Gesi sasa kuuzwa kama mafuta

diana chumbikino

JF-Expert Member
Joined
May 29, 2018
Posts
428
Reaction score
368
KAMPUNI 20 za ndani na nje ya nchi zimejitokeza kuwekeza katika ujenzi wa vituo vya gesi asilia vya kuuza mitaani kwa jumla na rejareja kwenye vituo maalumu kama ilivyo kwa vituo vya mafuta. Kati ya kampuni zilizojitokeza kuonesha nia ya kuwekeza katika sekta hiyo ni zile zenye vituo vya kujaza mafuta katika maeneo mbambali nchini.

Hatua hiyo imefikiwa baada ya Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC) mwezi uliopita kutangaza watu binafsi na kampuni zenye nia ya kuwekeza katika ujenzi wa vituo hivyo kujitokeza. Kaimu Meneja wa Biashara za Gesi katika TPDC, Dora Ernest alisema baada ya kupokea maombi hayo ambayo uwasilishaji wake ulikamilika Agosti 19 mwaka huu, watafanya uchambuzi kwa ajili ya kuwaita kuwapa utaratibu wa kufuata.

Alisema uwekezaji huo unafanyika katika maeneo inayopita miundombinu ya gesi katika mikoa ya Mtwara , Lindi na Dar es Salaam huku kukiwa na fursa lukuki katika upatikanaji wa gesi asilia kwa gharama nafuu na kila mahali. Hatua hiyo imetokana na TPDC katika mwaka huu wa fedha kuazimia kujenga vituo vikubwa viwili vya kuuza gesi asilia ili kuwezesha magari makubwa kubeba nishati hiyo kwa kutumia magari maalumu kisha kupeleka katika vituo na kwa watumiaji.

Alisema katika vituo viwili vikubwa vya kusambaza gesi hiyo asilia kwa wateja wa jumla ni Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM ) na kingine Muhimbili kitakachotumiwa pia na wafanyabiashara wa Feri na wataosambaza katika vituo vya kujaza gesi kama ilivyo kwa mafuta. “Wenye nia ya kuwekeza katika sekta hii lazima wawe na magari maalumu ya kubeba gesi (CNG trailer ), na wenye magari hayo wanaweza kuwa wasafirishaji tu mpaka vituoni, eneo kwa ajili ya mradi huo, uwezo wa kifedha, kitaaluma ili kumwezesha kufanya biashara hiyo,” alisema.

Alisisitiza kuwa maombi hayo yatapelekwa Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA) itaangalia maombi hayo kisha ikiwemo vibali maalumu kama kile cha mazingira na mengineyo kisha kupatiwa leseni ili kuanza ujenzi. Alisema wanatarajia utekelezaji wa mradi huo kuanza Agosti mwakani wakati michakato yote itakapokamilika ya ujenzi wa vituo vya kuuza gesi huku wawekezaji wakikamilisha ujenzi wa vituo ili waweze kuchukua gesi na kusambaza.

Aliongeza kuwa, fursa hiyo inakwenda sambamba na fursa nyingine za kubadilisha mfumo wa magari kutoka mafuta kwenda gesi kufanyia matengenezo magari hayo na mengineyo ambayo vibali vyote vinapatikana EWURA.

“Unaweza kuona fursa zilivyo nyingi katika matumizi ya gesi asilimia , kwani kuna wataalamu watahitaika kwa wingi ambao ni wale wanaohakiki mifumo wa CNG kwenye magari ,ambapo kwa sasa nchini yupo mmoja tu,” alibainisha. Alisema licha ya kuwa Chuo cha Teknolojia Dar es Salaam (DIT), kinatarajiwa kusomesha wawili na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam watatu, bado kuna fursa za kusomea katika eneo hilo kwa wale wanaotaka, kwani kwa ukanda wa Afrika Mashariki mitihani yake hufanyika nchini Uganda.
 
Kumbe gesi ipo ya kutosha!
Sasa mazingira yetu kwa ndugu zetu wandengereko mbona yanafanyiwa mtima nyongo?
 
mkuu kituo cha mauzo Muhimbili serious? malori sasa yaingie mjini kuchukua gesi ambayo wangeichukulia Mbagala... hii ni hatari.
Nime log in baada ya kuona jambo hilo hilo nakuta post yako yaani uingize magari makubwa maeneo ambayo tayari yana matatizo ya foleni tena mostly residential areas, hawa watu wazima kweli.
 
