Geita: Mwanamke auawa kwa kuchomwa na kitu chenye ncha kali na mume wake

Geita: Mwanamke auawa kwa kuchomwa na kitu chenye ncha kali na mume wake

Mkalukungone mwamba

JF-Expert Member
Joined
Aug 29, 2022
Posts
862
Reaction score
1,755
Mapenzi na migogoro ya ndoa imeendelea kuleta shida na hata kutoa roho za watu kila kukicha jamaani!
==================

Mwanamke mmoja mkazi wa kata ya Ludete wilayani Geita, Adventina Nicolaus (37) amefariki baada ya kuchomwa na kitu chenye ncha kali na mume wake, huku tukio hilo likihusishwa na mgogoro wa kifamilia.

Inaelezwa kuwa tukio hili limetokea usiku wa kuamkia Januari 7, 2025.

Kwa mujibu wa mashuhuda na ndugu wa marehemu, mtuhumiwa alitekeleza kitendo hicho na baadaye kuwapigia simu ndugu wa Adventina kuomba msamaha kwa kile alichokitenda.

Soma Pia: NJOMBE: Amkata Mume wake sehemu za Siri ya kubaini anachepuka nje

Yasinta Nicolaus, mdogo wa marehemu na Elizabeth Nicolaus, pia mdogo wa marehemu wameeleza kushtushwa na msiba huo wa ghafla.

Baadhi ya majirani wa familia hiyo wameonyesha masikitiko yao makubwa kuhusu tukio hilo na kulaani vikali kitendo cha kuua, wakieleza kuwa, hata kama kunatokea kutokuelewana kati ya wanandoa, suluhu inapaswa kutafutwa bila kutumia nguvu au kujichukulia sheria mkononi.

Adventina Nicolaus ameacha mtoto mmoja wa kike mwenye umri wa miaka miwili. Jamii na mamlaka zinahimizwa kushirikiana kuhakikisha haki inapatikana na matukio ya aina hii

 
Tunaendelea na hatutaacha kusisitiza kama unaakili timamu, KATAA NDOA.Ona sasa mwamba anaenda kunyea debe nyuma ya nondo.

#kataa ndoa,ndoa ni utapeli!!!
 
Mapenzi na migogoro ya ndoa imeendelea kuleta shida na hata kutoa roho za watu kila kukicha jamaani!
==================

Mwanamke mmoja mkazi wa kata ya Ludete wilayani Geita, Adventina Nicolaus (37) amefariki baada ya kuchomwa na kitu chenye ncha kali na mume wake, huku tukio hilo likihusishwa na mgogoro wa kifamilia.

Inaelezwa kuwa tukio hili limetokea usiku wa kuamkia Januari 7, 2025.

Kwa mujibu wa mashuhuda na ndugu wa marehemu, mtuhumiwa alitekeleza kitendo hicho na baadaye kuwapigia simu ndugu wa Adventina kuomba msamaha kwa kile alichokitenda.

Soma Pia: NJOMBE: Amkata Mume wake sehemu za Siri ya kubaini anachepuka nje

Yasinta Nicolaus, mdogo wa marehemu na Elizabeth Nicolaus, pia mdogo wa marehemu wameeleza kushtushwa na msiba huo wa ghafla.

Baadhi ya majirani wa familia hiyo wameonyesha masikitiko yao makubwa kuhusu tukio hilo na kulaani vikali kitendo cha kuua, wakieleza kuwa, hata kama kunatokea kutokuelewana kati ya wanandoa, suluhu inapaswa kutafutwa bila kutumia nguvu au kujichukulia sheria mkononi.

Adventina Nicolaus ameacha mtoto mmoja wa kike mwenye umri wa miaka miwili. Jamii na mamlaka zinahimizwa kushirikiana kuhakikisha haki inapatikana na matukio ya aina hii


Mbona huu mkoa ghafla umekuwa na watu wakatili kiasi hiki? Nini kimetokea na kubadilisha mtazamo wao kifikra? Njombe shida za mauaji ni kuwa matajiri.
Katavi sijui wanaua ili iweje...ila Geita, comes as shock
 
Geita wamefungulia pazia la 2025! Hawapoi hawa jamaa. Soon Njombe na Tabora watajibu kwa mapigo makali sana! Stay tuned.
 
Mbona huu mkoa ghafla umekuwa na watu wakatili kiasi hiki? Nini kimetokea na kubadilisha mtazamo wao kifikra? Njombe shida za mauaji ni kuwa matajiri.
Katavi sijui wanaua ili iweje...ila Geita, comes as shock
Geita toka zamani kuna issue za ujambazi na mauaji ya kafara sababu ya madini... ila hizi issue za kuuana kwa wivu wa mapenzi sio kiviiile sana
 
Back
Top Bottom