Gesi na Mafuta kati ya Tanzania, Congo, Malawi na Mozambique tutaibiana?

Gesi na Mafuta kati ya Tanzania, Congo, Malawi na Mozambique tutaibiana?

Ubungoubungo

JF-Expert Member
Joined
Jul 28, 2008
Posts
2,502
Reaction score
741
Wajameni, naombe kueleweshwa, kwa sasa hivi, mozambique wanagundua gas nyingi sana karibia mara tatu ya hii tuliyogundua hapa tz, na wapo hadi karibia mpakani mwetu, yaani mto Ruvuma. pia kule ziwa Tanganyika wanasema kunaweza kuwa na mafuta na ziwa lile ni jembamba sana na mpaka upo katikati. swali langu ni kwamba, hivi haiwezekani tukaibiwa mafuta au gesi zetu na wenzetu aliotangulia au wakatu ule tunapokuwa tunachimba wote?

Mfano, Mozambique hawawezi kunyonya gas yetu kwenye visima karibu na mpaka wetu wakiwa kwao kule kule and vice versa?

Je, Congo na sisi hatuwezi kunyonyeana mafuta/gas kila mtu akiwa kwake?

Malawi na Tanzania hatuwezi kuibiana kila mtu akiwa kwake?

Au uchimbaji wake huwa unakuwaje kwa anayefahamu, mimi nikiwa pale mtwara siwezi kunyonya chini kwa chini gas iliyoko Mozambique au Wamozambique hawawezi kufanya hivyo wakiwa upande mwingine kule mpakani nasi?

Tukianza kuchimba, ni atakaye wahi ndio atafaidi au haiwezekani kuibiana?


Naongea hivi si ili kutaka sisi tuibe au kwamba tunawaonea wivu, hapana, naongea kwa nia nzuri tu ili kujua kama Mozambique wakitutangulia wanaweza kunyonya gas yetu ambayo vitalu vimekaribiana hata kabla sisi hatujajiimarisha kuichimba?

Maana kule Mozambique wamarekani wanataka kuingia ubia wajenge kituo cha kuprocess gas iwe processed tayari kuanza kuuza Asia na wametenga karibu $15 Billion. Please mwenye kufahamu hili naomba aniweke wazi ili nijue.

Thanks.
 
Conspirancy theories which could easily cause troops to be deployed across the boarders....haaaahaaa. Mi sijui hata inakuwaje ingawa Sadam aliwahi kuvamia Kuwaiti kwa kutumia vigezo kama hivyo.
 
kwani nchi zetu zimeshakaa pamoja kudadili na kukubaliana namna zitakavyochimba gas hizi? ili biashara itakapochanganya tusiingie vitani...manake mi sielewi, naona kama inawezekana tukawaibia wenzetu au sisi tukaibiwa vile....mimi sio injinia.nilisoma arts hivyo naomba maijinia watueleweshe hapa.
 
kivipi? fafanua[/QUOT
Ok! haiwezekani kwasababu kuna sheria za kimipaka... Uliza tena ni kujibu
sitauliza tena kwasababu naona hujui kitu, haujui kujibu maswali na unaonekana wewe si mtu aliyebobea kwenye hiyo fani, hivyo waache wanaojua wajibu. kuna sheria za mipaka zipi ambazo unashindwa kuzieleza? mtu anayejua kujibu kitu atasema kune hiki kwasababu ya hiki na anatoa na mifano, huko ndo kujibu swali. ungekuwa umeeleza hiyo sheria ni sheria ipi, sheria gani inasemaje etc. hapo ungeeleweka. otherwise, have a nice day, waachie wengine wajibu.
 
Haiwezekani

Kwa nini isiwezekane?. Reserve moja ya gesi/mafuta inaweza kuenea kutoka nchi moja hadi nyingine. Kwa vile hizo bidhaaa ni vimiminika vyaweza kunyonywa hata karibu vyote kutoka upande moja tu iwapo reserve imeungana. Gesi kwa mfano haiwezi kuheshimu mpaka ikakataa kusogea inakonyonywa.

