Gharama ya Gesi Vs Umeme katika Kupikia kwa Bei za Sasa za Tanzania

Gharama ya Gesi Vs Umeme katika Kupikia kwa Bei za Sasa za Tanzania

Logikos

JF-Expert Member
Joined
Feb 26, 2014
Posts
15,460
Reaction score
24,233
Katika muendelezo wa Makala zangu za Nishati safi ya kupikia; kumekuwa na sintofahamu kuhusu gharama za umeme kwamba ni kubwa sana hivyo kwa kumuwezesha mwananchi ni bora kumpa gesi. Nimeona bora tuangalie ukweli huo kwa kutumia mahesabu yasiyo rasmi....
1kg ya Gesi = 13.6kwh (units)
Kwenye Mtungi wa 15kgs (
ingawa gesi iliyopo kwenye mtungi sio 15kgs kutokana na uzito wa Mtungi)
Kwahio kwenye Mtungi wa gesi wa 15kgs kuna Units Ngapi

13.6kwh x 15 equals to approx = 204 Units
Kwahio Mtungi wa kilo 15 una Units takriban 204

BEI ZA UNITS ZA UMEME KWA BEI YA SASA
.
Bei-ya-unit-moja-ya-umeme (1).jpg

Kama tulivyoona Mtungi wa 15Kgs una Units Takriban 204;
Hivyo basi kwa wale wa mijini ambao sasa wananunua Units kwa Tshs. 292/= wakiamua kununua Kwa Pesa ambayo wananunua watu wa gesi itawagharimu
292/= x Units 204 itakuwa sawa na 59,668/=

Kwa Wale wa Vijijini na wa Tariff 0 ambao Units ni Tshs 100 wakiamua kupikia Umeme badala ya Kununua Mtungi wa Gesi
100/= x 204 Units itakuwa sawa na 20,400/=
Hivyo basi kwa dakika hii Bado Umeme ni Bei rahisi na kwa kumwabia mtu anunue gesi kwamba ndio Nishati ya Gharama Nafuu tunapotoka...

UFANISI WA VYOMBO VYA UMEME
Kwa sasa kuna vyombo vyenye ufanisi wa kutosha kuliko majiko ya umeme ya zamani ya Coils; Kuna vyombo vina ufanisi zaidi ya mara tatu ya mtu anayepikia gesi (kutokana na upotevu wa Nishati); Kuna Slow Cooker za mpaka Watts 100 (Hii ni sawa sawa na taa za zamani za nje ambazo watu walikuwa wanatumia) yaani ni kama kusema kipindi kile unawasha taa ya nje usiku kucha hapo ungeweza kupika mlo wako wa siku.

KUNA UWEZEKANO WA TANESCO KUSHUSHA UNITS
Tukumbuke ya kwamba mara baada ya kumaliza Bwawa la Nyerere kutakuwa na Ongezeko la Uzalishaji wa zaidi ya mara mbili na gharama za uzalishaji huu ni ndogo kuliko ambavyo tulikuwa tunanunua umeme kwa madalali hivyo kuna uwezekano wa kuwawezesha wananchi wakanunua Units kwa chini ya Tshs 100/= na hata kama wasiposhusha kumbuka kwa sasa kutokana na mahesabu mtu wa kijijini au Tariff Zero ni kama ananunua gesi ya 15kgs kwa elfu Ishirini (kama badala ya kununua gesi angetumia umeme)

TUSIFANYE MAKOSA....; Tuanzie Tulipo, Tutumie Tulichonacho, Tufanye Tunachoweza
 
Makala nyingine za Mtiririko Huu:







 
Asante kwa taarifa mkuu,
Inaonekana unafamu mambo ya umeme na mambo yao ya tariff,
Mimi nipo Kijijini lakini umeme nanunua kwa 292 shida inaweza ikawa nini hapo
 
hawawezi kushusha, ikumbukwe bado wanadai wanajiendesha kihasara
Moja hata wakijiendesha kwa hasara umeme / Nishati ni Huduma tunachangia kwenye Kodi Tanesco haipo pale kutuletea pesa / Gawio bali ipo pale kuhakikisha umeme ni affordable na unapatikana kila mahali.., Sasa tujiulize iwapo walikuwa wanajiendesha kwa hasara hapo nyuma sababu ya kununua umeme kwa madalali na wezi kina Dowans sasa hivi Bwawa likiisha na tukaanza kuzalisha wenyewe hio difference inakwenda wapi ?

Mbili Mpaka dakika hii huko kijijini Mwananchi anaweza akatumia equivalent ya elfu ishirini sawasawa na mtu anayenunua mtungi wa gesi kwa elfu sitini (je ni busara tuendelee kumshauri huyu atumie gesi ambayo tunanunua kutoka nje)? JE KWA FAIDA YA NANI ? Yeye, Sisi Wananchi au Wachache pamoja na nchi za nje ?

Tatu tunataka kutumia Kodi zetu ili kufidia bei ya gesi ili tujifanye tunamuuzia mwananchi kwa bei ndogo ?

Unasema hawawezi kushusha kina nani wakati sisi ndio wananchi ambao ndio wenye NCHI ? Binafsi nafanya my civic duty kutoa hizi habari sababu wananchi hawalalamiki sababu hawana taarifa kamili..., na naomba wewe kama una mbunge wako mpatie hili Jarida...

 

Attachments

Asante kwa taarifa mkuu,
Inaonekana unafamu mambo ya umeme na mambo yao ya tariff,
Mimi nipo Kijijini lakini umeme nanunua kwa 292 shida inaweza ikawa nini hapo
Kama matumizi yako ni chini ya Units 75 kwa mwezi chukua risiti chache kuhakikisha matumizi yako wasiliana na TANESCO ili wakuweke kwenye Tariff nzuri zaidi...

