Gari laniumiza mgongo

Habari zenu wakuu
Mimi nina tatizo la kuumwa mgongo hasa maeneo ya karibu na kiunoni na tatizo hili huwa linanikumba kila baada ya kuendesha gari
So naombeni msaada wenu wa kuweza kulitatua hili tatizo

Ni gari la aina gani? Kuna siku nilisikia mada Clouds TV daktari akizungumzia matatizo kama yako. Akasema huwakumba zaidi wanaoendesha magari madogo kutokana na nature ya viti vyake. Aidha akasema hata maofisini kuna viti vile vya kibosi ambavyo havina angle Nyuzi 90. Kifupi angalia kiti cha gari yako kikoje kwa ushauri wa Daktari nilimsikia, sehemu unayosema inauma uti wa mgongo umehang haijashikiliwa na mbavu hivyo uko delicate. Cha muhimu hakikisha mgongo unakuwa kwenye nyuzi 90 unapoendesha gari. Hivyo naona fanya maarifa labda kuweka vimito vidogo au kuwa conscious mgongo wako unyooke unapoendesha gari. Halafu alishauri kujitahidi kunyoosha mgogmngo kwa kusimama kwani wenye magari na wanaofanya kazi kwa kukaa muda mrefu wana risk ya kuumwa mgogngo kwa sababu ya huo mkao ambao sio rafiki kwa uti wamgongo sehemu ya nyonga.
Lakini kupata ushauri wa uhakikka muone Daktari hususn wa mifupa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…