Jamani mitandao yetu ya simu imebadili gharama zao kimya kimya. Mimi natumia airtel, wamebadili vifurushi vyao kwa kupunguza dakika walizokuwa wakitoa. Kwa maneno mengine wameongeza gharama.
Mfano, kifurushi cha wiki walichokuwa wanauza kwa Tsh1995 tulipata dk60 SMS 700 na 175MB. Sasa hivi kwa bei ileile tunapata dk 40, SMS 500 na 150MB.
Mitandao mingine hali ikoje? Naombeni michanganuo huko pia maana nataka kufanya utafiti mdogo hapa kwa nia njema kabisa.
Asante