Gharama ya finishing ya nyumba

Bei Mbaya

JF-Expert Member
Joined
Nov 24, 2010
Posts
2,262
Reaction score
847
Amani iwe kwenu

Kwa mwenye uzoefu gharama/vifaa/maduka/design za finishing kwa nyumba yenye 180 sqm

1. Grill za madirisha na milango
2. Kupiga ripu(plasta) na rangi
3. installation ya umeme na plumbing
4. Gypsum na Tiles
5. Masink ya chooni/jikoni
6. Madirisha ya vioo(aluminium au PVC)
7. Milango ya mbao/pvc/soft board
 

Bei ya hizo gharama inategemea uko maeneo gani?, ingekuwa busara ukasema uko maeneo gani ili usaidiwe kiundani,
 
"Bei "ya hivyo vitu ni "mbaya "so pochi yako lazima iwe nene[emoji12]
 
Gharama yake inaweza kulingana au hata kupita gharama ya kujenga boma na kupiga bati
 

Kwa Tiles na ma sink, watafute GoodOne. Bidhaa zao ni nafuu lakini quality ni nzuri pia. Labda kama mambo yamebadilika sasa baada ya Mh Magu kuingia madarakani.
 

Bei ni mbaya naomba nikadirie ingawa mimi nilijengea kijijini
1. nakadiria madirisha yapo kumi madirisha 120000x10 na milango mbao nzuri 250000x10 (milango kumi)
2. 2M
3. Hapo kama 2M
4. Gypsum 2M na ufundi + tiles (mchanga, tiles, maji na ufundi) 3M
5. Inategemea unapenda style ipi?? andaa kama 1.5M na ufundi
6. Madirisha kumi inategemea na ukubwa wa dirisha lako 300,000x10
7. sijaelewa, kuna milango namba moja juu na milango ya mbao, PVC????
 
Kwa Tiles na ma sink, watafute GoodOne. Bidhaa zao ni nafuu lakini quality ni nzuri pia. Labda kama mambo yamebadilika sasa baada ya Mh Magu kuingia madarakani.
Tiles kwa sasa naskia spain na italy ndio vinara kama Thailand,China walivyo kwa Gypsum
 
Reactions: SMU
Tiles kwa sasa naskia spain na italy ndio vinara kama Thailand,China walivyo kwa Gypsum
Ni kweli mkuu ingawa bei zao kubwa sana (mimi naona zaidi wanauzi jina).
 
Tiles kwa sasa naskia spain na italy ndio vinara kama Thailand,China walivyo kwa Gypsum
Sio kwa sasa, spanish tiles ni bora kwa wakati wote, gypsum ni Thailand na india ndio vinara.
Kama ujenzi wako ni wa viwango epuka maneno ya mtaani, tafuta mtaalam.
Nionavyo huwezi kupata msaada stahiki kwani maelezo yako ni very general mkuu.
 
Asante kwa uzoefu wako japo hujazingatia mahitaji ya mteja/mleta hoja. Hivi dirisha la aluminum ni 120,000!!!??
 
Nionavyo huwezi kupata msaada stahiki kwani maelezo yako ni very general mkuu.

nimesema 180sqm kwa mzoefu anaweza jua ripu itakula kiasi gn pia gypsum na tiles za ukubwa gn mkuu
 
nimesema 180sqm kwa mzoefu anaweza jua ripu itakula kiasi gn pia gypsum na tiles za ukubwa gn mkuu
Nikusaidie mkuu, ungeeleza;
1.kiasi cha rooms+ukubwa wake
2.dirisha ngapi na ukubwa wake
3.milango mingapi
4.jiko?..ukubwa wake
5. Dining?.ukubwa wake
6. Lounge?. Ukubwa wake
7.vyoo 2.ukubwa wake?

Hapa utapata makadirio 100%
Mkuu wangu
 
7. sijaelewa, kuna milango namba moja juu na milango ya mbao, PVC????

nashukuru mkuu kwa 1 mpaka 6

hiyo 7 ni either kulingana na experience ya mtu. kuna baadhi ya nyumba milango ya vyumbani ni soft board na vyooni na jikoni ni pvc yenye kioo tinted
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…