Fursa kwa serikali kuhamia Dodoma kutokana na kauli ya Magufuli siku anapewa uenyekiti wa CCM

Fursa kwa serikali kuhamia Dodoma kutokana na kauli ya Magufuli siku anapewa uenyekiti wa CCM

Nyakageni

JF-Expert Member
Joined
Feb 1, 2011
Posts
15,045
Reaction score
5,108
Wakuu naomba tujadili kwa pamoja baadhi ya fursa ambazo wajasiriamali tunaweza kuzipata. Michango yenu inaweza kuzingatia SWOT ANALYSIS ili mtu anapoandaa project plan yake iwe virahisi zaidi

Mimi kwa haraka haraka naona fursa zifuatazo

1. Guest Houses kwani watumishi wengi wataenda kule kupata huduma

2. Usafiri kama madaladala na taxi kwa sababu ya ongezeko la watu

3. Mighahawa na hotels kwa ajili ya wageni

4. Vituo vya mafuta

5. Biashara ya kuosha magari

6. Kukamata viwanja kwenye prime areas

7. Photocopiers, fax na stationery jaribu na maofisi makubwa

8. Maji ya kunywa

9. Kung'arisha viatu kabla watu hawajaingia wizarani

10. nk

Tuendelee kujadili kwa pamoja. Na watakaofanikiwa kwa baadaye si mbaya ukatoa shukrani hapa jukwaani

Karibuni sana wa ndugu
 
So far Dodoma Imekuwa Makao ya bunge na Chama tawala Miaka kadhaa.Nini Kitaongezeka?
1)Ofisi za serikali na wakala zake.
2)Watumishi Kuhamisha
3)Ujio wa Wageni wa ndani na Nje Kufuata Huduma.
Uwekezaji wa Nyumba za Makazi,Supermarkets,Gyms,Shule za Kisasa,inaweza kuwa Fursa muhimu.Migahawa (Restaurants)/Fast Food's pia itakuwa fursa.
 
hahaha!!! hizo fursa zipo tangu 1970s.
 
Wakuu naomba tujadili kwa pamoja baadhi ya fursa ambazo wajasiriamali tunaweza kuzipata. Michango yenu inaweza kuzingatia SWOT ANALYSIS ili mtu anapoandaa project plan yake iwe virahisi zaidi

Mimi kwa haraka haraka naona fursa zifuatazo

1. Guest Houses kwani watumishi wengi wataenda kule kupata huduma
2. Usafiri kama madaladala na taxi kwa sababu ya ongezeko la watu
3. Mighahawa na hotels kwa ajili ya wageni
4. Vituo vya mafuta
5. Biashara ya kuosha magari
6. Kukamata viwanja kwenye prime areas
7. Photocopiers, fax na stationery jaribu na maofisi makubwa
8. Maji ya kunywa
9. Kung'arisha viatu kabla watu hawajaingia wizarani
10. nk

Tuendelee kujadili kwa pamoja. Na watakaofanikiwa kwa baadaye si mbaya ukatoa shukrani hapa jukwaani

Karibuni sana wa ndugu

Mkuu, haya ni mawazo chanya kabisa watu kama wewe ndio mnatakiwa kuendeleza gurudumu la maendeleo.
 
blog au gazeti la kucover mambo ya kisiasa, kiuchumi, kiutawala na kijamii yanayoendelea Dodoma.

Ila kiukweli ofisi ya mkuu wa mkoa ndiyo sasa inapaswa kujitengezea "website" ambayo itakuwa na kila kitu cha kuvutia wageni na wawezekezaji mkoani humo.

Ni wakati wa Jordan Rugimbana kuchangamka.
 
Richard nakupongeza kwa wazo lako,Lakini kama kuna wajasiliamali nawaomba wachangamkie fursa ,kwa sasa anza kuwekeza kwenye viwanja,then wakianza kuhamia na wewe unaweka miundombinu iliyosemwa na mtoa maada.Nampongeza mtoa maada isipokuwa kama Mtanzania wa kuwafikilia wanyonge wenzangu nawaomba mchangamkie fursa na kuwapuuza wanaopinga hoja au kukatisha tamaa.Mungu yupo atawasaidia wenye mawazo chanya na kuwasaidia wwnye maawazo hasi wabadilike.
 
Richard naamini watu wa ofisi ya RC Dodoma kama wapo humu ndani watamfikishia ujumbe na ushauri wako muhimu sana
 
Richard nakupongeza kwa wazo lako,Lakini kama kuna wajasiliamali nawaomba wachangamkie fursa ,kwa sasa anza kuwekeza kwenye viwanja,then wakianza kuhamia na wewe unaweka miundombinu iliyosemwa na mtoa maada.Nampongeza mtoa maada isipokuwa kama Mtanzania wa kuwafikilia wanyonge wenzangu nawaomba mchangamkie fursa na kuwapuuza wanaopinga hoja au kukatisha tamaa.Mungu yupo atawasaidia wenye mawazo chanya na kuwasaidia wwnye maawazo hasi wabadilike.
I agree completely with you kukamata viwanja m muhim sana kwa sasa, hta hivyo mji WA Dodoma unakua kwa kasi sana ukilinganisha na miaka 10 iliyopita
 
Back
Top Bottom