From Peru to Tanzania

Alpha

JF-Expert Member
Joined
Aug 30, 2007
Posts
688
Reaction score
335

At the same time...


Sound familiar?

When will Tanzanians wake up and start fighting for what is rightfully theirs. It seems mass protest and unrest is the only way to get the message across to our so called 'leaders'
 
Heri Kutumia Akili Nyingi Na Nguvu Kidogo...... Na Si Kutumia Nguvu Nyingi Akili Kidogo ......! Tutaumia Sisi....!
 
Alpha,
Nimeona BBC wakibwabwaja kuhusu China inavyowekesha Peru na kuivamia Africa kiasi kwamba wanaita ati ni Colonising Africa hali wao Westeners wanayo makampuni mia kidogo yaliyotapakaa Africa nzima.
Kilichonichosha zaidi ni mkataba wa Peru ambao China wameingia mkataba na serikali ya Peru wakinunua shaba kwa dollar 400 kwa tani hali market rate ya shaba ni kitu kama 8,000..Nilippiga hesabu za haraka niliona hii 400 ni kitu kama asilimia 5 tu lakini mali yote bado ni ya serikali na kodi zote wanalipa including cooperate taxes kisha kuna miradi ya ujenzi a barabara, shule na hospital.
Pamoja na kwamba wameliwa lakini kuna unafuuu sana ukilinganisha na sisi tulioweka mkataba wa dhahabu tunachopewa ni ruzuku tu ya silimia 3 na bado mkulu Sinclair anakata kisu cha 1.9. Kodi ndio kama ulivyosikia hatuna kitu hadi leo hii kisha bado kuna watu wanamtetea Mkapa na uongozi wake wa CCM.
Majuzi tu, Joseph kabila pia ameingia mkataba na wachina kawafukuza ma missionaries (askari wa kukodishwa) ambao walikuwa wakilinda baadhi ya mashirika ya nchi za magharibi ambayo hayakuwepo nchini kihalali...Mkataba alioingia na China baabu kubwa kuliko mkataba wowote ambao nchi za magharibi walitoa kwanza hawakutaka kabisa kuwepo na mkataba ati kwa sababu Kongo hakuna usalama....
Nitazidi kuwakumbusha serikali yetu kwamba mnunuzi mkubwa wa dhahabu (consumer) duniani ni China sio Canada wala Marekani ipo haja kubwa ya ku deal na mnunuzi moja kwa moja bila kupitia walanguzi hawa kina Barrick!..China wana zana zote za Uchimbaji na yawezekana kuwa ni wakoloni kama walivyo nchi nyingine lakini tutazame manufaa ya madini haya kwani mwisho wa yote haya hawa wote watakuja tuachia mahandaki..Hakuna mwenye nafuu ktk mazingira ya nchi inapokuja swala la madini..
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…