kluger
JF-Expert Member
- Jun 16, 2016
- 2,093
- 1,899
Tanzania kumekuwa hatufanyi vizuri Kwnye mchezo wa mpira wa miguu kwa muda sasa.
Leo tunashinda, kesho tunapoteza, kesho kutwa tunasubiria mechi ya mwisho na kumsumbua Mungu kwa maombi ili kupata nafasi za kufuzu.
Tatizo kubwa ninaloliona kwa nchi yangu katika mashindano mengi kubwa ni UTIMAMU WA AKILI NA FIKIRA kwa wachezaji. Pili, ni SIASA michezoni.
Tukianza na kauli hii ya "Fyeka Burundi, tusonge mbele " niwapongeze sana waandishi wa habari za michezo, wanania njema sana.
Lakini sambamba na jitihada hizi za wanahabari, je wahusika wakuu "WACHEZAJI" wanaandaliwa vipi kiutimamu wa AKILI zao mchezoni??
Sijapata kufahamu namna ambavyo benchi la ufundi na wataalamu wengine wanawaandaaje wachezaji kisaikolojia? Mazoezi ya viungo na stamina ya mwili sina shida napo, vipi utimamu wa akili ya mchezaji kuelekea mchezo husika.
Je wanajua vizuri majukumu yao?
Je wanajua vizuri umuhimu wa mashindano yenyewe?
Je ni yapi malengo yao?
Je kama mchezaji anafahamu ubora wake au kiwango chake? Nini anatakiwa afanye kuboresha au kubakia na kiwango bora?
Mwisho, Je wanajua athari za mitandao ya kijamii dhidi ya viwango vyao? Wanalewa sifa? Wanaumizwa na maneno mabaya dhidi yao huko mitandaoni? Wanatumia muda mwingi kiasi gani Kwnye mitandao ya kijamii? Kweli wanapumzika wakati wa kupumzika? Au wanapoteza muda mitandaoni?
Haya yote yanachangia utimamu wa akili ya mchezaji.
Waandishi nao, kuliko kusifia kila kitu kuhusu timu yetu na wachezaji wetu, mnafanya uchunguzi wa timu pinzani, yapi mapungufu yao, wanajiandaaje na kipi kifanyike kuwafunga?
Nimeandika huu uzi kwa sababu sifa mnazotoa kwny makala zenu kwa wachezaji wetu saa nyingine zinawalewesha sana kabla ya mchezo na matokeo yake kuichukulia mechi katika uzito usio stahili.
Mfano Mzuri mechi ya Simba SC dhidi ya timu toka Msumbiji. Kila gazeti lilisifia timu ya Simba na wachezaji bila kuangazia wapinzani.
Matokeo yake wachezaji na mashabiki waliaminishwa matokeo bora nyumbani.
Tuache Siasa za michezoni, kusifia bila utaalamu halisi.
Kila la Heri, Taifa Stars.
Leo tunashinda, kesho tunapoteza, kesho kutwa tunasubiria mechi ya mwisho na kumsumbua Mungu kwa maombi ili kupata nafasi za kufuzu.
Tatizo kubwa ninaloliona kwa nchi yangu katika mashindano mengi kubwa ni UTIMAMU WA AKILI NA FIKIRA kwa wachezaji. Pili, ni SIASA michezoni.
Tukianza na kauli hii ya "Fyeka Burundi, tusonge mbele " niwapongeze sana waandishi wa habari za michezo, wanania njema sana.
Lakini sambamba na jitihada hizi za wanahabari, je wahusika wakuu "WACHEZAJI" wanaandaliwa vipi kiutimamu wa AKILI zao mchezoni??
Sijapata kufahamu namna ambavyo benchi la ufundi na wataalamu wengine wanawaandaaje wachezaji kisaikolojia? Mazoezi ya viungo na stamina ya mwili sina shida napo, vipi utimamu wa akili ya mchezaji kuelekea mchezo husika.
Je wanajua vizuri majukumu yao?
Je wanajua vizuri umuhimu wa mashindano yenyewe?
Je ni yapi malengo yao?
Je kama mchezaji anafahamu ubora wake au kiwango chake? Nini anatakiwa afanye kuboresha au kubakia na kiwango bora?
Mwisho, Je wanajua athari za mitandao ya kijamii dhidi ya viwango vyao? Wanalewa sifa? Wanaumizwa na maneno mabaya dhidi yao huko mitandaoni? Wanatumia muda mwingi kiasi gani Kwnye mitandao ya kijamii? Kweli wanapumzika wakati wa kupumzika? Au wanapoteza muda mitandaoni?
Haya yote yanachangia utimamu wa akili ya mchezaji.
Waandishi nao, kuliko kusifia kila kitu kuhusu timu yetu na wachezaji wetu, mnafanya uchunguzi wa timu pinzani, yapi mapungufu yao, wanajiandaaje na kipi kifanyike kuwafunga?
Nimeandika huu uzi kwa sababu sifa mnazotoa kwny makala zenu kwa wachezaji wetu saa nyingine zinawalewesha sana kabla ya mchezo na matokeo yake kuichukulia mechi katika uzito usio stahili.
Mfano Mzuri mechi ya Simba SC dhidi ya timu toka Msumbiji. Kila gazeti lilisifia timu ya Simba na wachezaji bila kuangazia wapinzani.
Matokeo yake wachezaji na mashabiki waliaminishwa matokeo bora nyumbani.
Tuache Siasa za michezoni, kusifia bila utaalamu halisi.
Kila la Heri, Taifa Stars.