Kinachotakiwa iwapo reserve ya gesi imesambaa pande zote za mpaka ni nchi hizo kukubaliana namna ya kugawana.
 
Kwa nini isiwezekane?. Reserve moja ya gesi/mafuta inaweza kuenea kutoka nchi moja hadi nyingine. Kwa vile hizo bidhaaa ni vimiminika vyaweza kunyonywa hata karibu vyote kutoka upande moja tu iwapo reserve imeungana. Gesi kwa mfano haiwezi kuheshimu mpaka ikakataa kusogea inakonyonywa.

Kinachotakiwa iwapo reserve ya gesi imesambaa pande zote za mpaka ni nchi hizo kukubaliana namna ya kugawana.
wewe ndio unaongea point, sio uyo mwingine. sasa hadi sasa watz tumefanya nini kuhusu hili ili tusiibiwe na mozambique?
 
Kwa nini isiwezekane?. Reserve moja ya gesi/mafuta inaweza kuenea kutoka nchi moja hadi nyingine. Kwa vile hizo bidhaaa ni vimiminika vyaweza kunyonywa hata karibu vyote kutoka upande moja tu iwapo reserve imeungana. Gesi kwa mfano haiwezi kuheshimu mpaka ikakataa kusogea inakonyonywa.

Kinachotakiwa iwapo reserve ya gesi imesambaa pande zote za mpaka ni nchi hizo kukubaliana namna ya kugawana.

Unachosema ni kweli, ninacho maanisha Kama Gas au Oil, 100% vipo ndani ya tz kitakacho angaliwa ni mpaka kwa yeyote atakae tokea kujaribu kufanya uvamizi, ila Kama hiyo kitu ipo katika nchi mbili utaratibu ni yule mwenye asilimia kubwa ndio atakua anashika mpini, mfano Burundi 79% na Tanzania ni 21% basi burundil anakua ndio mtabe hapo kwenye ku share
 
Wajameni, naombe kueleweshwa, kwa sasa ivi, mozambique wanagundua gas nyingi sana karibia mara tatu ya hii tuliyogundua hapa tz, na wapo hadi karibia mpakani mwetu, yaani mto Ruvuma. pia kule ziwa Tanganyika wanasema kunaweza kuwa na mafuta na ziwa lile ni jembamba sana na mpaka upo katikati. swali langu ni kwamba, hivi haiwezekani tukaibiwa mafuta au gesi zetu na wenzetu aliotangulia au wakatu ule tunapokuwa tunachimba wote? mfano, Mozambique hawawezi kunyonya gas yetu kwenye visima karibu na mpaka wetu wakiwa kwao kule kule and vice versa? je, congo na sisi hatuwezi kunyonyeana mafuta/gas kila mtu akiwa kwake?, malawi na tz hatuwezi kuibiana kila mtu akiwa kwake?...au uchimbaji wake huwa unakuwaje kwa anayefahamu, mimi nikiwa pale mtwara siwezi kunyonya chini kwa chini gas iliyoko mozambique au wamozambique hawawezi kufanya hivyo wakiwa upande mwingine kule mpakani nasi? tukianza kuchima, ni atakaye wahi ndo atafaidi au haiwezekani kuibiana?....naongea hivi si ili kutaka sisi tuibe au kwamba tunawaonea wivu, hapana, naongea kwa nia nzuri tu ili kujua kama mozambique wakitutangulia wanaweza kunyonya gas yetu ambayo vitalu vimekaribiana hata kabla sisi hatujajiimarisha kuichimba?....manake kule mozambique wamarekani wanataka kuingia ubia wajenge kituo cha kuprocess gas iwe processed tayari kuanza kuuza Asia na wametenga karibu $15 Billion....please mwenye kufahamu hili naomba aniweke wazi ili nijue..thanks.


