George Arnautoglu mhisani wa Waafrika wa Tanzania

George Arnautoglu mhisani wa Waafrika wa Tanzania

Mohamed Said

JF-Expert Member
Joined
Nov 2, 2008
Posts
21,967
Reaction score
32,074
GEORGE ARNAUTOGLU

Ukumbi wa Arnautoglu ulikuwa ukumbi maarufu sana Dar es Salaam katika miaka ya 1950 na shughuli nyingi za kijamii na za kiasi zimefanyika pale.

Jambo la kusikitisha sana ni kuwa hakuna mtu amjuaye mjenzi wa jengo hilo wala hakuna picha yake popote katika hilo jengo.

Wala historia ya George Arnautoglu haijulikani sana na wanoijua watakuambia kuwa alikuwa Giriki tajiri mwenye mashamba ya mkonge.

Hapo chini ni picha ya George Arnautoglu niliyoletewa na Hafidh Kido mwandishi wa Jamvi la Habari kutoka gazeti la Mambo Leo la mwaka wa 1943.

Nimekutana na George Arnautoglu wakati natafiti historia ya TANU siku nilipokwenda kuzungumza na Ali Mwinyi Tambwe aliyekuwa Secretary wa Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika mmoja wa viongozi wa juu wa TANU katika siku zake za mwanzo miaka ya 1950

Ali Mwinyi Tambwe anasema aliwahi kupewa fedha nyingi na George Arnautoglu azifikishe TANU zisaidie harakati za uhuru.

Ali Mwinyi Tambwe alinieleza kuwa George Arnautiglu akiwachukia sana Waingereza kwa kuwa wakati ule Ugiriki ilikuwa chini ya utawala wa Uingereza na wananchi walikuwa wanapambana na ukoloni huu.

Hii ikawa sababu kubwa ya George Arnautoglu, Mgiriki kuwachukia Waingereza.

George Arnautoglu kwa kuonyesha shukurani kwa Tanganyika nchi ambayo ndimo alimotajirika aliwajengea watu wa Tanganyika Ukumbi wa Arnautoglu kwa ajili ya shughuli za maendeleo ya Waafrika.

Picha ya pili ni Ukumbi wa Arnautoglu.]
GEORGE ARNAUTOGLU.jpeg
ARNAUTOGLO HALL.png
 
Shukrani sana mkuu kwa historian safi. Huyu nilidhani ni mmojawapo ya viongozi wa Afrika waliokufa katika kupigania uhuru maana walioleta uhuru wote nawajua.
 
Hivi huu ukumbi wa Arnatoglou bado upo active leo hii? Lile eneo wazi la Mnazi mmoja ambamo ndimo ukumbi ulikuwa umejengwa nililiacha likiwa linavamiwa kwa kasi sana miaka ya tisini na elfu mbili nikawa na wasiwasi kuwa wanaweza kubomoa ukumbi huo wenye historia nyingi, kupisha ujenzi wa maghorofa marefu ya kisasa. Ningali kijana niliwahi kuwa nafanyia mazoezi ya ngumi hapo miaka sabini kabla ya vita kuanza.
 
Hivi huu ukumbi wa Arnatoglu bado upo active leo hii? Lile eneo wazi la Mnazi mmoja ambamo ndimu ukumbi ulikuwa umejengwa nililiacha likiwa linavamiwa kwa kasi sana miaka ya tisini na elfu mbili nikawa na wasiwasi kuwa wanaweza kubomoa ukumbi huo wenye historia nyingi, kupisha ujenzi wa maghorofa marefu ya kisasa. Ningali kijana niliwahi kuwa nafanyia mazoezi ya ngumi hapo miaka sabini kabla ya vita kuanza.
Kichuguu...
Ukumbi upo na katika hali nzuri nilipopita kiasi miaka minne uko chini ya City Council na ni ukumbi wa mikutano.
 
