Gharama za kuanzisha kilimo umwagiliaji kwa kutumia visima vya vina virefu

WENYELE

JF-Expert Member
Joined
Apr 2, 2012
Posts
1,433
Reaction score
1,442
Habari wakuu,
Naomba msaada kwa yeyote anayejua gharama za kuanzisha mradi wa kilimo cha umwagiliaji kwa kutumia maji kutoka kwenye visima vya vina virefu.
Naomba kujuzwa gharama za kuchimba visima na mashine za umwagiliaji.
Ahsanteni
 
Kisima peke yake weka milioni kama 20, kwa maana ya kuchimba kama ni eg 100 mts 6-11 mil depending on rock type, umeme kama huna weka like 1.6 mil plus vifaa, fundi, networking ya maji. Simtanks itategemea unataka reservoir ya kujengea au simtanks lakini roughly 2 mil.

bado kupanda kijana.

Hizo gharama nimekupa kwa sababu nina uzoefu nilikuwa na 12 mil nimechemka!!!!!!
 

Duh hizi gharama mbona nzito sana

Hapo bado hujaweka zile drip lines au sprinklers??
 

Ni vyema ungejua kwa kiwango gani anachomwagilia, upatikanaji wa maji mahali alipo. Mfano ukiwa unahitaji lita 500 kwa siku unaweza kutafuta wale wanaochimba kwa mikono ukawapa laki sita ukamaliza mchezo, lakini pia inategemea upatikanaji wa maji wa mahali ulipo
 
ndugu, nimeipenda hii plan yako, nami siku moja natumaini kuwa mkulima mkubwa, bado nazichanga.
 
Mmm na hizi gharama ilikuwa upate maji lita ngapi kwa siku? Kisima ml 20 mbona sijawahi kusikia au nimekosea, means mita 1 inachimbwa kwa ml 2 @ Da Pilly?
Kuna uzi uliongelea sana visima pump na kiasi cha maji utayopata, mdau unataka kuanza na eka ngapi? Pia visima hapa kuna mtu anachimba 65000-100000 kwa mita moja. Lakini wachimbaji wengi roughly ml 3 wanakubali. Hebu utafute uzi wa kisima na pump uone gharama zake
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…