Gas kg 15 kutoka 45,000 hadi 55,000 hadi 70,000

Gas kg 15 kutoka 45,000 hadi 55,000 hadi 70,000

Mpangamji

JF-Expert Member
Joined
May 12, 2010
Posts
540
Reaction score
140
Leo nimeshitushwa na simu ya mtu niliyemtuma kwenda kununua gas kg 15 nikiwa nimempatia Tshs 55,000 lakini aliniambia kuwa gas ni Tshs 70,000 nilimwambia aache porojo, ndipo aliposisitiza kuwa bei imepanda, niliamua kuulizia sehemu nyingine ili nijue, nikaambia bei ni 70,000 kwa mtungi wa kg 15. tunakwenda wapi jamani, afadhali tuingie barabarani hawa watu tuwatoe madarakani, kwa mshahara wa 290,000 hii nini, chumba na sebure 150,000 kwa mwezi, gas 70,000 maji Tshs 300/dumu X dumu 5 X siku 30 = 45,000 daladala Tshs 700/siku x siku 20 = 14,000 mkate Tshs 500 x siku 30 =15,000 (294,000)
Mchele, unga, sukari, mafuta, umeme, mafuta ya kujipaka mwilini, kunyoa nywele, salon kwa wadada. tunakwenda wapi?????
 
Umeme nao ume2. Jamani mimi nimeichoka CCM, jamani siitakiiiii e!!!!!!!!!!!!!. Mbona hawasikiiiiii.
 
Mi naona tunachelewa kuingia barabarani tufanye haraka jamani kabla mambo hayajawa mabaya zaidi maana hawa jamaa wanarudisha mihela waliyotumia kwenye kampeni ya kifisadi mabango, Tshirt, Khanga na kofia nchi nzima.
 
Ndiyo maana mimi niko tayari kwa maandamano hata yakitangazwa jioni hii....pesa haina thamani tena ukiwa 10,000 usipo angalia kwa siku haitoshi sijui wanaolipwa 75,000/mwezi wanaishije....halafu tunaambiwa uchumi unapanda sijasomea uchumi lakini kwa hili..
 
Leo nimeshitushwa na simu ya mtu niliyemtuma kwenda kununua gas kg 15 nikiwa nimempatia Tshs 55,000 lakini aliniambia kuwa gas ni Tshs 70,000 nilimwambia aache porojo, ndipo aliposisitiza kuwa bei imepanda, niliamua kuulizia sehemu nyingine ili nijue, nikaambia bei ni 70,000 kwa mtungi wa kg 15. tunakwenda wapi jamani, afadhali tuingie barabarani hawa watu tuwatoe madarakani, kwa mshahara wa 290,000 hii nini, chumba na sebure 150,000 kwa mwezi, gas 70,000 maji Tshs 300/dumu X dumu 5 X siku 30 = 45,000 daladala Tshs 700/siku x siku 20 = 14,000 mkate Tshs 500 x siku 30 =15,000 (294,000)
Mchele, unga, sukari, mafuta, umeme, mafuta ya kujipaka mwilini, kunyoa nywele, salon kwa wadada. tunakwenda wapi?????

Kweli haya ni maisha boro kwa mtanzania,tutafika .... sijui.
 
:Cry:Jamani gas juu mno umeme juu mi sitafika kwa njia hii jamani mbona serikali haisikiiiiiiiiiiiiiiiiiiiii??????

mambo gani ya kumpigia mbuzi gitaa??
 
Duh ,ntaendelea kuichagua ccm daima

Acha utani katika mijadala ya msingi. Na kama kweli unamaanisha utakuwa ni sehemu ya mafisadi wanaotafutwa. Ipo siku utakamatwa tu. Kama Sadamm Hussein alikamatwa, wewe hautashindikana.
 
LPG storage nchini ni ndogo na matumizi ya LPG yamekuwa kwa kasi kubwa. Supply yake inahitaji forecast ya kueleweka ingawa inaonekana kama matumizi yamepanda kupita makadirio.Hata hivyo upatikanaji wa meli zinazoleta LPG nchini nao ni tatizo nahivyo kuleta usumbufu wa mara kwa mara kwa kukosekana gas.
Nafikri TIPER wangeweza kuwekeza katika stogare ya LPG gas ili kuondoa tatizo hili in future. Kuyaachia makampuni ya mafuta tu tena mengi ya kigeni, tutatengeneza tatizo kubwa la supply za gas.Bei ya gas ni lazima iwe reasonable maana hatuna tena nishati mbadala. I believe serikali, kupitia EWURA inaliangalia tatizo hilo kwa mapana zaidi
 
Mimi na CCM Daima mileleeee wacha tu maana nakikubali sana chama hiki akifanyi makosa kabisa ukichagua sasa unarudisha gharama za uchaguzi wakati wa uchaguzi tunawapa khanga mmesahau na pia nakikubali Ureeee Ifike laki au Kilo kwa mtungi ndo mwake mwake na mshara usipande. Hatutaki yaliotokea TUNISIA uREEE ccm OYEEEEEEEEEEEEEEEE
 
