Cute Wife
JF-Expert Member
- Nov 17, 2023
- 1,906
- 5,000
Wakuu,
Mbunge wa Jimbo la Arusha Mjini, Mrisho Mashaka Gambo, ameonesha kujali changamoto zinazowakabili waendesha bodaboda jijini Arusha kwa kuchangia shilingi milioni 2 kwa ajili ya kulipia kodi ya ofisi ya chama chao hadi kuanzia Februari hadi Disemba 2025.
Hatua hiyo imekuja baada ya kukutana na viongozi wa waendesha bodaboda na kujadiliana changamoto wanazopitia katika shughuli zao za kila siku. Gambo amesema changamoto ya kodi ya ofisi ilihitaji ufumbuzi wa haraka ili kuepuka kero kwa waendesha bodaboda.
Kupata taarifa na matukio ya kimkoa kuhusu Uchaguzi Serikali za Mitaa ingia hapa: LGE2024 - Special Thread: Orodha ya Mijadala ya Mikoa yote Tanzania Bara inayoshiriki katika Uchaguzi wa Serikali za Mitaa 2024
Mbali na mchango huo wa fedha, Gambo pia amekabidhi televisheni ya inchi 32 kwa ofisi ya chama cha bodaboda ili waendesha bodaboda waweze kufuatilia matukio mbalimbali yanayoendelea duniani. Vilevile, ametoa viti vya ofisini kwa ajili ya kuboresha mazingira yao ya kazi.
Mbunge wa Jimbo la Arusha Mjini, Mrisho Mashaka Gambo, ameonesha kujali changamoto zinazowakabili waendesha bodaboda jijini Arusha kwa kuchangia shilingi milioni 2 kwa ajili ya kulipia kodi ya ofisi ya chama chao hadi kuanzia Februari hadi Disemba 2025.
Hatua hiyo imekuja baada ya kukutana na viongozi wa waendesha bodaboda na kujadiliana changamoto wanazopitia katika shughuli zao za kila siku. Gambo amesema changamoto ya kodi ya ofisi ilihitaji ufumbuzi wa haraka ili kuepuka kero kwa waendesha bodaboda.
Kupata taarifa na matukio ya kimkoa kuhusu Uchaguzi Serikali za Mitaa ingia hapa: LGE2024 - Special Thread: Orodha ya Mijadala ya Mikoa yote Tanzania Bara inayoshiriki katika Uchaguzi wa Serikali za Mitaa 2024
Mbali na mchango huo wa fedha, Gambo pia amekabidhi televisheni ya inchi 32 kwa ofisi ya chama cha bodaboda ili waendesha bodaboda waweze kufuatilia matukio mbalimbali yanayoendelea duniani. Vilevile, ametoa viti vya ofisini kwa ajili ya kuboresha mazingira yao ya kazi.