Freeman Mbowe: Kutekwa kwa watu ni maelekezo kutoka juu

Freeman Mbowe: Kutekwa kwa watu ni maelekezo kutoka juu

Chachu Ombara

JF-Expert Member
Joined
Dec 11, 2012
Posts
6,067
Reaction score
10,938
Mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Mbowe akizungumza na waandishi wa habari makao makuu ya CHADEMA Mikocheni amesema

Kwa mwaka huu (2024) na sehemu ya mwaka jana (2023), wako Watanzania zaidi ya 200 katika ukanda huu na nje ya ukanda huu, ndani ya kanda hii ya Pwani, ya Dar es Salaam na nje ya kanda hii ambao hawajulikani waliko, siyo hawa 80 walioripotiwa na TLS, zaidi ya watu 200 wamepotea.

Mambo haya ni mwendelezo wa maelekezo ya viongozi wa serikali ambao huko nyuma walipata kusema shughulikeni nao yaani kwamba sasa yawezekana baadhi ya watu wamepotezwa walikuwa na jinai zinazowahusu, inawezekana, lakini hakuna jinai kwa sheria na katiba ya nchi yetu inayoruhusu vyombo vya dola kuhukumu mtu kwa jinai aliyofanya bila kumfikisha kwenye mahakama za nchi yetu.

Kwa hiyo hakuwezi kuwa kisingizio chochote kwamba huyu tuliyemshughulikia ni Panya road au ni mwizi, hakuna uhalalishaji huo, hata mwizi anapaswa kupelekwa kwenye vyombo vya sheria katika nchi yetu.
 
Natamani kuona na hao wanyonge wakianza kujitetea kwa mikono yao, dhidi ya hao watekaji wao wenye roho za kikatili na kinyama.
 
TLS, LHRC na wadau wengine... hakuna namna yakudai haki yetu ya kuwa salama sisi na Mali zetu kwa kuliwajibisha jeshi kisheria?

Na liseme au litamke kuwa limeshindwa kutekeleza wajibu wa kulinda rain na Mali zao ili raia wachukue jukumu la kujilinda wenyewe au kuunda vikundi vya kujilinda dhidi ya hatari yoyote?
 
Mpaka watoto wadogo wanapotezwa Mungu irehemu Tanganyika
Mbona Znz hayapo
 
TLS, LHRC na wadau wengine... hakuna namna yakudai haki yetu ya kuwa salama sisi na Mali zetu kwa kuliwajibisha jeshi kisheria?

Na liseme au litamke kuwa limeshindwa kutekeleza wajibu wa kulinda rain na Mali zao ili raia wachukue jukumu la kujilinda wenyewe au kuunda vikundi vya kujilinda dhidi ya hatari yoyote?

Lamadi jana wameonyesha mfano.

Ile sheria iliyopitishwa kuhusu usalama wa taifa wanaweza kuchukua hatua, lengo lake ndio lilikuwa hili la kuteka na kupoteza watu.
 
Hii nchi wasipoangalia huko mbeleni watu watakuwa kama Haiti...

Ova
Unajua hii tekateka madhara yake baadae ni makubwa tunaweza kujikuta kila sehemu tuna gangs, halafu zikiwa nyingi kudhibiti itakua shida
 
Back
Top Bottom