menuka Jr, kweli wewe ni mzalendo, nafuatilia Siredi zako zipo nondo. Mwenye macho na haambiwi ona. Sisi chetu macho
 
mkuu unaelezea habari alafu unatushawishi tuelewe kama ulivyoelewa wewe kwanini usitupe habari uache sisi wenyewe tufanye mchanganuo
 
Back
Top Bottom