Mkalukungone mwamba
JF-Expert Member
- Aug 29, 2022
- 862
- 1,755
Mbunge wa Arusha Mjini, Mrisho Mashaka Gambo, ameongoza wanachama na wafuasi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) katika uzinduzi wa kampeni za uchaguzi wa serikali za mitaa katika jimbo lake, akisisitiza umuhimu wa uwajibikaji na utumishi wa kweli kwa wananchi.
Akizungumza wakati wa kampeni hizo, Gambo amewataka wenyeviti wa serikali za mitaa watakaoshinda katika uchaguzi huo kutekeleza majukumu yao kwa uwazi na uadilifu, badala ya kujinufaisha kupitia mihuri ya serikali.
Mbunge huyo ameeleza kuwa mwenyekiti wa serikali ya mtaa hana mishahara rasmi bali anapata posho, hivyo ni muhimu kwa wagombea kuelewa kuwa nafasi hiyo si ya kutafuta maslahi binafsi.
Soma Pia:
Aidha, Gambo ametoa wito kwa wenyeviti hao kuhakikisha kuwa vijana, wanawake, na watu wenye ulemavu katika mitaa yao wananufaika na mikopo inayotolewa na halmashauri ya Jiji la Arusha.
Akizungumza wakati wa kampeni hizo, Gambo amewataka wenyeviti wa serikali za mitaa watakaoshinda katika uchaguzi huo kutekeleza majukumu yao kwa uwazi na uadilifu, badala ya kujinufaisha kupitia mihuri ya serikali.
Mbunge huyo ameeleza kuwa mwenyekiti wa serikali ya mtaa hana mishahara rasmi bali anapata posho, hivyo ni muhimu kwa wagombea kuelewa kuwa nafasi hiyo si ya kutafuta maslahi binafsi.
Soma Pia:
- Special Thread: Orodha ya Mijadala ya Mikoa yote Tanzania Bara inayoshiriki katika Uchaguzi wa Serikali za Mitaa 2024
- Arusha: Mrisho Gambo amuahidi Rais Samia kulinda mitaa kwenye Uchaguzi Wa Serikali Za Mitaa ili kutengeneza jeshi kwenye Uchaguzi Mkuu
Aidha, Gambo ametoa wito kwa wenyeviti hao kuhakikisha kuwa vijana, wanawake, na watu wenye ulemavu katika mitaa yao wananufaika na mikopo inayotolewa na halmashauri ya Jiji la Arusha.