Nime log in baada ya kuona jambo hilo hilo nakuta post yako yaani uingize magari makubwa maeneo ambayo tayari yana matatizo ya foleni tena mostly residential areas, hawa watu wazima kweli.
watu wengi(sio wote) wa serikalini huwa hawafikiri,wamezowea kufuata utaratibu uliowekwa na wachache,hili husababisha ulemavu wa kifikra,mtu anafanya kazi ile ile kwa ratiba ile ile kwa miaka 30,lazima alemae kichwani
 
watu wengi(sio wote) wa serikalini huwa hawafikiri,wamezowea kufuata utaratibu uliowekwa na wachache,hili husababisha ulemavu wa kifikra,mtu anafanya kazi ile ile kwa ratiba ile ile kwa miaka 30,lazima alemae kichwani
Surely wana shirikisha maafisa wa mipango miji kwenye maamuzi kama haya maana ata kwa mtu mwenye uelewa mdogo tu wa social geography anaweza ona hiyo siyo sehemu sahihi kwa mazingira.

Isitoshe TPDC wanajua gas ni highly flammable kuweka plant karibu na residential area ni risk na hatari kubwa sana.
 
Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM ) na kingine Muhimbili kitakachotumiwa pia na wafanyabiashara wa Feri na wataosambaza katika vituo vya kujaza gesi kama ilivyo kwa mafuta.

Kwanini iwe maebeo hayo, kwa jinsi watamzania tulivyo hatuoni hayo maeneo ni hatari kwa wanafunzi na wagonjwa? Kwani ardhi imekwusha sehemu zingine?
 
... hii gesi itafaa kwa matumizi ya majumbani? I mean inafaa kwenye meko? Kama ndivyo excellent! Otherwise, bado; tunahitaji kuwakomboa wananchi masikini dhidi ya tatizo la nishati; tunahitaji kuyalinda mazingira yetu dhidi ya uharibifu uliokithiri.
 
... hii gesi itafaa kwa matumizi ya majumbani? I mean inafaa kwenye meko? Kama ndivyo excellent! Otherwise, bado; tunahitaji kuwakomboa wananchi masikini dhidi ya tatizo la nishati; tunahitaji kuyalinda mazingira yetu dhidi ya uharibifu uliokithiri.
Kama una bomba inafaa ila kwenye mitungi sijui kama yafaa
 
... hii gesi itafaa kwa matumizi ya majumbani? I mean inafaa kwenye meko? Kama ndivyo excellent! Otherwise, bado; tunahitaji kuwakomboa wananchi masikini dhidi ya tatizo la nishati; tunahitaji kuyalinda mazingira yetu dhidi ya uharibifu uliokithiri.
Inafaa kwa kutumia pipe, sio mitungi. Ila hata kwa hili kama likifanikiwa litaleta mapinduzi makubwa kiuchumi na kimazingira pia. Kwanza gesi ni rafiki kwa mazingira kuliko mafuta, Pia Taasisi kubwa zitaunganishiwa pipe za gesi hivyo utegemezi wa mkaa/kuni, mafuta yatapungua.

Kiuchumi pesa nyingi itabaki hapa ndani, tutapunguza kuagiza mafuta nje. Hivyo sarafu yetu haitasumbuka sana. Hasa kama mzozo wa sasa huko Saudia kunapelekea bei ya mafuta kupanda.

Nashangaa Kwanini wanachelewesha huu mradi hadi mwakani. Hii wanatakiwa waikimbize haraka. Na waache ubahili kujenga depot za gesi UDSM Au Muhimbili ambako watapata viwanja kwa mteremko kama Jangwani na BRT. Depot zikae mbali na miji na zijengewe miundombinu yote wezeshi ya kurahisisha usafirishaji na usalama.
 
Ni kwa nini miundombinu ya gas isisambazer majumbani, tukaondoa utitili wa haya ma mitungi? Kwani kuna shida hmgani system za usambazaji zikaenea majumbani mwa watu na tukalipia kwa mfumo kama wa umeme?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…