Gerald Hando apewa onyo baada ya kuhudhuria show ya VINEGA

Gerald Hando apewa onyo baada ya kuhudhuria show ya VINEGA

Mwita25

JF-Expert Member
Joined
Apr 15, 2011
Posts
3,831
Reaction score
1,169
Gerald Hando ameingia kwenye mgogoro na uongozi wa Clouds Radio baada ya kuonekana kwenye shoo iliyoandaliwa na Mbunge wa Mbeya mjini maarufu Sugu. Mtangazaji huyo wa kipindi cha asubuhi cha Power Breakfast ameandikiwa barua ya onyo kali kwa kitendo chake ambacho kimekiuka sheria iliyowekwa hapo awali kuwa hatakiwi mfanyakazi yeyote kuhudhuria onesho hilo ambalo kimantiki lilipangwa kama muendelezo wa vita ya maneno kati ya Sugu na Clouds Radio. Hando hakuwa tayari kuelezea tukio hilo pale alipotafutwa kwa njia ya simu na mpekenyuzi wetu.
 
Wampe onyo na Adamu Mchomvu kwenye facebook wall yake ameweka picha za uzinduzi wa ant virus na picha za sugu kuonensha kumkubali,unajua Mwita sio wafanyakazi wote wa Wafu fm wanafurahia huo unyonyako unaofanywa na ruge,ingawaje hiyo habari yako sio ya kweli hata kidogo.

http://facebook.com/amchomvu (About Adam brother from another mother.... )
 
Hando alishawahi hata kupiga nyimbo moja kutoka ndani ya AntiVirus Part One
 
Huyu Ruge mwenyewe ndio anasema hizi habari..halafu ww Ruge uache kujiita Mwita hilo jina letu wakurya na sisi hatupendi mambo ya kichini chini
 
labda alivaa kofia na tungemuona tungemfanya kitu mbaya
 
Yaani nyinyi ni mazuzu wa mwisho kabisa
 
Gerald Hando ameingia kwenye mgogoro na uongozi wa Clouds Radio baada ya kuonekana kwenye shoo iliyoandaliwa na Mbunge wa Mbeya mjini maarufu Sugu. Mtangazaji huyo wa kipindi cha asubuhi cha Power Breakfast ameandikiwa barua ya onyo kali kwa kitendo chake ambacho kimekiuka sheria iliyowekwa hapo awali kuwa hatakiwi mfanyakazi yeyote kuhudhuria onesho hilo ambalo kimantiki lilipangwa kama muendelezo wa vita ya maneno kati ya Sugu na Clouds Radio. Hando hakuwa tayari kuelezea tukio hilo pale alipotafutwa kwa njia ya simu na mpekenyuzi wetu.

Mwita25 umeanza lini kazi ya uandishi wa habari? kwa upande mwingine jamaa wanamnyanyasa sana pale,kuna kipindi walimpiga chini akawa analalama kwenye facebook sijui wakamuonea huruma wakamrejesha sasa naona kapewa nyingine..ushauri wangu kwake..Kwani wafu fm ni baba yake?

377916_280833345293531_100001006044388_784886_1935174216_a.jpg
 
Hivi kumbe wafanyakazi wa clouds hawana private life baada ya kazi.... hii kiboko
 
Wanahangaika hawa, kwani alikua kikazi?
 
Nilikuwa sijui kama wafanyakazi wa clouds huwa hawana private life baada ya kazi....!!!! sasa sijui hizi ajira za sikuhizi ni ajira ama utumwa lol!!
 
Sheria gani hizo ambazo zinakinzana na katiba ya nchi,yaani kila mtu ana uhuru wa kwenda popote pale maadamu havunji sheria ya nchi na si sheria za Clouds,hayo mambo ni fikra duni haitakiwa yawepo katika ulimwengu wa sasa,sasa hawa clouds wangekuwa na uthubutu fulani wa dola si ingekuwa taabu,haya mambo madogo tu wanakomaa ,mambo mengine ni ya kibnafsi sana kumkataza mtu mzima na akili yake,je kama familia yake ilipenda iende huko na yeye akakataa si ndio mwanzo wa kuvunja amani katika familia,kitendo si cha uungwana kupingana kwa Clouds na Sugu kusiambukizwe na kwa watu wengine,demokrasia ni popote pale sio kwenye vyama vya siasa tu hata huko Clouds,heshimuni haki za wafanya kazi wenu hao ndio ng'ombe watoao maziwa
 
Ila jamaa b12 na mbili alikuwepo maisha club.........tena alikua happy mbaya jamaaa.........sema yule changudoa feee hawezi coz anajikanyaga sana na mambo asiye yajua............. Ila adam mchomvu ni kinega wa siri siri
 
Back
Top Bottom