Gharama za kutoa gari bandarini

Habari zenu wadau

Ninaitaji kufahamu jumla ya gharama za kutoa gari bandarini, aina ya Nissan X trail ya mwaka 2007.

Ina 1990cc.
CIF price Ni USD 6361.


Make:NISSAN
Model:X-TRAIL
Body Type:SUV
Year of Manufacture:2007
Fuel Type:PETROL
Engine Capacity:1001 - 2000 CC
Customs Value CIF (USD):5164.00
Import Duty (USD):1291.00
Excise Duty (USD):322.75
Excise Duty due to Age (USD):968.25
VAT (USD):1394.28
Total Taxes (USD):3976
Total Taxes (TSHS):7128968
 
Una hakika?
Last May niliagiza gari nikakutana nayo...

Ndio nina uwakika, naagiza mara gari mara nyingi,
Siku hizi hakuna mambo ya kukadiria, kila kitu kipo wazi kwenye FOMULA.

haata gari lako ukipewa bure au zawadi au ukinunua mabilioni fomula ni moja Ndugu yangu.
 
Ndio nina uwakika, naagiza mara gari mara nyingi,
Siku hizi hakuna mambo ya kukadiria, kila kitu kipo wazi kwenye FOMULA.

haata gari lako ukipewa bure au zawadi au ukinunua mabilioni fomula ni moja Ndugu yangu.

Utaratibu umebadilika lini....
 

Wana calculator mpya isiyo na complication...hata kijana wangu wa chekechea anaweza kuitumia
 
Utaratibu umebadilika lini....

Sikun nyingi utaratibu ndio huo, tokea waanze kutumia FOMULA hakunaga tena longolongo.

na ndivyo ilivyo kwa wajanja tunajitahidi unapoagiza gari CIF iwe kubwa kuliko KODI maana ni bora kununua gari zuri kwa bei mbaya kuliko gari baya kwa bei rahisi na kuja kuwachangia KODI MAFISADI.
 
Kibanga hizo bei unazoweka hapo hazina registration na other charges. Utawalisha watu tango pori
 
Last edited by a moderator:

Unatia mashaka mkuu....
Hiyo calculator naijua....ila inatumika tu endapo bei yao ni kubwa kuliko bei yako!
 
Unatia mashaka mkuu....
Hiyo calculator naijua....ila inatumika tu endapo bei yao ni kubwa kuliko bei yako!

Mkuu naona kama unabisha tu.
 
Mkuu naona kama unabisha tu.

Labda nabisha tu mkuu....labda....
Mara ya mwisho nliagiza gari mei.... hiyo calculator ilikuwepo....
Cif yangu ilikua $2650....calculator ilikua $2000....
Wakatumia $2650 kupata kodi....
 
RR agent wako alikulisha tango pori. Alitakiwa arekebishe invoice isome kama cif ya kwenye database inavyosema. Njoo kwa maprofessional kwenye industry hii tukufanyie kazi yako fair.
 
RR agent wako alikulisha tango pori. Alitakiwa arekebishe invoice isome kama cif ya kwenye database inavyosema. Njoo kwa maprofessional kwenye industry hii tukufanyie kazi yako fair.

Mkuu hapo umesema sawa....
Kwamba unerekebisha invoice....which is illegal mkuu....
Naujua ujanja huo....ila yapaswa mtu aambiwe ukweli kwanza....kwamba kisheria iko hivi......ila kwa ujanja ni hivi...
 
Abra One cif means Cost, Insrance na Freight. Kiswahili maana yake ni gharama ya mzigo, bima ya mzigo ukiwa melini au kwenye ndege au usafiri wowote utakao tumia na gharama ya usafirishaji (nauli)
 
Last edited by a moderator:
Abra One cif means Cost, Insrance na Freight. Kiswahili maana yake ni gharama ya mzigo, bima ya mzigo ukiwa melini au kwenye ndege au usafiri wowote utakao tumia na gharama ya usafirishaji (nauli)

CIF ni nin wapendwa?

Jibu la nappy boy ni sawia...
Kifupi ni gharama ya kufikisha mzigo bandarini au uwanja wa ndege....kabla ya kodi na charges nyingine.
 
Last edited by a moderator:
Kibanga Ampiga Mkoloni
Asante sana Mkuu, naomba mwongozo wako juu ya gari tajwa hapo juu, uwezo wa kuhimili mikiki mikiki, ulaji wa Mafuta, mwingiliano wa spare na magari mengine, upatikanaji wa spare na bei zake.
 
Last edited by a moderator:
Wewe kibanga unapotosha watu. Unapoongelea swala linalohusu hela especially ushuru inabidi ukamilishe mahesabu. Mpe mtu gharama zote kama tansad itakavyotoka. What if huyo mtu aweka budget ya 3.4m halaf inakuja kuongezeka kwenye tansad?? Nakufundisha tena unapompa mtu estimation ya kodi hakikisha umeweka na gharama ya registration na psi ya tra.
 
Kibanga hizo bei unazoweka hapo hazina registration na other charges. Utawalisha watu tango pori

NIkweli mkuu,
Mimi naweeka KODI kamili kamili lakini wakitaka TOTAL yote inadibi waongeze kitu si chini ya Laaki tano.
maana sikuhizi mambo yameoingezeka inabidi ulipie hadi Yard Dryport na sikuhizi naona magari mengi yanapelekwa Mbagala kule.
 


Mkuu wnagu mimi nimesema naweka Hesabu ya KODI tu na sio vitu vingine, hivyo vingine wengine waweke au akaulize huko clearing lakini kwaharaka haraka mtu kitaka nimesema atenge sio chini ya laki tano.
 
Hasante sana Mkuu, naomba mwongozo wako juu ya gari tajwa hapo juu, uwezo wa kuhimili mikiki mikiki, ulaji wa Mafuta, mwingiliano wa spare na magari mengine, upatikanaji wa spare na bei zake.


Mkuu sina uzowefu nalo ila nimelichungulia online naona Bei yake ni ndogo sana sijuhi kwanini labda kwakuwa halijawa maarufu bado, ila nashaka sana na ubora wake maana ni rahisi mnoooo bei yake.
 
Mkuu Kibanga naona hio Nissan inakula milioni hizo 7 na ushei hivi.

Vipi kuhusu mwaka wa registration maana nasikia gari zikiwa nyuma kwa mfano lingekuwa ni mwaka 2006 kurudi nyuma, ushuru ungekuwaje wa juu au ungelingana na huo ulochanganua.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…