Mkuu ulikuwa unakatika kama kawaida, usitufanye kama hatukuwepo kipindi hiko! Mwaka 2017 kulikuwepo mgao wa umeme!Kwanini wakati wa Magufuli hakukuwa na mgao au ulikuwa uhamishoni nje ya nchi, tatizo la umeme limenza baada ya Makamba kuwa wAZIRI acha kudanganya watu..unajua mambo yaliyofanywa na makamba wizara ya nishati? unafahamu biashara anazofanya makamba na mashirika ya wizara ya wizara ya nishati?
Mkuu acha kupotosha, sio kweli hata kidogo. Matatizo ya umeme nchi Tanzania yapo kabla hata Makamba hajazaliwa.Anaweza kuchafuka sawa, lakini Makamba ndio chanzo cha matatizo ya umeme nchini. Baada ya kuonekana HAWEZI kulimaliza tatizo ndio akaondolewa. Mh. Dotto Biteko atakuwa "bangusilo"!
Mkuu kwa tafsiri yako wenye chuki ni watu wa aina gani?Hii nchi kama mamlaka za teuzi zitakuwa zinawasikiliza watu wenye chuki binafsi tutawapoteza watu wa maana Sana katika maendeleo ya nchi yetu.
Tuache siasa za chuki tutalikwamisha taifa hili na kuwapoteza watendaji wa maana kwa maslahi ya nchi.
🤪🤪🤪🤪🧑🦯Nyuso zimewashuka hawana cha kusema, maana mvua zinanyesha mpk milima inaporomoka lkn mgawo unaendelea. Dotto Biteko bure kabisa huyu.
Eti mwalimu wa primary anakuwa naibu waziri mkuu. Puaaa!
wajinga huwona werevu wapuuziHv mwl wa Primary sifa yake ni bogus kweli.hv ww hukupita primary school mdogo wangu?naomba tuache dharau kwa walimu tafadhali.
Kwani ni lini aliwahi kuwa msafi?Dotto Biteko aliteuliwa 30 August, 2023 na kuapishwa 1 September, 2023. Siku ya kuapishwa mhe rais alitoa miezi 6 kero za umeme ziwe zimemalizika.
Kimahesabu kutoka 1 September 20223 mpk leo 15 December 2023 bado miezi 2 na nusu muda uwe umeisha. Lkn sioni mipango, mikakati wala mbinu za Biteko kuondoa kadhia na kashda za umeme hapa nchini.
January Makamba akiwa waziri wa nishati alionesha mikakati, mipango, dira na mbinu za kuondoa shida na kashda za umeme. Makamba alikuwa mkweli kwa kusema kuwa itachukuwa muda kulimaliza tatizo.
Lkn maadui na mahasimu wa Makamba (ambao kwa sehemu kubwa ni sukuma gang) walikuwa wakipiga kelele kana kwamba matatizo ya umeme kayaleta Makamba. Mama akaona isiwe shida kamteua Dotto Biteko Siwasikii tena kusema ingawa matatizo yanaongezeka lkn kwa kuwa ni sukuma gang mwenzao wameufyata.
Sasa hili fupa la umeme halitamwacha salama Biteko. Litamchafua tu. Kumbukeni akina Karamagi, Msabaha, Muhongo, Ngereja, n.k. Huyu Kalemani aliponea mgongo wa udikteta wa jiwe aliyebinya uhuru wa vyombo vya habari na ule wa watu kujieleza. Vinginevyo naye angechafuka tu.
Biteko amewekwa kwenye mtego wa umeme.
Unasemaje sukuma gang?Wewe ni bogus...
Tatizo lako hujui unaye mzungumziaTutakosea tukikuita chawa wa makamba?
Ndani ya ccm hakuna mtendaji anaye wajali wahitaji wa hudumaKatika hao wote Le Profeseri Muhongo alitatua kero ya kukatika umeme ovyo na kuchelewa kupata huduma toka watu wa dharula wa TANESCO.
Mvurugano ukaanza kwa Kalemani akaja kuvuruga kila kitu Januari Makamba.