ccm HIYO.....Jana siku ya jumatatu 26.08.2024 nilimsindikiza mgonjwa Muhimbili akaandikiwa kipimo cha Ultrasound tulivyoenda kulipia tumekuta bei imepanda zamani ilikuwa Tsh 25,500 lakini jana tumelipishwa 35,500,je ina maana na vipimo vingine navyo vimepanda bei au imekaaje hii.
Je hali ikiwa hivi sisi tunaolipia matibabu by cash tutatoboa kweli?
Mwenyekiti wao anagawa hela kwa machawa huku hali ya wananchi ikizidi kudidimia.ccm HIYO.....
Wananchi tumeshindwa kum discipline na hayo ndiyo matokeo yake.Mwenyekiti wao anagawa hela kwa machawa huku hali ya wananchi ikizidi kudidimia.
Basi waharakishe mchakato wa ule mpango wa bima ya afya kwa wote nasi tusio waajiriwa tukate hizo bima maana hizo za sasa wanazoziita za vifurushi hazina maana yoyote kwa sababu hazibebi gharama za vipimo vingi.Toka gharama za bima zishushwe, cash imepanda ili ku compensate hilo gap