Roving Journalist
JF Roving Journalist
- Apr 18, 2017
- 3,984
- 13,760
WanaJF,
Mada hii itakuwa na 'Updates' za Matukio kuelekea Uchaguzi Mkuu wa Urais, Ubunge na Udiwani 2025 kama yanavyotujia kutoka kwenu kutoka mkoa wa Geita. Ukiwa na taarifa yoyote ambayo ni ya eneo hili tafadhali usisite kuweka.Mkoa wa Geita upo Kanda ya Ziwa katika Tanzania na ni maarufu kwa shughuli za kilimo na ufugaji, pamoja na madini, hasa dhahabu. Mkoa huu una historia ya utajiri wa madini, hususan kupitia mgodi maarufu wa Geita Gold Mining.
Idadi ya Watu
Matokeo ya Sensa ya Watu na Makazi ya Mwaka 2022 yanaonesha kuwa idadi ya watu katika Mkoa wa Geita ni watu 2,977,608; wanaume 1,463,764 na wanawake 1,513,844.Mkoa huu una Halmashauri sita (6) na majimbo saba (7) ya uchaguzi ambapo Jimbo la Busanda linaongoza kwa kuwa na watu wengi (671,761) likifuatiwa na Jimbo la Chato (watu 584,963). Jimbo lenye idadi ndogo ya watu ni Jimbo la Nyang'hwale ambalo lina watu 225,803, huku ukiwa na wilaya 6.
Idadi ya Majimbo ya Uchaguzi
Mkoa wa Geita una jumla ya majimbo 7 ya uchaguzi:- Jimbo la Geita Vijijini
- Jimbo la Busanda
- Jimbo la Geita Mjini
- Jimbo la Nyang'hwale
- Jimbo la Mbogwe
- Jimbo la Bukombe
- Jimbo la Chato
Mkoa wa Geita ulishiriki kikamilifu katika uchaguzi wa Rais, Wabunge, na Madiwani ambapo Chama Cha Mapinduzi (CCM) kiliibuka na ushindi mkubwa.
Mgombea wa urais kwa tiketi ya CCM, Hayati John Pombe Magufuli, alipata kura nyingi zaidi kulinganisha na wapinzani wake.
Katika uchaguzi wa Ubunge, wagombea walishinda kwa kishindo kwa kura nyingi, huku wengine wakipita bila kupingwa na CCM kujinyakulia majimbo yote.
Uchaguzi wa Madiwani, (CCM) walipata ushindi mkubwa kwenye nafasi za madiwani ikifanikiwa kushinda kwa kishindo. Hii ilitokana na upinzani kukumbwa na changamoto nyingi, zikiwemo wagombea wao kuenguliwa kutokana na matatizo ya kisheria au kutokidhi vigezo
Kulikuwa na malalamiko kutoka kwa vyama vya upinzani kama vile CHADEMA na ACT-Wazalendo kuhusu kutokuwepo kwa uwazi na haki katika mchakato wa uchaguzi.
Updates
January
- Pre GE2025 - Stephen Wasira Amjibu John Heche Kuhusu Umri Wake Mkubwa. Asema Gari ni Injini Na Siyo Bodi
- Pre GE2025 - Wassira: Maridhiano ni lazima, nchi nyingi za Africa zilipitia Mapinduzi ya Kijeshi Lakini Tanzania tumekuwa Kisiwa Cha Amani!
- Pre GE2025 - Wassira: Wanaosema CCm imekaa sana walikuwa wapi wakati tunadai uhuru
- Pre GE2025 - Wassira: CCM ni chama kikubwa hakiwezi kuamrishwa na 'Kibaka'
- Pre GE2025 - Wasira: Mabeberu na Vibaraka wao wanataka kuleta Ushoga
- Pre GE2025 - Geita: Viongozi wa dini Chato wachangisha Tsh. Mil 1.4 kwaajili ya Rais Samia kuchukua fomu ya kugombe Urais
- Pre GE2025 - Mbunge Kassu: Sitovumilia tuhuma za uongo dhidi yangu kuhusu matumizi ya mfuko wa jimbo
- Pre GE2025 - Mwenyekiti NCCR Mageuzi: Doto Biteko apite bila kupingwa nafasi ya ubunge ndani ya CCM, kwenye udiwani tutapambana
- Pre GE2025 - Jakaya Kikwete: Niwaambie kuwa mambo mazuri ya Bukombe yasingetokea kama msingemchagua Dkt. Biteko
- Pre GE2025 - Halmashauri ya Wilaya ya Geita imetoa mkopo wa milioni 689 kwa vikundi 39 vinavyoundwa na wanawake, vijana, na watu wenye ulemavu
- Pre GE2025 - Evaristi Gerevas: Vijana msiishie kuwa wapambe na wabeba mikoba ya wagombea, gombeeni ubunge na udiwani
- Pre GE2025 - Wazee maarufu Geita wakabidhi fimbo na kuku kwa mwenyekiti wa UVCCM mkoa
- Pre GE2025 - Samia Teachers Mobile Clinic inayoratibiwa na CWT inatarajiwa kusikiliza changamoto mbalimbali za walimu Geita
- Pre GE2025 - Mwenyekiti UVCCM Geita: Wapinzani wanatetemeka. Tunaenda kwenye uchaguzi, nyie jiandaeni. Asiwatishe mtu!
- Pre GE2025 - Dtk. Biteko awataka walimu wasijione duni waeleze shida zao, ataka pia wasikilizwe wakiwasilisha shida hizo
- Pre GE2025 - Geita: CCM yawanunulia wanafunzi TV kwa ajili ya kufuatilia yanayofanywa na Rais Samia ili yawasaidie katika masomo yao
- Pre GE2025 - Mwenyekiti UVCCM, Geita: Boda boda Nyang'hwale msijihusishe na shughuli za kiuhalifu
- Pre GE2025 - Medard Kalemani: CCM Chato tunahita utulivu na umoja kwenye kipindi hiki cha kuelekea Uchaguzi
- Pre GE2025 - Shule mpya 71 zajengwa Geita miaka minne ya Rais Samia
- Pre GE2025 - Luhaga Mpina: Unakuta waziri mwizi, katibu mkuu mwizi ukimbana kwenye wizi anasema wewe huipendi CCM
- Pre GE2025 - Luhaga Mpina: Sitakaa kimya dhidi ya Ufisadi na Matumizi Mabaya ya Fedha za Umma
- Pre GE2025 - UVCCM Geita: Hakuna atakayezuia Uchaguzi Mkuu Oktoba 2025
- Pre GE2025 - Mradi wa uboreshaji wa miji Tanzania (TACTIC) Geita Mjini, Mbunge alalama ubabaishaji wa mkandarasi, Tuliahidi mradi kukamilika kabla ya uchaguzi
- Pre GE2025 - Mwenyekiti UVCCM Geita: Hatufurahishwi kuona vijana wetu wanaondoka duniani kwa kutekwa! Tunalaani na kukemea matendo haya!
- Pre GE2025 - Mbunge Musukuma atumia zaidi ya Tsh bilioni 1 kununua ambulance, gari la Polisi na kujenga kituo cha Polisi Geita Vijijini
- Pre GE2025 - Mbunge Kanyasu aeleza Mafanikio ya uongozi wake katika Jimbo la Geita
- Pre GE2025 - UVCCM Geita yamtaka Mbunge Kanyasu aombe radhi vijana kwa kauli zake
ZINGATIA: Mikoa yote ina mada yake ya 'Update' ili kuweka wepesi katika ufuatiliaji.