LPG storage nchini ni ndogo na matumizi ya LPG yamekuwa kwa kasi kubwa. Supply yake inahitaji forecast ya kueleweka ingawa inaonekana kama matumizi yamepanda kupita makadirio.Hata hivyo upatikanaji wa meli zinazoleta LPG nchini nao ni tatizo nahivyo kuleta usumbufu wa mara kwa mara kwa kukosekana gas.
Nafikri TIPER wangeweza kuwekeza katika stogare ya LPG gas ili kuondoa tatizo hili in future. Kuyaachia makampuni ya mafuta tu tena mengi ya kigeni, tutatengeneza tatizo kubwa la supply za gas.Bei ya gas ni lazima iwe reasonable maana hatuna tena nishati mbadala. I believe serikali, kupitia EWURA inaliangalia tatizo hilo kwa mapana zaidi

Napenda sana watu wanaojibu hoja kwa kuangalia hali halisi yaani facts. Nafikiri hapa ndio tatizo lilipo na kuna haja ya kutafuta suluhisho la haraka sana. Daima unapopandisha gharama za nishati tena kwa ghafla uchumi huyumba sana na kusababisha mfumuko wa bei kirahisi sana. Pengine hawa viongozi wetu hawajui tatizo hili manake wao hawanunui chochote.

Wao ikifika sa saba chakula kipo mezani, mtungi unauzwa bei gani, sijui mchele kilo ni bei gani, nyama inauzwaje, bei ya nyanya waho hivo haviwahusu hata kidogo...!

Kikwwete anapoelekea ni pabaya manake kwa jinsi siku zinavozidi kwenda inaonekana kama nakua anajitenga na matatizo ya watu au anayafumbia macho...!

Wakati taifa linalalamika kupata umeme halafu kiongozi unaonekana unaenda kuwalika mabalozi ikulu kwa ajili ya chakula cha mchana, ufujaji wa matumizi upo wazi wazi, mawaziri kutembelea magari ya mamilioni ya fedha, hii ndio inafanya wananchi wapoteze imani na kuona kwamba Serikali inawatenga na kutowajali...!
 
Haya yote yasingeniumiza sana kama ningekuwa nimefanya bad choice wakati wa uchaguzi.............mimi nililiona kabisa kuwa nchi hii inaelekea kubaya nikaamua kuto wachagua CCM lakini wakachakachua.......................inaniuma sana kwasababu maamuzi yangu yalichezewa kwa manufaa yao na mateso yangu na watoto wangu. Wbunge mna ona haya mambo? mnasikiliza matatizo ya watu wenu? Msimamo wenu uko wapi juu ya hali hii?

Chonde chonde miaka mitano kwa mwendo huu kweli hapatoshi ukichukulia leo ni mwezi wa kwanza wa mwaka wa kwanza katika mitano.......
 
Yaani kwa kweli nilichanganyikiwa sana juzi mtungi wa gesi ambao nilizoea kuununua kwa Tshs 42,000 nikaambiwa shs 70,000 yaani kidogo nipigane maana ilikuwa ngumu kunielewesha aisee........... hivi kusema ukweli hakuna coordination ??......hakuna uwezekano wa serikali kusubsdize some of the important items kwa maskahi ya nchi??.... Umeme wa siku hizi haushikiki, si kwa maana ya mgao pekee bali hata bei yake kwa mtanzania kupikia isitoshe ni watanzania wangapi wenye kuaccess nishati hii?

Najiona kabisa kurudia nisghati yangu ya mkaa ambayo niliapa kuiacha kwa nia thabit kabsa ya kuyalinda, kuyatunza na kuyahifadhi mazingira ya nchi yangu Tanzania. Ni wazi upandaji wa bei ya gesi unakinzana na dhana nzima ya kuzuia utumiaji mkubwa wa Mkaa kwa nia ya kutunza mazingira........ I wish serikali ingeliangalia hilo upya ili kujaribu kuilinda heshima iliyojitwalia katika vita dhidi ya ukataji wa miti kwa minajili ya kutengeneza mkaa. Madhara ya utuliaji mkaa ni makubwa na mengi sana zaidi ya madhara ya kushusha bei ya gesi.
 
Ni ugumu wetu wa kuelewa tulipokuwa tukiambiwa kuwa hawa jamaa hawana nia ya dhati kumkomboa mtanzania, tulidhani ni uongo!!! Lakini tatizo kubwa ni sisi wenyewe. Nina uhakika kabisa kama hawa jamaa wasingekuta kura hata moja lwenye yale masanduku ya kura mwaka jana hata uchakachuzi ungeshindikana..... Lakini kwa kuwa baadhi yetu tulijifanya tunajua zaidi, basi kuna miaka mitano mingine ya maisha magumu sana, hii ya gesi na umeme ni hatua ya mwanzo tu, tutafunga mikanda mpaka viuno vikatike..... Na tusipokuwa na maamuzi ya busara 2015.......... :Cry: :Cry:
 
Tatizo ni kwamba kuna miaka minne mbele...by the time huyu mkwere anatuachia nchi itakua hatari! Naona 'signals' ama hazitoshi au mkwere anazipotezea!..yaani hakuwa chagua langu toka 2005! Bahati mbaya walimchakachua Salim...very disappointing!
 
Mod,tafadhali peleka hii mada kwenye jukwaa la siasa,tafadhali sana!!
 
Wadau,

Mimi sikuamini nilimtuma mtu aninulie Gesi last Friday,akarudi akaniambia gesi ni shs 75,000 Kwa mtungi wa kilo 15. sikuamini ikanibidi niende mwenyewe, kukuta bei ndiyo hiyo hiyo jamani Tz,inaenda wapi jamani,mishahara iko pale pale hali ya maisha iko juu sana! solution is needed immediately!
 
This is too much jamani......Najuta kuzaliwa Tanzania.
 
Back
Top Bottom