Ila zaidi ya hapo fanya your Civic Duty mpatie mbunge wako hii makala na kumuuliza kwanini tusitumie umeme kupikia na mnataka mtuletee gesi ? Yaani ni kama chakula tunacho nyumbani alafu tunaenda kula hotelini

 
Asante kwa taarifa mkuu,
Inaonekana unafamu mambo ya umeme na mambo yao ya tariff,
Mimi nipo Kijijini lakini umeme nanunua kwa 292 shida inaweza ikawa nini hapo
Tarrif zero hutakiwi kuzidi elf kumi kwa matumizi yako ya mwezi
 
Bei ya umeme itashuka tu Kama tutapata waziri mwingine wa fedha.
Mnakumbuka zamani kulikua na kero ya kulipia road licence na driving licence, alipoingia Mpango hizi kero zilitokomea kusiko julikana. Mpango is a true economist.
 
Bei ya umeme itashuka tu Kama Mwigulu ataindoka hazina.
Bei ya Umeme itashuka iwapo Wananchi watapata Taarifa Rasmi yenye ukweli sababu sasa hivi wanapigwa propaganda.., hivyo wananchi wakifahamu ukweli hata siku wakija kupigwa porojo watasema mhhh mbona taarifa zangu zinasema vingine ?

 
Kama matumizi yako ni chini ya Units 75 kwa mwezi chukua risiti chache kuhakikisha matumizi yako wasiliana na TANESCO ili wakuweke kwenye Tariff nzuri zaidi...

Ila zaidi ya hapo fanya your Civic Duty mpatie mbunge wako hii makala na kumuuliza kwanini tusitumie umeme kupikia na mnataka mtuletee gesi ? Yaani ni kama chukula tunacho nyumbani alafu tunaenda kula hotelini

Inakuwa ubishoo
 
Nyie mkumbuke kuwa waziri wa fedha ni Mwigulu ( Mzee wa tozo) hawezi kushusha bei ya umeme maana angependa sana watu wanunue gas kwasababu kwenye gas kuna tozo kubwa. Huyu mtu hayuko pale kwa maendeleo yetu. Kumbuka alitaka kuongeza tozo kwenye gas ya kwetu ambayo tunaitumia kwenye magari ili watu waendelee kununua petrol.
 
Ku
Nyie mkumbuke kuwa waziri wa fedha ni Mwigulu ( Mzee wa tozo) hawezi kushusha bei ya umeme maana angependa sana watu wanunue gas kwasababu kwenye gas kuna tozo kubwa. Huyu mtu hayuko pale kwa maendeleo yetu. Kumbuka alitaka kuongeza tozo kwenye gas ya kwetu ambayo tunaitumia kwenye magari ili watu waendelee kununua petrol.
Kumbe wa ovyo hivi😠
 
Nyie mkumbuke kuwa waziri wa fedha ni Mwigulu ( Mzee wa tozo) hawezi kushusha bei ya umeme maana angependa sana watu wanunue gas kwasababu kwenye gas kuna tozo kubwa. Huyu mtu hayuko pale kwa maendeleo yetu. Kumbuka alitaka kuongeza tozo kwenye gas ya kwetu ambayo tunaitumia kwenye magari ili watu waendelee kununua petrol.
Nyenzo pekee ni kwa wananchi kupata ufahamu...,
  1. Wengi hawajui kwamba gesi ya mitungi ya majumbani sio yetu wala kamwe haitakuwa yetu sababu inazalishwa wakati wa uchimbaji wa petroli na tunaiagiza kutoka nje.
  2. Wengi wanadhani Gesi yetu ya Mtwara nayo inaweza kuwekwa kwenye mitungi hivyo wakiona hii Mitungi wanajua tunakula cha nyumbani na sio kumfaidisha jirani.
  3. Wengi wanadhani Umeme ni gharama kubwa kuzidi gesi (kumbe sio kweli hata kwa bei za sasa vijijini Umeme ni nafuu) na pia hakuna sababu ya maana units ziwe 292 inaweza zikashuka.
  4. Wengi wanaomba na watashangilia iwapo ruzuku itawekwa kwenye gesi ili ipungue bei ila wanasahau kwamba ruzuku ni pesa yao ya Kodi huenda ambayo itabidi itoke kwenye kumletea panadol mzee ili ije kwenye kusaidia kupunguza bei ya gesi ili dalali apate ulaji
Nadhani kwa hili kumlaumu Mwigulu pekee ni kumuonea inabidi tuwalaumu watunga sera wote, wale wanaonufaika kwa mgongo wa watanzania wenzao inabidi tuwalaumu zaidi..., na sisi tunaojua lakini hatusemi nadhani tunastahili lawama (angalau mimi nimesema nadhani nimejotoa kwenye kundi la kulaumiwa)
 
Uzi mzuri
Mzuri sana sema ndio hivyo Elimu kubwa inahitajika.
Mimi nilikuwa natumia Induction cooktop nyumba ya kupanga wakawa wananipigia kelele kwamba namaliza Unit nimewaelimisha waapi ikabidi lile jiko niwapelekee wazee watumie(Wanashukuru linawasave kinoma)
Cha ajabu matumizi ya umeme hapa yamepanda badala ya kushuku na yalikuja kushuka kipindi cha likizo hadi kila mtu anashangaa,now yamepanda tena na mlaji umeme kashabainika ni mama Kibonge aliyerudi toka likizo TV lake plasma la mtumba analowasha kutwa nzima ndio jini linalokunywa umeme
 
Back
Top Bottom