LGE2024 Geita: Katibu wa CCM mkoa ajihakikishia ushindi kwenye Wilaya ya Nyang'hwale

LGE2024 Geita: Katibu wa CCM mkoa ajihakikishia ushindi kwenye Wilaya ya Nyang'hwale

Uchaguzi wa Serikali za Mitaa 2024

Mindyou

JF-Expert Member
Joined
Sep 2, 2024
Posts
1,869
Reaction score
4,877
Chama cha Mapinduzi (CCM) mkoani Geita kimeonyesha kujiamini kushinda Vijiji na Vitongoji vyote Wilayani Nyang’hwale baada ya Vijiji 39 kukosa wapinzani, huku vyama vya Upinzani vikifanikiwa kusimamisha Wagombea katika vijiji 23 pekee.

Kwa upande wa vitongoji, CCM imepita bila kupingwa katika vitongoji 220 kati ya 270, huku wapinzani wakijipatia nafasi kwenye vitongoji 50.

Kauli hiyo ilitolewa na Katibu wa CCM Mkoa wa Geita, Alexandrina Katabi, wakati wa kumnadi Mgombea wa nafasi ya Uenyekiti wa kijiji pamoja na wajumbe wake katika Wilaya ya Nyang’hwale.

 
Back
Top Bottom