Its started miaka ya tisini na kitu, enzi hizo Niko form four weruweru secondary.
Kama mjuavyo mwezi WA kwanza shule hufunguliwa, wanafunzi ni kipindi chao kurudi shuleni hivyo usafiri pale UBUNGO unakuwa mgumu sana.
Basi siku hiyo nikaamka asubuhi na mapema kwenda kukata ticket kwa ajili ya safari kesho take, mabasi yote yalikuwa yamejaa na sikuwa na tumaini LA kupata basi.
Miongoni mwa wahanga wa adha ya usafiri siku hiyo alikuwa ni huyu kijana mtanashati mbele yangu.
Kijana akanyanyua simu yake ya Mobitel, akapiga namba Fulani, kisha akaanza kuongea kwa kudeka na kwa sauti yenye utoto WA kishua akilaumu ugumu WA usafiri.
Baada ya dakika chache akakata simu na kunigeukia, akasema "Usijali, kesho tutasafiri wrote, baba atatupeleka."
Nikashukuru.
Akaniambia wanaishi Upanga East, Seaview, niwaelekeze nyumbani watanipitia.
Niliwaekekeza kwetu, kuwa nakaa mjini, Samora Avenue KWENYE flats za Railway.
Nikawapa namba yetu ya landline, sikuwa na simu ya mkononi.
Nilipofika nyumbani niliwahulisha namna usafiri ulivyo mgumu na jinsi nilivyobahatika kupata lift, na kesho asubuhi safari ya Moshi inaanza.
Wazazi hawakuwa na kinyongo wala pingamizi, waliniamini sana hasa kwakuwa nilikuwa mnyenyekevu na kichwa darasani.
Tupate matangazo mafupi kutoka kwa wadhamini.
Pata appetizer nzuri ya MATUNDA na mbogamboga organic.
Piga simu 0652825751, 0717/0767-454455, 0682 013199