MFUNGWA mmoja amefariki na wengine saba kujeruhiwa baada ya gari la magereza kupinduka huko Kathageri karibu na Daraja la Thuci, Wilaya ya Embu, leo.
Aliongeza kwamba wafungwa hao walikuwa wakisafirishwa kutoka Gereza la Embu kwenda Mahakama za Meru ambapo pia dereva alijeruhiwa vibaya. na kupelekwa kwa matibabu katika Embu Level Five Teaching and Referral Hospital.
Shuhuda, Maureen Mwende, alisema ajali hiyo ilitokea asubuhi wakati wa mvua.
“Nafikiri ni kutokana na utelezi gari likashindikana kudhibitiwa,” alisema mwanamke huyo.