FT: Ligi Kuu Bara | Dodoma Jiji FC 0-1 Simba SC | Jamhuri Stadium 22/01/2023

Jana Simba passing yetu haikuwa bora kukaa na Mpira issue sana aisee
 
Simba kuna baadhi ya wachezaji wenye miili mikubwa lakini hawana nguvu za kuitumia mfano Kennedy, Nyoni, Kyombo, afadhali hata Kibu anapambana na kutumia mwili wake vizuri kupambania na kucontrol mipira. Outtara ana mapungufu yake lakini mnamuonea.
Humuoni kuwa hana mbio, washambuliaji wenye kasi wanampita kama upepo au huangaliagi mikimbio yake ?

Tunasema ili asikie na ajirekebishe. Sio kumchukia.
Toka aje hajabadilika
 
Humuoni kuwa hana mbio, washambuliaji wenye kasi wanampita kama upepo au huangaliagi mikimbio yake ?

Tunasema ili asikie na ajirekebishe. Sio kumchukia.
Toka aje hajabadilika
Hizo mbio unazozitaka siyo za center defenders.

Mapungufu yake niliyoyaona mimi ni kutowasiliana vizuri na wenzake na mipira mingi ya juu jana ilikuwa inawapita. Nilikuwa nashangaa sana na urefu ule wa kina Outtara, Nyoni na Kennedy mipira mingi iliyokuwa ndani ya vimo vyao ilikuwa inawapita. Nadhani tatizo kubwa ni fitness siyo nzuri katika timu.

Tatizo la lugha mama mbalimbali zinazotumika na wachezaji na makocha wa Simba nadhani tunalichukulia poa ila pia linachangia sana. Wachezaji hawawezi kuwasiliana kwa lugha rahisi kati yao.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…