Gazeti la Mwananchi waache upotoshaji

rodrick alexander

JF-Expert Member
Joined
Feb 12, 2012
Posts
16,784
Reaction score
23,312
Kwa yeyote aliyesoma gazeti la Mwananchi la desemba 30, 2016 upande wa michezo atagundua kuna upotoshaji mkubwa uliofanywa na mwandishi wa habari za michezo wa mwananchi kwenye habari "Simba yafunga vyema hesabu 2016".

Katika habari hiyo beki wa hesabu method Mwanjali ametajwa kama mshambuliaji pia wameandika kipa wa Ruvu Shooting alionyeshwa kadi nyekundu kitu ambacho hakikuwepo.

Kuna watu ambao hawaangalii tv ama hawana uwezo au wanakosa muda hivyo wanategemea vyombo kama magazeti kupata habari za matukio yanayoendelea lakini ni aibu kubwa kwa chombo cha habari kama mwananchi kufanya makosa kama hayo.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…