Ghorofa la Posta Mji Mkongwe Zanzibar lakodishwa kuwa "night club"

Baraghash

JF-Expert Member
Joined
Dec 18, 2012
Posts
2,713
Reaction score
1,790
MJI Mkongwe wa Zanzibar unadaiwa kuwa katika hatari ya kuondolewa kwenye ramani ya Hifadhi ya Urithi wa Kimataifa.Kwa kukabiliana na hali hiyo, Mamlaka ya hifadhi na Uendeshaji wa Mji Mkongwe Zanzibar imewataka wakaazi na taasisi zilizomo kwenye mji huo kuzingatia taratibu za mji huo ili kuepusha kuondolewa kwenye urithi wa dunia.

Lakini katika jambo la kusikitisha sana viongozi wajanja wa Shirika la Posta wanakwenda kinyume na hayo na imefikia hatua kuwakodisha(foreigners) wataliana(kulipia kwa dola)kwa kulifanya jumba hilo lenye urithi mkubwa wa kihistoria kugeuzwa kuwa klabu ya Pombe na chakula wakati wa mchana na " night club"wakati wa usiku. Yanayofanyika wakati huo wa usiku sikaraha kwa silka na mila ya wazanzibari tu lakini ni kero kwa majirani. Malalamiko yamefikishwa kwa sheha lakini yameshindwa kudhibitiwa kutokana na taasisi hiyo kuwa ya muungano.

Baya zaidi ni kuwa Jumba lenyewe ni la karne na limechoka na linahatarisha maisha ya watu.
Shirika la Posta ni la muungano na linaratibiwa kila kitu kutoka Dar es Salaam na ndio wamiliki wa jengo hio kisheria.
 
Si zile huduma zetu zitakuwa zinapatikana lakini
 
Jumba La Maajabu Aliloishi Sultan Pale Mji Mkongwe Ndiyo Hali Yake InakuwA Tete
 
Huku kwetu zanzibara sera ni kuongeza mapato ninyi mnaishi km huku!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…