Freeman Mbowe mwanasiasa, mfanyabiashara na mkulima asiye ogopa hasara

Hebu kamateni hiyo msimuone mtu ni wa kisport wa njaa za ruzuku.
Freeman Aikaeli Mbowe amezaliwa 14 Septemba 1961 Wilaya ya Hai mkoa wa Kilimanjaro ni mwanasiasa Mtanzania, mwanachama na mwenyekiti wa Chama cha kisiasa cha Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA).

Alikuwa mmoja wa waasisi wa CHADEMA mwaka 1992. Freeman Mbowe alikuwa mbunge wa Jimbo la Hai lililopo mkoa wa Kilimanjaro tangu mwaka 2000 hadi 2020.

Familia ya Mbowe
Freeman Mbowe alizaliwa na wazazi Aikael Alfayo Mbowe na Mama Aishi Ephraimu Shuma akiwa mtoto wa 10 kwa baba yake na mtoto wa 9 kwa Mama yake, ivyo yeye kuwa mtoto wa mwisho kwa baba na Mama.

Freeman Mbowe alibatizwa 09,12,1961 siku ya Uhuru wa Tanganyika na kupewa jina Freeman maana yake mtu huru. Baba wa Ubatizo wa Freeman Mbowe alikuwa Mwalimu Nyerere.

Nilizaliwa mwaka 1961 mwaka ambao nchi yetu ilipata uhuru tarehe 14/9/1961 na nikabatizwa siku ya 9/12/1961 siku bendera ya mwingereza yaani (Union Jack) inashushwa na mimi nikabatizwa siku ya uhuru kwa maana 1961 nikapewa maji ya uzima ya ubatizo na ndio sababu nikapewa jina la Freeman ikiwa na maana mtu huru kwa sababu nilibatizwa siku ya uhuru baada ya kuzaliwa mwaka wa Uhuru.Alisema Mbowe kwenye kipindi cha Speaking out with Tundu Lissu

Uhusiano wa Mwalimu Nyerere na familia ya Freeman Mbowe ulianzia wapi?

Kwa mujibu wa Freeman Mbowe kwenye Mahojiano kati ya Tundu Lissu na Freeman Mbowe yaliyofanyika katika kipindi cha Speaking out with Tundu Lissu, alisema kuwa Julius Kambarage Nyerere na Aikael Alfayo Mbowe walikuwa na mahusiano ya karibu sana na mahusiano yao yalianzia kwenye harakati za kutafuta uhuru wa Tanganyika.

Lissu: Hebu tuambie Mzee Mbowe alikuwa na connection gani na Mwalimu Nyerere au na mambo ya kisiasa, siasa za TANU?

Mbowe:Kwa kweli nikiri tu kwamba wakati Mzee anaanza kufanya mambo ya siasa na akina Mwalimu na wazee wenzake mimi nilikuwa bado ni mtoto mdogo sana lakini historia nimeikuta simulizi nimezipata maandiko nimeyakuta, Mzee alikuwa na mahusiano ya karibu sana na Mwalimu Nyerere na mahusiano yao yalianzia kwenye harakati za kutafuta uhuru wa Tanganyika.

Mzee Mbowe alikuwa na umashuhuri katika Tanganyika kanda ya Kaskazini katika mikoa ya Kaskazini ya Kilimanjaro, Arusha na Manyara na alikuwa na uhusiano na watawala wa kiasili, kuanzia Mangi Maruma wa Rombo, Mangi Shangali wa Machame, alikuwa karibu nao kutokana na umashuhuri wake kabla ya uhuru.

Katika mazingira kama hayo baba alikubaliana na wenzake kadhaa kuhamasisha harakati za kutafuta uhuru wa Tanganyika katika kanda ya Kaskazini kwa kuwa watawala wa jadi walikuwa na nguvu sana na walihitaji mtu ambae alikuwa na ushawishi mkubwa sana na waliweza kuingiza TANU kanda ya kaskazini hasa sehemu ya Kilimanjaro na hapo ndio mahusiano ya familia ya Mwalimu ilipoingia kwenye familia yetu na alikuwa na ukaribu hata na Oscar Kambona na wazee wengine kadha wa kadha ambao walishiriki katika harakati za uhuru wa nchi kwa hiyo historia ya Mwalimu na baba ilikuwa hivyo.

Picha mnayoona hapo huyo mwenye koti refu akisalimiana na Nyerere ni mzee Aikaeli Mbowe.Baba mzazi wa FreeMan Mbowe.Hapo ametembelewa nyumbani kwake Machame Kilimanjaro na rafiki yake mkubwa Raisi Nyerere.Angalieni huo mjengo hapo upo kijijini
 

Attachments

  • mbowe.png
    321.3 KB · Views: 4
Dah ! watu bana sasa mbowe ashike BUNDUKI ya nini ashike wapi sasa kwa ajili ya nini

Mkuu SILAHA PESA KISU MZIGO
Mtu yoyote SMART msingi kwake ni maneno
 
Una uhakika na unachokisema ?huyu mwenyekiti angekuwa na huyo utajiri wa huku Jamii forum basi


✅✅✅✅
kama umezaliwa baada ya uhuru na hukuona bendera ya union jack you have got no right to speak however you can comment and be corrected.
 
Una uhakika na unachokisema ?huyu mwenyekiti angekuwa na huyo utajiri wa huku Jamii forum ingekuwa ni hatari sana.
Wewe ukoo wenu mzima mkijikusanya hamuwezi fikia utajiri wa Mbowe siasa ni damu tu na tena usije shangaa huyu Mbowe unayemuona akawa ni Pro-CCM

Wewe ukoo wenu mzima mkijikusanya hamuwezi fikia utajiri wa Mbowe siasa ni damu tu na tena usije shangaa huyu Mbowe unayemuona akawa ni Pro-CCM
kama umezaliwa baada ya uhuru na hukuona bendera ya union jack you have got no right to speak however you can comment and be corrected.
You are trying to overate Mbowe Farmily of which I have the righty to question.
 

Pamoja na tofauti za siasa hakuna anayebisha Mbowe ni Husler
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…