TUKANA UONE
JF-Expert Member
- Jan 3, 2018
- 2,345
- 6,970
KUHUSU GAMONDI
Nilidhani baada ya mechi huyu mtu hakupaswa hata kukanyaga Avic town,lakini Kwa mshangao nimeshangaa hadi muda huu yupo tu anadunda kama kitenesi!
Viongozi wa Yanga mnatukosea sana mashabiki na wanachama hadi muda huu!,niwaulize nyie viongozi,Je,huyo Gamondi ni mwanahisa hapo Jangwani kiasi kwamba hafukuziki?
Sitarajii na sitegemei kuona Gamondi akimaliza saa 24 zijazo,mkiendelea kumng'ang'ania huyo kichwa kigumu nitavunja kadi yangu ya Uanachama na nitachoma jezi zote za Yanga na sitonunua tena jezi na sitalipia kadi tena!
KUHUSU UWANJA WA CHAMAZI
Binafsi huu uwanja hauna tatizo,nawashangaa sana mashabiki hoya hoya ambao Wana viherehere na vidomodomo ya kwamba eti, timu iachane na uwanja wa Azam kwasababu ya Hujuma!
Hujuma zipi?yaani timu ifanye vibaya tuseme Hujuma?,hizo hujuma zilikuwa wapi wakati tunacheza na Vital O?,Hizo hujuma hazikuwepo wakati tunashinda mechi nyingine?
Ndiyo yawezekana Kuna wafanyakazi wa Uwanja (Stewards) ambao si waaminifu Kwa kutengeneza mazingira ya kuidhoofisha Yanga na kuwafanya wapinzani wetu watukejeli!
Hebu nielezeni,timu ikiacha kutumia Uwanja wa Azam (CHAMAZI) watatumia uwanja gani?,Kwani hatuelewi uwanja wa Taifa upo kwenye ukarabati?,kwani hatujui uwanja wa New Amani Complex nao wameufunga Kwa muda usiojulikana pia upo kwenye ukarabati?,hebu niambieni tutaenda kuchezea wapi?
Wapuuzi wengine nimewasikia wanasema eti timu ikacheze uwanja wa Mwanza (CCM kirumba) kama uwanja wake wa nyumbani!,hivi huo uwanja mnaujua lakini au mnauonaga kwenye TV mnadhani ni kiwanja Bora? Au mnataka timu iende uwanja wa KMC ambalo Makolo tayari wamesimika mizimu Yao?
Binafsi uwanja kwangu hauna tatizo!
KUHUSU MASHABIKI
Kama Kuna mashabiki nchi hii ambao naweza kusema ni wapuuzi,bila shaka watakuwa mashabiki wa Yanga!
Jana Kuna mwingine kidogo nimpigie hadi niue kwasababu ya ujinga wake,Mimi nipo sehemu tunazungumzia mpira,yeye na kiherehere Chake akataka kuniletea Ujuaji!
Hivi unawezaje ukiwa kama shabiki wa Yanga huna Jezi ya Timu yako?,Hivi unawezaje ukiwa kama shabiki wa timu yako uwanjani uendi?
Timu imechukua Ubingwa mara 3 mfululizo lakini mashabiki wa kuchajaza tu pale CHAMAZI niwa kuwatafuta Kwa tochi,Je mnataka Yanga ifanye kitu gani ili muweze kwenda uwanjani?
Binafsi nawapongeza mashabiki wa Makolo,japokuwa Makolo wanefanya vibaya miaka 3 lakini wameendelea kujaza uwanja wowote pale timu Yao inapo cheza!,Hebu fikiria wangekuwa wanafanya vizuri hali ingekuwaje!
Huku kwetu unakuta shabiki yupo kibanda umiza huko anapiga kelele tu!
Ni lini mtabadilika nyie?
Yangu ni hayo tu jioni ya leo?
N.B - Matusi kwangu ni utuli,tukana sana ili nami niendelee kunukia sana!
Nilidhani baada ya mechi huyu mtu hakupaswa hata kukanyaga Avic town,lakini Kwa mshangao nimeshangaa hadi muda huu yupo tu anadunda kama kitenesi!
Viongozi wa Yanga mnatukosea sana mashabiki na wanachama hadi muda huu!,niwaulize nyie viongozi,Je,huyo Gamondi ni mwanahisa hapo Jangwani kiasi kwamba hafukuziki?
Sitarajii na sitegemei kuona Gamondi akimaliza saa 24 zijazo,mkiendelea kumng'ang'ania huyo kichwa kigumu nitavunja kadi yangu ya Uanachama na nitachoma jezi zote za Yanga na sitonunua tena jezi na sitalipia kadi tena!
KUHUSU UWANJA WA CHAMAZI
Binafsi huu uwanja hauna tatizo,nawashangaa sana mashabiki hoya hoya ambao Wana viherehere na vidomodomo ya kwamba eti, timu iachane na uwanja wa Azam kwasababu ya Hujuma!
Hujuma zipi?yaani timu ifanye vibaya tuseme Hujuma?,hizo hujuma zilikuwa wapi wakati tunacheza na Vital O?,Hizo hujuma hazikuwepo wakati tunashinda mechi nyingine?
Ndiyo yawezekana Kuna wafanyakazi wa Uwanja (Stewards) ambao si waaminifu Kwa kutengeneza mazingira ya kuidhoofisha Yanga na kuwafanya wapinzani wetu watukejeli!
Hebu nielezeni,timu ikiacha kutumia Uwanja wa Azam (CHAMAZI) watatumia uwanja gani?,Kwani hatuelewi uwanja wa Taifa upo kwenye ukarabati?,kwani hatujui uwanja wa New Amani Complex nao wameufunga Kwa muda usiojulikana pia upo kwenye ukarabati?,hebu niambieni tutaenda kuchezea wapi?
Wapuuzi wengine nimewasikia wanasema eti timu ikacheze uwanja wa Mwanza (CCM kirumba) kama uwanja wake wa nyumbani!,hivi huo uwanja mnaujua lakini au mnauonaga kwenye TV mnadhani ni kiwanja Bora? Au mnataka timu iende uwanja wa KMC ambalo Makolo tayari wamesimika mizimu Yao?
Binafsi uwanja kwangu hauna tatizo!
KUHUSU MASHABIKI
Kama Kuna mashabiki nchi hii ambao naweza kusema ni wapuuzi,bila shaka watakuwa mashabiki wa Yanga!
Jana Kuna mwingine kidogo nimpigie hadi niue kwasababu ya ujinga wake,Mimi nipo sehemu tunazungumzia mpira,yeye na kiherehere Chake akataka kuniletea Ujuaji!
Hivi unawezaje ukiwa kama shabiki wa Yanga huna Jezi ya Timu yako?,Hivi unawezaje ukiwa kama shabiki wa timu yako uwanjani uendi?
Timu imechukua Ubingwa mara 3 mfululizo lakini mashabiki wa kuchajaza tu pale CHAMAZI niwa kuwatafuta Kwa tochi,Je mnataka Yanga ifanye kitu gani ili muweze kwenda uwanjani?
Binafsi nawapongeza mashabiki wa Makolo,japokuwa Makolo wanefanya vibaya miaka 3 lakini wameendelea kujaza uwanja wowote pale timu Yao inapo cheza!,Hebu fikiria wangekuwa wanafanya vizuri hali ingekuwaje!
Huku kwetu unakuta shabiki yupo kibanda umiza huko anapiga kelele tu!
Ni lini mtabadilika nyie?
Yangu ni hayo tu jioni ya leo?
N.B - Matusi kwangu ni utuli,tukana sana ili nami niendelee kunukia sana!