Gharama za kwenda China

1. Nauli kwenda na kurudi: USD 1,200
2. Chakula kwa siku: USD 22
3. Hotel Single Room: USD 50
4. Nauli ya mizunguko town: USD 49 (Taxi+Metro+Daladala)
5. Mzigo wako unaotaka kununua: (Na hii tukupe jibu?): Minimum USD3,500

asant sana mkuu kwa ushauri wako,naufanyia kazi
 
mmmhm!!! hivi ni machoyangu au

wewe sio nitonye kweli au? maana hii id mweeeee
Usijaribu kutafuta watu eti kwa sababu wana simu.

Utatapeliwa hapa hapa halafu uanze kutoa mimacho kama umebanwa haja kubwa.

Mjini hapa
 
Last edited by a moderator:
Kwani gharama ya usafiri kwa cbm moja ni bei gani,na je ushuru wanatoza kwa cbm au wanaangalia gharama uliyonunulia mzigo?
 
Habari za jioni wakuuu,mimi ni mfanyabiashara wa nguo aina zote huwa nanunua mzigo wangu Kariakooo, nataka kufata mzigo China gharama zikoje. Natakiwa niwe na sh ngapi ili niweze kununua mzigo wa kutosha anayejua anijuze

Tembelea mitandao ya mashirika ya ndege ya Ethiopian Airlines, Kenya Airways, Emirates, na Fly Dubai. Tutapata namba zao za simu na hata bei kwenye tovuti zao.
 
Ndugu zangu nina swali lingine kama kuna mtu anaweza kutupatia msada
Je unapoleta mzigo unahitaji formalities zipi including certifications ,certificate of origine......
Je China ni rahisi kuzipa unaponunua mzigo.Maana tumeona makontena akichomwa moto kwa madai kwamba bidhaa zao ni chini ya viwango.Mweze ujuzi huu atusaidie kuhusu nini kinahitajika.Je certificate of import or import permit inahitajika?
 
Kwani gharama ya usafiri kwa cbm moja ni bei gani,na je ushuru wanatoza kwa cbm au wanaangalia gharama uliyonunulia mzigo?

CBM charges inategemea na agent anayekusafirishia mzigo.. wengine wanaanzia 400-600USD.... na hapo haijalishi umenunua nguo za aina gani..!
 
inategemea na kiasi cha mzigo.. ukiwa tayari nitafute0715744220

Kweli hapa mjini!!! lakini mbona wenzenu wanaweka information hapa kila mtu anaona!! kwanini nyie mnaficha ficha ??
 
Habari za jioni wakuuu,mimi ni mfanyabiashara wa nguo aina zote huwa nanunua mzigo wangu Kariakooo, nataka kufata mzigo China gharama zikoje. Natakiwa niwe na sh ngapi ili niweze kununua mzigo wa kutosha anayejua anijuze

Wadau wa china, naona PM na maswali juu ya china yamekuwa mengi.

Kutokana na majukumu ya kazi zangu, siwezitoa details zote kwa kila mtu.

Nakaribisha wote mpate consulting service kwenye ofisi zetu hapo tz.

Gharama zitakuwa nafuu, yeah tukiwa charge hela ndiyo mtakuwa serious.

Okay, tips za consulting service ya uchina ni kama ifuatavyo:-

1. General information
2. Visa support
3. Market information in China
4. Clearing and Forwarding
5. Transportation
6. Living and shelter
7. Manufacturers and Suppliers directory
8. Translation
9. Study in China & Chinese Scholarships
10. Business opportunities
11. Product Quality Assurance

Nyote mnakaribishwa.
 

Hongera ujasiliamali huo
 

engineer nilitegemea utatuwekea na anuani ya website ili tuifahamu kampuni vizuri
 
Nifafanulie maana ya loose cargo
 
Nifafanulie maana ya loose cargo

Loose cargo ni mzigo au kifurushi ambacho kwa pamoja hukusanywa na kujaza kontena au ni mzigo usioweza kujaza kontena...

Hii mara nyingi huwa ni kwa wale watu ambao wanataka kutuma mzigo ambao hauenei kontena lote...

Vifurushi vyao hukusanywa na makampuni ya watumaji na kwa pamoja hujaza kontena zima...

Mathalani wewe mkuu ununue nguo za dola 2000 na ukizicompress upate kama 4CBM, ujazo huu ni mdogo kulipia kontena zima hivyo inabidi usubiri au ujumuishwe na mizigo ya watu wengine ili kukamiliza ujazo wa kontena lote...
 
1. Kuna makampuni mengi ya watz ya kusafirisha mizigo. Siwezi weka link zao hapa.

Nakumbuka zamani kidogo kulikuwa na ustaadh mmoja anaitwa Abdallah sijui kama huyu jamaa bado yupo Guangzhou...

Alikuwa msafirishaji mzuri sana wa cargo kwa Wabongo...

Mtu ukiwa na mzigo ulikuwa unafanya kwenda nao godown kwao, mnapimiana CBM na kuandikiwa risiti...

Malipo yalikuwa yakifanywa mzigo ukifika na mambo yote ya ushuru walikuwa wanafanya wao kina Dullah...

2. Ndege za mizigo zipo pia hasa pale Guangzhou city, china

Wapo pia Watanzania wanaosafirisha kwa ndege na gharama ya usafirishaji hutegemea uzito...
 

Cubic meter

Ni ujazo wa urefu, upana na kimo kutengeneza mita moja ya ujazo...
Asante sana Watu8 now nimepata darsa murua hapa,
 
Last edited by a moderator:
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…