Wadau hii gari nimekuwa nikiielewa sana kuanzia muonekano, space kwa ndani na uwezo wa kubeba watu wengi (7 seats). Naomba mwenye uzoefu au anayeielewa vizuri anidadavulie kuanzia unywaji mafuta mpaka ubora na upatikanaji wa spea. Nawasilisha
Bila shaka unataka lile Gaia la kumvua mtu ili tu kutimiza hitaji la moyo wako! maana sijawahi kuona gari aina ya Gaia lenye namba za usajili za C au D! Machache niliyoyaona ni A na B tu! Gari za Toyota zote spea siyo tatizo. Mafuta kama rav 4 old model kama sikosei. cc 1900's.
Mkuu Uko Mkoa gani? Hizi Gaia ni za kitambo sana...kama Issue ni Seven Seater Nunua hata Toyota Isis Platana. Gaia sikushauri... labda kama unaishi Mbeya maana huko ziko nyingi sana[emoji23][emoji23][emoji23]