Hii ni historia nzuri, nimejifunza, asante kwa kutuelimisha
 
GEORGE ARNAUTOGLU

Ukumbi wa Arnautoglu ulikuwa ukumbi maarufu sana Dar es Salaam katika miaka ya 1950 na shughuli nyingi za kijamii na za kiasi zimefanyika pale.

Jambo la kusikitisha sana ni kuwa hakuna mtu amjuaye mjenzi wa jengo hilo wala hakuna picha yake popote katika hilo jengo.

Wala historia ya George Arnautoglu haijulikani sana na wanoijua watakuambia kuwa alikuwa Giriki tajiri mwenye mashamba ya mkonge.

Hapo chini ni picha ya George Arnautoglu niliyoletewa na Hafidh Kido mwandishi wa Jamvi la Habari kutoka gazeti la Mambo Leo la mwaka wa 1943.

Nimekutana na George Arnautoglu wakati natafiti historia ya TANU siku nilipokwenda kuzungumza na Ali Mwinyi Tambwe aliyekuwa Secretary wa Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika mmoja wa viongozi wa juu wa TANU katika siku zake za mwanzo miaka ya 1950s.

Ali Mwinyi Tambwe anasema aliwahi kupewa fedha nyingi na George Arnautoglu azifikishe TANU zisaidie harakati za uhuru.

Ali Mwinyi Tambwe alinieleza kuwa George Arnautiglu akiwachukia sana Waingereza kwa kuwa wakati ule Ugiriki ilikuwa chini ya utawala wa Uingereza na wananchi walikuwa wanapambana na ukoloni huu.

Hii ikawa sababu kubwa ya George Arnautoglu, Mgiriki kuwachukia Waingereza.

George Arnautoglu kwa kuonyesha shukurani kwa Tanganyika nchi ambayo ndimo alimotajirika aliwajengea watu wa Tanganyika Ukumbi wa Arnautoglu kwa ajili ya shughuli za maendeleo ya Waafrika.

Picha ya pili ni Ukumbi wa Arnautoglu.]View attachment 1519965View attachment 1519959


Shukrani kutujuza hizi historia zilizofuchikana.
 
Mzee wangu Mohamed said Leo nimekuelewa sana,ukisikia kufukua makaburi ndio huku sasa
 
Kichuguu...
Ukumbi upo na katika haki nzuri nilipopita kiasi miaka minne uko chini ya City Council na ni ukumbi wa mikutano.
Asante sana mkuu wangu; nina uhusiano fulani na ule ukumbi wakati wa ujana wangu.
 
Asante sana mkuu wangu; nina uhusiano fulani na ule ukumbi wakati wa ujana wangu.
Kichuguu,

Hapa chini ni John Lennon Memorial, Central Park New York.

Aliyesimama hapo ni mimi.

Uki-zoom utaona kwenye hiyo duara pameandikwa, "Imagine."

Nilipata kujuana na Mmarekani ambae alikuwa rafiki wa Lennon akanionesha nyumba aliyokuwa akiishi na si mbali na hapa Central Park.

Jamaa siku hiyo nilimshangaza kupita kiasi.

Nikamwimbia "Things We Said Today," hii ni nyimbo ya Beatles na nikazidi kumchosha nilipomfahamisha kuwa nikiipiga kwenye guitar langu nikiwa na umri wa miaka 16.

Rafiki yangu huyu akaniambia kuwa siku moja kabla Lennon hajauliwa alikwenda kumuona lakini alikuwa amelala kwa hiyo akazungumza na mkewe Yoko Ono kisha akaondoka.

Huko ndiko nilikotoka na nina uhusiano mkubwa na Arnautoglu Hall udogoni kwangu.
Screenshot_20200729-220831.jpg
 
Hakika historia unazoweka jukwaani zitakuwa na mchango mkubwa kwa kizazi kijacho.

