Gerald pique: vilabu vya ulaya vinavyomilikiwa na serikali za kiarabu zinaharibu soka la ulaya

Gerald pique: vilabu vya ulaya vinavyomilikiwa na serikali za kiarabu zinaharibu soka la ulaya

uwe hodari

JF-Expert Member
Joined
Dec 16, 2022
Posts
4,045
Reaction score
8,608
Sheria ya financial fair play kwa makusudi inafanya siasa kwa baadhi ya vilabu vya barani ulaya

Ukiangalia timu zinazomilikiwa na serikali kutoka huko uarabuni ni km wapo juu ya sheria wanafanya kila wanachojosikia kwasababu hawategemei mapato ya club kuendesha mpira pesa zinatoka uko uarabuni

Hii sio afya kwa mpira wa ulaya alisema Gerald pique mchezaji wa zamani wa manchester united na Barcelona

Ikumbukwe PSG inamilikiwa na serikali ya katari, manchester city inamilikiwa na utawala wa emirates,new castle inamilikiwa na riadhi

Pia manchester united ipo katika hatua za mwisho kumilikiwa na serikali ya Qatar


My take
Inasemekana kuna kampeni zinaendeshwa chini kwa chini kwa vilabu vya ulaya hasa zile ligi kumi bora kuviondoa vilabu vinavyomilikiwa na serikali au vinavyotegemea mapato ya serikali kuendesha club kushiriki mashindano ya UEFA

Tusubri tuone
 
Wishful thinking, hela ni sabuni ya roho, wahenga walisema
 
Acha hela ifanye kazi, hakuna haja ya kuwekeana vikwazo. Kila timu itumie pesa kadiri ya walizonazo ili soka likue zaidi.
 
Halafu aache wivu. Muda wake umeshapita, awaachie wenzake sasa wale hela za Waarabu.
 
Serikali husika zinaangalia pesa na kodi, hayo mengine hayawahusu.

Ukiangalia hivyo vilabu vya waarabu ni City na PSG pekee ndo wanatamba
 
Mpira haupo Sustainable Ni madeni kwa kwenda mbele..., Hata Real Madrid bila Council ya Madrid inayowa-bail out kila kukicha isingeweza kufanya iliyoyafanya enzi za Galacticos...

Anyway sio mpira wa ulaya tu hata timu za ulaya zinaua soka la Afrika kama vilabu vikubwa kwenye nchi vinavyoua soko la nchi husika kwa kununua watu na kuwaweka benchi ili wengine wasiwanunue

Itafika wakati hii formula inayotumika will be the end of football....; Nilisema miaka mingi sana nyuma

 
Back
Top Bottom