Mipaka mingi ni imaginary lines au natural fautures (River ect) na inasimama pale kwa minajili ya coordinates tu, lakini geology ni regional extension ambayo haiangalii hii mipaka ya kuwekwa na watu,

Posibilities ya Mafuta ama Gas ya Tanzania kuchukuliwa na Malawi ni kubwa sana, Factor kubwa inayocontrol hayo mafuta na gas ni porous rocks (Permiability), sasa kama kuna Gas/Oil Host rocks ambazo zinaextend kutoka Tanzania na kuelekea Mozambique kuna uwezekano mkubwa kwa Tanzania na Mozambique wakawa wanachukua Mafuta na Oil kutoka kwenye source moja
 
sasa sisi tz tumeshafanya nini katika hili kulinda maslahi yetu?
 
Yaani kama hii kitu inawezekana hizo nchi nyingine zitaimba haleluya kuu cause Tanzania tuna wezi Professionals a.k.a Mafisadi walio kubuhu hapa ni kuwaomba tu waibe kwa niaba ya nchi
 
Yaani kama hii kitu inawezekana hizo nchi nyingine zitaimba haleluya kuu cause Tanzania tuna wezi Professionals a.k.a Mafisadi walio kubuhu hapa ni kuwaomba tu waibe kwa niaba ya nchi

hahaha
 
Kama source ni moja wanafanya approximation eneo la ujazo wa gas iliyo-extend TZ ni kiasi gani vivyo hivyo upande wa msumbiji. Ndio mwamba unaweza kuwa ktk nchi zote mbili ila uvunaji hauta weza vuka ujazo uliokisiwa kuwa upo ndani ya mipaka ya nchi..
Ndio maana unaona gas iliyogunduliwa karibu na mipaka ujazo wake umetangazwa kwa wakato mmoja
 
Kama source ni moja wanafanya approximation eneo la ujazo wa gas iliyo-extend TZ ni kiasi gani vivyo hivyo upande wa msumbiji. Ndio mwamba unaweza kuwa ktk nchi zote mbili ila uvunaji hauta weza vuka ujazo uliokisiwa kuwa upo ndani ya mipaka ya nchi..
Ndio maana unaona gas iliyogunduliwa karibu na mipaka ujazo wake umetangazwa kwa wakato mmoja
duh, hii kitu mbona inanitisha, tusijeibiwa hapa, manake ni nani ataanza kuchimba na ni kwa mitambo yenye nguvu kiasi gani, asije yule anayeanza akanyonya yote tukabaki na mapango tu.
 
Naona mnazipigia hesabu kali hyo gesi wakati wataomkaonufaika ni wale wale Wa cku zote
 
Naona mnazipigia hesabu kali hyo gesi wakati wataomkaonufaika ni wale wale Wa cku zote
mkuu kama kweli hao watu wanatuibia kiasi hicho, hatunabudi kujitia moyo kwani hata wakila walau makombo watadondosha haitakuwa sawa na bure.
 
Ubungoubongo , ni kweli nchi moja ina uwezo wa kuiba gesi au mafuta bila ya kuvusha drilling rig upande wa nchi unayoiibia, mfano Tz tunaweza kuchimba Mtwara na kuwaibia wa Msumbuji na vivyo hivyo kwa Wa Msumbuji.
Ila mtu yoyote ataefanya hii kitu (horizontal drilling mpakani ) lazima itagundulika baada ya muda na atakuwa ame risk maisha ya watu na mali sababu mostly kitachotokea ni explosion baada ya upande wa pili kuchimba kisima sehemu hiyo hiyo bila ya kujua uwepo wa kisima toka upande wa pili wa mpaka.
BTW, Kwa east Africa na Msumbuji, visima vyote vilivyochimbwa mpaka sasa ni vertical wells ambapo hakuna uwezekano wa kuiba kutoka upande wa pili, lakini pindi production itakapoanza horizontal wells zitachimbwa sana na kila mtu itabidi ajirinde kutokana na uwezo wake.
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom