Wadau, juzi nimesafiri na ndugu mmoja, ni mtu mzima wa makamo, miaka sitini hivi na kuendelea.
Njiani tumeongea sana kuhusu kilimo na mashamba. Akasema ana heka hamsini ktk Bonde la Mto Wami, Mkoani Pwani ambako pia Vigogo kadhaa wana mashamba. Amesema kwa sasa wamezuiwa kulima na wanasubiri mchakato wa malipo ya fidia kwa maana imegunduliwa gesi, na ktk shamba lake Wagunduzi wameweka 'beacons' mbili ambapo vitachimbwa visima viwili.
Hizi habari nilikuwa sikuwahi kuzisikia awali, hivi miongoni mwenu wadau, wapo wanaofahamu uvumbuzi huu wa gesi ktk Bonde la Mto Wami?