Usichoke kutuhabarisha mkuu
 
Kan...
Amin
Hujawahi kuniboa na maandiko yako..hata ukiteleza naona nitakuwa wa kwanza kukusamehe kuliko kukushambulia ...japo Kuna ambao wanakuona ww Ni mdini lkn hapana huwa uko sahihi kbs japo mm ni mkristo na Ni mkatoriki ..nakuunga mkono Sana Sana kwenye harakati zako
 
Hongera Mzee wetu kwa historia. Ungeandaa kitabu cha picha zote za watu na vitu mbalimbali na maelezo juu yake.



Je huyo tajiri aliishia wapi? Je watoto wake au wajukuu wapo wapi?
 
Hongera Mzee wetu kwa historia. Ungeandaa kitabu cha picha zote za watu na vitu mbalimbali na maelezo juu yake.



Je huyo tajiri aliishia wapi? Je watoto wake au wajukuu wapo wapi?
Akili...
Kuna taarifa chache sana za Arnautoglo sijui kwa nini.

Hata picha yake hakuna.

Sijui kwa nini imekuwa hivi.
 
GEORGE ARNAUTOGLU

Ukumbi wa Arnautoglu ulikuwa ukumbi maarufu sana Dar es Salaam katika miaka ya 1950 na shughuli nyingi za kijamii na za kiasi zimefanyika pale.

Jambo la kusikitisha sana ni kuwa hakuna mtu amjuaye mjenzi wa jengo hilo wala hakuna picha yake popote katika hilo jengo.

Wala historia ya George Arnautoglu haijulikani sana na wanoijua watakuambia kuwa alikuwa Giriki tajiri mwenye mashamba ya mkonge.

Hapo chini ni picha ya George Arnautoglu niliyoletewa na Hafidh Kido mwandishi wa Jamvi la Habari kutoka gazeti la Mambo Leo la mwaka wa 1943.

Nimekutana na George Arnautoglu wakati natafiti historia ya TANU siku nilipokwenda kuzungumza na Ali Mwinyi Tambwe aliyekuwa Secretary wa Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika mmoja wa viongozi wa juu wa TANU katika siku zake za mwanzo miaka ya 1950

Ali Mwinyi Tambwe anasema aliwahi kupewa fedha nyingi na George Arnautoglu azifikishe TANU zisaidie harakati za uhuru.

Ali Mwinyi Tambwe alinieleza kuwa George Arnautiglu akiwachukia sana Waingereza kwa kuwa wakati ule Ugiriki ilikuwa chini ya utawala wa Uingereza na wananchi walikuwa wanapambana na ukoloni huu.

Hii ikawa sababu kubwa ya George Arnautoglu, Mgiriki kuwachukia Waingereza.

George Arnautoglu kwa kuonyesha shukurani kwa Tanganyika nchi ambayo ndimo alimotajirika aliwajengea watu wa Tanganyika Ukumbi wa Arnautoglu kwa ajili ya shughuli za maendeleo ya Waafrika.

Picha ya pili ni Ukumbi wa Arnautoglu.]View attachment 1519965View attachment 1519959
At least hujaingiza udini katika habari hii. Hongera sana Mzee Mohamed!
 
At least hujaingiza udini katika habari hii. Hongera sana Mzee Mohamed!
Isele...
Mimi sijaandika habari za dini.

Nimezaliwa na hawa waliopigania uhuru wa Tanganyika na hawa ndiyo waliounda African Association, Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika (Umoja wa Waislam wa Tanganyika)na TANU.

Hawa ndiyo waliompokea Nyerere Dar es Salaam.

Hawa baada ya uhuru kupatikana historia hii ikafutwa kwa hofu ya kuonekana kuwa Waislam walikuwa mstari wa mbele kupambana na ukoloni.

Mimi nikanyanyua kalamu nikaandika historia hii.

Ikiwa kufanya hivi kwako ni udini hii ni bahati.

Kunipa hongera ati sijaingiza udini ni wewe kutafuta kujifariji.
 
Back
Top Bottom