Freeman Mbowe: Kwenye mahoteli yetu wameajiriwa Wakenya

Freeman Mbowe: Kwenye mahoteli yetu wameajiriwa Wakenya

Nyanda Banka

JF-Expert Member
Joined
Mar 14, 2023
Posts
304
Reaction score
1,054
1721080066088.jpeg

"Mna tabia ya kufikiri Wakenya wana akili sana, Wakenya hawana akili yoyote ya maana kuliko Watanzania ila tofauti yao na sisi wale walifundishwa Kiingereza tangu chekechea kwahiyo ukienda kwenye mabenki yetu, mahoteli ya mbuga za wanyama huko wameajiri Wakenya kwa sababu waliandaliwa kushindana kwenye soko la ajira la kimataifa," - @freemanmbowetz Mwenyekiti wa CHADEMA Taifa

"Viongozi wanawaambia Watanzania wa kawaida Kiswahili ni lugha nzuri sana endeleeni kusoma Kiswahili tuenzi lugha ya Taifa ni sawa wala sisi hatupingi lakini ambacho @chadematzofficial tunatofautiana na CCM ni huu ubaguzi wa elimu, tunasema watoto wetu hawa ni lazima tuwape elimu ambayo wanaweza wakashindana na watoto wengine wowote duniani, ili watoto hawa waweze kushindana kwenye soko la ajira la dunia ni lazima wafundishwe elimu zenye lugha za kimataifa," - @freemanmbowetz Mwenyekiti wa CHADEMA

#CHADEMAArusha
 
Wakenya kawaida sana shida wabongo lugha inawapiga chenga, na lugha ndo inawafanya pia kukosa exposure.....zile battle za Twitter wabongo walikuaga wanatoka nduki, uwanja wao wa kujidai ulikua insta tu ila battle za hoja hata na Uganda tu hapo wabongo walikua wanatoka nduki
 
Hata Waliosoma Magar ya njano Ngeli kwao ni Tatizo,Nini kifanyike Na Sisi Tuandae kizazi Tishio?
 
tunatofautiana na CCM ni huu ubaguzi wa elimu, tunasema watoto wetu hawa ni lazima tuwape elimu ambayo wanaweza wakashindana na watoto wengine wowote duniani, ili watoto hawa waweze kushindana kwenye soko la ajira la dunia ni lazima wafundishwe elimu zenye lugha za kimataifa," -
Maneno mazima kabisa haya
 
Hata Waliosoma Magar ya njano Ngeli kwao ni Tatizo,Nini kifanyike Na Sisi Tuandae kizazi Tishio?
Wachina English kwao pia haipo sana lugha sio inayoleta maendeleo ila viongozi imara na wazalendo wenye maono.

Kuwa na viazi madarakani kama hawa ccm hata wananchi tuongee lugha 100 tutabakia kuwa wajinga na tusio na maendeleo tu.
 
"Mna tabia ya kufikiri Wakenya wana akili sana, Wakenya hawana akili yoyote ya maana kuliko Watanzania ila tofauti yao na sisi wale walifundishwa Kiingereza tangu chekechea kwahiyo ukienda kwenye mabenki yetu, mahoteli ya mbuga za wanyama huko wameajiri Wakenya kwa sababu waliandaliwa kushindana kwenye soko la ajira la kimataifa," - @freemanmbowetz Mwenyekiti wa CH

#CHADEMAArusha
Fact
 
Wachina English kwao pia haipo sana lugha sio inayoleta maendeleo ila viongozi imara na wazalendo wenye maono.

Kuwa na viazi madarakani kama hawa ccm hata wananchi tuongee lugha 100 tutabakia kuwa wajinga na tusio na maendeleo tu.
Hakika Tunahitaji Viongozi bora
 
Back
Top Bottom