Cute Wife
JF-Expert Member
- Nov 17, 2023
- 1,906
- 5,000
Wakuu,
Mambo ni moto kila sehemu, ni mwendo wa kuengua tu na kubakisha wa kupita bila kutoa jasho.
=====
Viongozi na Wanachama wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) katika Jimbo la Geita Mjini mkoani Geita, wamelalamikia kuenguliwa kwa majina ya wagombea wao wa nafasi za Uenyekiti na Ujumbe katika Uchaguzi wa Viongozi wa Serikali za mitaa unaotarajiwa kufanyika Novemba 27, mwaka huu.
Akizungumza mara baada ya kufika kwenye ofisi za Serikali ya mtaa wa NMC, Kata ya Kasamwa kwa ajili ya kufikisha malalamiko yao, Mwenyekiti wa CHADEMA Jimbo la Geita Mjini Pasiquna Lucas amesema miongoni mwa sababu zilizopelekea kuenguliwa kwa wagombea wao ni makosa katika ujazaji wa fomu.
Hata hivyo, alilalamika kuwa baadhi ya wagombea wa vyama vingine wamepitishwa licha ya kuwa na mapungufu mengi.
Mambo ni moto kila sehemu, ni mwendo wa kuengua tu na kubakisha wa kupita bila kutoa jasho.
=====
Viongozi na Wanachama wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) katika Jimbo la Geita Mjini mkoani Geita, wamelalamikia kuenguliwa kwa majina ya wagombea wao wa nafasi za Uenyekiti na Ujumbe katika Uchaguzi wa Viongozi wa Serikali za mitaa unaotarajiwa kufanyika Novemba 27, mwaka huu.
Akizungumza mara baada ya kufika kwenye ofisi za Serikali ya mtaa wa NMC, Kata ya Kasamwa kwa ajili ya kufikisha malalamiko yao, Mwenyekiti wa CHADEMA Jimbo la Geita Mjini Pasiquna Lucas amesema miongoni mwa sababu zilizopelekea kuenguliwa kwa wagombea wao ni makosa katika ujazaji wa fomu.
Hata hivyo, alilalamika kuwa baadhi ya wagombea wa vyama vingine wamepitishwa licha ya kuwa na mapungufu mengi.
